KIGENE
JF-Expert Member
- Jan 22, 2011
- 1,552
- 813
Siku moja jamaa alitoka zake safari ya mbali baada yakulakiwa na mtoto wake mdogo mazungumzo yao yalikuwa hivi Mtoto: Baba mbona safari hii umekaa muda mrefu? Baba: Mwanangu miangaiko ilikuwa mingi mno Mtoto: Lakini baba unajua nana alikuwa analala na mama kipindi chote ulipokuwa umesafiri?Baba: Sijui tafadhari niambie kabla mamako hajarudi Mtoto: Siwezi kutoboa siri yangu mpaka uninunulie kibaisikeli Haraka baba mtu akaenda na kukileta kibaisikeli na akamkuta mwanae na mkewe wakiwa sebuleni Mazungumzo yakaendelea hivi Mtoto: Baba kwa vile umeniletea kile ulichonihaidi siku nyingi bila mafanikio sina budi nikwambie leo ni nani huwa analala na mama ukiwa safari niseme au nisiseme Mama: Mwanangu nakusihi sana usiseme Baba : Sema mara moja Mtoto: Simwingine bali niiíí ni miii mimi hapa mwanenu mpendwa!