Tuseme tu ukweli nchi hii haitaenda mbele hata kidogo kama huyu mama ataendelea kuwa rais. Yaani kwasasa nchi haijijui iko chini ya nani maana aliyejishindisha ameingiwa na woga haijawahi kutokea, jeshi nalo ni kama halielewi linatakiwa lifanye nini.
Kwahiyo tunajikuta nchi iko chini ya rais wa kujitwalia na jeshi. Japo makundi yote yanaogopana vibaya mno.
Fanyeni hivi wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama mtoeni huyu mama nchi iendelee kama kawaida kama tutaenda tunavyoenda hakuna kitakachofanyika. Nyinyi mliapa kulinda maslahi mapana ya taifa na si matumbo yenu acheni kutufanyia upumbavu yanapokuja maslahi mapana ya taifa.
Nchi kwanza mtu au kikundi cha watu bila kujali ukwasi walionao yanapokuja maslahi mapana ya nchi wao wawe wa baadaye sana.
Mtaonekana jeshi la ovyo na la kipumbavu sana mkiendelea kuichekea hii serikali iliyoiba kura zote za wabunge na rais. Hilo tu na wizi mkubwa namna ile lilitosha kuiweka kando hii serikali. Kuweni serious basi acheni uboya nyinyi ni imara sana na huu ndo wakati wenu wa kulilinda taifa hili pendwa ambalo ndiyo nyumbani kwao na mlima Kilimanjaro, Serengeti National Park nk, Tanzanite,ziwa Victoria na mengine mazuri mengi.
Mungu ibariki Tanzania
Mungu wabariki watanzania.
Nawatakia utekelezaji mwema.