Bado siamini kama wote walikufa

Bado siamini kama wote walikufa

Mwanzoni, sikuamini kwamba walikuwa wamekufa. Kwa hakika nikiwaza sana namna gani wote waliweza kufa kwa pamoja... Wakati pale nilitambua kwamba ilikuwa kweli wamekufa, bado ilinichukua muda kitambo kuamini kama kweli walikua wamekufa.
Ama kwahakika, hili ni tukio lililo niliumiza sana na kunifanyia majeraha makubwa moyoni, na katika maisha yangu sikuwahi kuumizwa na kujeruhiwa moyoni kwa namna ile...
Siku zilivyo zidi kusogea nilijisikia kama kuishi bila wao haina maana. Kwa muda wa miezi mingi, nilikuwa ninalia kila siku.. Nilijilaumu kwa sababu niliacha mtu mwingine aendeshe gari lile kwasababu tu nilichelewa kurudi kutoka kwenye starehe.... Pengine hawangekufa ikiwa ni mimi ndie ningekua naendesha gari lile.
“Miaka kumi na sita imepita, na nimerudilia maisha yangu ya kawaida. Lakini, kifo chao kimeacha jeraha na sonona katika moyo wangu. Hiki ni kidonda ambacho hakijapona mupaka sasa, kwa babu nahisi kama pengine nisinge enda kwenye starehe, watu hawa wasinge kufa"


View attachment 889137
Mwendo mkali unaua.Pikipiki ilikuwa katika mwendo mkali na gari ilikuwa kwenye mwendo mkali pia.Ukaguzi wa eneo la tukio pamoja na vyombo husika itasaidia kupata ukweli mzima.
 
Mwendo mkali unaua.Pikipiki ilikuwa katika mwendo mkali na gari ilikuwa kwenye mwendo mkali pia.Ukaguzi wa eneo la tukio pamoja na vyombo husika itasaidia kupata ukweli mzima.
Hauja kosea chief....
Hii ajali inaonekana wazi kwamba ili sababishwa na uzembe, pamoja na mwendo kasi
 
Waliokufa ni familia yako au?
Haikua familia mkuu, bali walikua watu wangu wa karibu.... na mbaya zaidi nilikua ndio nimechukua gari la mkopo na hata mwezi moja ilikua haijapita haki
 
Inaonekana umeunganisha PICHA NA STORY yako...kwnz hiyo gari na hiyo PIKIPIKI inaonekana sio hapa kwetu nyumbani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom