GE2025 'Babalevo' amejiharibia, amepiga teke fuko la pesa!

GE2025 'Babalevo' amejiharibia, amepiga teke fuko la pesa!

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Clayton Chipando almaarufu kama Babalevo, aliyekuwa mtiania na mgombea wa ndani wa Ubunge kwa tiketi ya CCM Jimbo la Kigoma Mjini amejiharibia. Kama ulikuwa ni mtego, umemnasa.

Kitendo chake cha kumpora 'kihuni' karatasi ya matokeo Katibu wake wa CCM wa Wilaya, aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi wa mgombea wa CCM jimboni humo, ni ukosefu wa nidhamu na ukiukwaji mkubwa wa taratibu za chama chake-CCM.


Soma >>> GE2025 - Baba Levo akinukisha, ataka kura zihesabiwe upya

Alipaswa kuwa mtulivu na msikivu. Kama kuna malalamiko yoyote aliyonayo, alipaswa kuyawasilisha kwa viongozi wake kwa mujibu wa taratibu za chama chake. Taarifa bado zitawasilishwa Kamati Kuu na uamuzi wa nani hasa ni mgombea wa CCM Kigoma Mjini utafanywa huko.

Ni kwakuwa hazijui taratibu za kichama au alikuwa na ajenda zake zilizojificha kuhusiana na uhalali wa uchaguzi ndani ya chama chake? Si mara moja wala mbili, Kamati Kuu ya CCM imewahi kuwapitisha walioshika nafasi za pili, tatu na hata nne kwenye kura za maoni. Fujo zake zimemharibia kabisa.

Pia soma >> GE2025 - Baba Levo aangukia pua, Ng’enda aibuka mshindi Kigoma Mjini kwa kura 2,168 dhidi ya 2,080
 
Let him cooking


FB_IMG_17535974231894628.jpg
 
Mihemko.
Ni tatizo kubwa, kavumilia kote huko kaja kuharibu mwishoni.

Angetulia tu, asubiri eidha apitishwe na kamati kuu au apate teuzi ndani ya chama au serikali.
 
Baba Levo ameshinda kihalali inabidi apewe ushindi wake halali na ninachojua huyo Baba Levo atateuliwa na Sisiemu kwakuwa katumwa na Diamond sio kwamba kajituma na Diamond anawasaidia sisiemu katika mambo yao ya kampeni so is about win win game.

Swala la integrity litajulikana Ila huyo Mbunge aliyekuwa nafasi ya kwanza hawezi kushinda .
 
Baba Levo ameshinda kihalali inabidi apewe ushindi wake halali na ninachojua huyo Baba Levo atateuliwa na Sisiemu kwakuwa katumwa na Diamond sio kwamba kajituma na Diamond anawasaidia sisiemu katika mambo yao ya kampeni so is about win win game.

Swala la integrity litajulikana Ila huyo Mbunge aliyekuwa nafasi ya kwanza hawezi kushinda .
Bila hata kutumwa, nadhani pia record yake inambeba pale Kigoma
 
Back
Top Bottom