GE2025 'Babalevo' amejiharibia, amepiga teke fuko la pesa!

GE2025 'Babalevo' amejiharibia, amepiga teke fuko la pesa!

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
Baba Levo ameshinda kihalali inabidi apewe ushindi wake halali na ninachojua huyo Baba Levo atateuliwa na Sisiemu kwakuwa katumwa na Diamond sio kwamba kajituma na Diamond anawasaidia sisiemu katika mambo yao ya kampeni so is about win win game.

Swala la integrity litajulikana Ila huyo Mbunge aliyekuwa nafasi ya kwanza hawezi kushinda .
Baba levo acha kujipa matumani hewa šŸ˜† umeshindwa kupenya tulia fanya mambo mengine.
 
Huyo hata uteuzi ndo basi hapati tena discipline ndogo..NI aidha afanye maamuzi magumu agombee upinzani anashinda mapema Sana asubuhi au arudi wasafi kwa boss wake diamond
Hujui ushindi anaamua ccm sio ishu ya kura
 
Clayton Chipando almaarufu kama Babalevo, aliyekuwa mtiania na mgombea wa ndani wa Ubunge kwa tiketi ya CCM Jimbo la Kigoma Mjini amejiharibia. Kama ulikuwa ni mtego, umemnasa.

Kitendo chake cha kumpora 'kihuni' karatasi ya matokeo Katibu wake wa CCM wa Wilaya, aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi wa mgombea wa CCM jimboni humo, ni ukosefu wa nidhamu na ukiukwaji mkubwa wa taratibu za chama chake-CCM.

Alipaswa kuwa mtulivu na msikivu. Kama kuna malalamiko yoyote aliyonayo, alipaswa kuyawasilisha kwa viongozi wake kwa mujibu wa taratibu za chama chake. Taarifa bado zitawasilishwa Kamati Kuu na uamuzi wa nani hasa ni mgombea wa CCM Kigoma Mjini utafanywa huko.

Ni kwakuwa hazijui taratibu za kichama au alikuwa na ajenda zake zilizojificha kuhusiana na uhalali wa uchaguzi ndani ya chama chake? Si mara moja wala mbili, Kamati Kuu ya CCM imewahi kuwapitisha walioshika nafasi za pili, tatu na hata nne kwenye kura za maoni. Fujo zake zimemharibia kabisa.
Hao ndio wahuni wanao semwa. Yaani wamesha jiona wao ni kila kitu. Chawa ni hatari
 
Baba Levo ameshinda kihalali inabidi apewe ushindi wake halali na ninachojua huyo Baba Levo atateuliwa na Sisiemu kwakuwa katumwa na Diamond sio kwamba kajituma na Diamond anawasaidia sisiemu katika mambo yao ya kampeni so is about win win game.

Swala la integrity litajulikana Ila huyo Mbunge aliyekuwa nafasi ya kwanza hawezi kushinda .
Unajuwa alivyokilea chama wakati wa utawala wake?
 
Kuna sehem nimesoma eti Mungu alifanya uumbaji na siku ya saba alipo maliza na kupumzika, shetani akaiba udongo na kuumba wajumbe 🤣
 
Baba Levo ameshinda kihalali inabidi apewe ushindi wake halali na ninachojua huyo Baba Levo atateuliwa na Sisiemu kwakuwa katumwa na Diamond sio kwamba kajituma na Diamond anawasaidia sisiemu katika mambo yao ya kampeni so is about win win game.

Swala la integrity litajulikana Ila huyo Mbunge aliyekuwa nafasi ya kwanza hawezi kushinda .
Kwanini asishinde na ccm wako peke yao kwenye huo uchaguzi.

Useme kwasababu atagombea na Zitto kabwe ccm B hivyo ccm wanao uwezo kumpa Zitto jimbo ili kuhalalisha wizi wao.

Ili waseme act wameshinda hivyo kuondoa dhana ya upinzani kulalamikia kanuni za uchaguzi.
 
Back
Top Bottom