Baba mdogo anakula kitimoto hadharani

Mawardat

JF-Expert Member
Joined
Apr 27, 2021
Posts
25,997
Reaction score
137,035
Wassalaam.

Ni hivi upande wa baba wapo mseto lkn %95 ni wakristo, %5 ndiyo siye,

Baba mdogo kaja nyumbani kutusalimia na ana wiki sasa,

Shida ba mdogo anapenda kula kitimoto balaa,

Yaani chai yake ni kitimoto na pepsi,

Shida anakuja nacho ndani, kama leo kamtuma boda amletee na muda boda kaja ba mdogo anaoga na akaniambia nikampokelee

Na kumuambia asilete ndani nitaanzaje??

Hawezi kuona tunamnyanyapaa??

Au hatumtaki??

Je anafanya kusudi?? maana anaelewa kuwa hatutumii,

Naombeni ushauri nitumie njia gani kumfikishia kuwa hatupendezewi na hii tabia?

NB. Mama hajui maana si mtu wa nyumbani.


MREJESHO..............................
______________________________

mchana huu,nimemwambia ba mdogo

Si unajua imani tumetofautiana,akasema ndiyo,

Nikamwambia hivyo hiyo nyama unayokujaga nayo siye hatutumi,uwage unakula huko mabandanii


Akasema sorry kwanini usingenishtua? maana nilijisahau mwanangu,NISAMEHE,


Nimemwambia haina shida baba kuwa na amani,
 
kwani wewe ni Muislam au haupendi tu Kitimoto?
Namaanisha kama wewe ni Muislam, muite Pembeni umueleze kuwa familia yako haitumii na kwa imani yako haifai kuleta hapo nyumbani hivyo unamuomba asifanye hivyo.
Akileta tena, itakuwa ni dharau ya hali ya juu nyumbani kwa mtu hivyo mtengenezee mazingira ya kuondoka chap!
 
Me muislam,

nashukuru kwa ushauri.
 
Pole mkuu.Basi kama ni hivyo sioni haja ya wewe kumuogopa ongea na mzazi aliyebaki atarekebisha tatizo,ukute kabla haujazaliwa ba mdogo alishazoea uhuru alionao mpaka muda huu. Kuna tabia huwa hazianzi ghafla tu mkuu
Loooh

Baba hayupo,kashatangulia mbele za haki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…