Mkuu, kuna ukweli ambao team marekani huwa wanakuwa wagumu wa kukubali. Kwanza kabisa Vita ya kumtoa Hittler ni mrusi ndo alifanya kazi kubwa sana. America alikuja baadaye wakati mziki unaishia. Pia kwenye kuiba technoloji ya siraha enzi hizo kutoka Germany hasa kombora za rocket, russia ndo alikuwa wa kwanza kupata tech hiyo na wataalam wa hittler ingawa Marekani nao walichukua pia.
Kuna kipindi Russia ilishasema ina monitor sayansi yote ya dunia kwa ujumla na haitaruhusu nchi yoyote iwe juu kitechnolojia kuizidi. Mambo ya ubabe, kuiba mafuta ya waarabu kuwait, iraq, libya ni mambo ambayo anayafanya marekani lakini siyo kuwa juu kisanyansi kuizidi russia.
Russia ndo wa kwanza kwenda kwenye space, na ndo ana vituo huko mwezini hata kuwauzia wengine mafuta nk.
Ki inteligensia jamaa wako mbali sana na wana watu wao all over europe na marekani. Lakini ni ngumu sana CIA au FBI kuingia ndani kabisa russia.
Ki electronic na internet russia ni rahisi sana kuingia kwenye system za marekani kuliko marekani kuingia kwenye system zao. Ndo maana unaona kila kukicha marekani analia kama mtoto kwamba russia anaingilia mifumo yao, kuanzia mifumo ya maji, umeme, etc.
Kwa hiyo kiualisia huwezi kulinganisha tech ya russia na marekani. Lakini ki propaganda na siasa ndo unaona kama marekani wapo juu