Baba mkwe, mahari hii imenishinda

Mdoa mada na Mimi yalishanikuta kama yako ila Mimi sio kwa mchaga,nilitajiwa kwa USD 3000,sawa na milioni 6 na laki 6,nimewapa tu zawadi ya mjukuu na nikajiongezea mihula miwili ya kwenye kiti cha ubaharia!
Sheria yangu niliyojiwekea mahari hata niambiwe Trilioni moja sitatoa zaidi ya laki 5 na itolewe na VAT kabisa hapo sitaki kukwepa kodi,na risiti nipewe ili ikitokea dharura mahakama wajue pa kuanzia
 
Pole sana Mkuu
Nakumbuka nilipotaka kujua mahari ni kiasi gani
Mahari ni zawadi ya Bi harusi hivyo nilitakiwa kumuuliza mhusika mwenyewe.
Akanitajia Mahari haifiki hata 100k
Nikamuuliza Mara ya pili hii ndio mahari yako?
Akajibu vipi una pesa nyingi nikutajie mzigo mkubwa
Aaah hapana Mamiloo. Basi nikabeba Toto biiiichiii kwa elfu 90+

Hii utaikuta tu katika familia yenye kushikamana na dini
 
USILOLIJUA NI USIKU WA GIZA. Kulipa mahari yote kwa wachaga ni dharau. Hiyo 5m waliyokutajia wanajua kabisa wewe huwezi kuilipa. Pia hata hiyo ya chakula uliyotoa ungesema hauna siku ingepita. Kwa ushauri wangu kama huyo mwanamke unampenda kubali deni lipa unapoweza utapata baraka za wazazi na uende na wazazi wako usiende kihuni. Kulipa mahali inakua kama umemnunua ila ukishindwa kulipa yote sio kosa na inawapa wakwe nguvu angalau ukileta zako utafikiria hata mahari hujamaliza.
Mwisho kama ukitaka kuo uchagani ukitajiwa mahari ni elfu 50. Usije ukalipa yote hapohapo watakuona kiburi. Kubali utailipa kidogokidogo ila usikimbie
 
Biashara ya utumwa bado ipo kimtindo. Haijalishi utalipa kidogo kidogo mpaka uzeeni bado amount ni ile ile, 5ml, unanunua kitega uchumi? Na hiyo kurudisha garama 280k duh hapo noma.
 
Ya nini kujisumbua na madeni wakati iko mikoa unapata mke hata kwa aya moja tu kwenye quran
 
Dah poa braza tunaheshimu maamuzi yako, usirudi tu ukweni, sio sababu ya mahari kubwa ila kuombwa kurudisha gharama ya tafrija ile sio sawa kabisa maana we hukuwaambia waandae tafrija ila ni wao kama wao
Sure hapa hawajamtendea haki mwana.Wamezingua kwa kifupi.Mm nisingerudisha maana akil yangu naijua mwenyewe jinsi ilivyo faster kufanya michanganuo na kuchukua maamuzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…