TOFU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2012
- 573
- 196
Wakuu nawasalimu kwa heshma na taadhima ...
Nianze kwakusema Baba alimuacha Mama na kuamua kuwa kijana wa Mambo mengi
Katika maangaiko yake kwa bahati mbaya akapata maambukizi ya VvU na kupelekea kuugua sana
Alipoenda kucheki afya aligundua tayari ni muadhirika wa UKIMWI
Ilhali Mama hakuwa na Maambukizi yoyote
Kipindi cha kwanza aliugua sana
Mama hakumuacha ila alimuuguza Mume wake mpaka alipopata nguvu
Kwa kumbukumbu zangu Baba alilala kitandani kama miaka saba (7) akiwa mgonjwa na kipindi chote hichi aliugizwa na Mke wake ambae ndio Mama mzazi
Balaa lilianza pale Baba alipopata nguvu na kutaka kuendelea na Mama ilhali alimuacha Mama kipindi akiwa mzima
Mama akagoma katu katu
Kila mmoja akawa na chumba chake japo wakawa wanaishi nyumba moja
Wachungaji wakajaribu kutatua mgogoro bila mafanikio
Ndugu nao wakajaribu bila mafanikio
Kwakuwa kulikuwa na ugomvi wa kila siku basi sisi watoto tuliamua Mama aishi nyumba tofauti japo kwenye boma moja
Baba akaamua kuleta Mwanamke mwingine
Mbaya zaidi yule Mama aliyeletwa kawa adui wa Mama pamoja na sisi watoto wake
Mpaka yale maeneo ambayo mzee alitugaia kama sehemu tutakazojenga makazi yetu nayo akabatilisha na kusema watoto tumeungana na Mama ili kumuangamiza yeye
Baba anataka Mama aondoke kabisa kwenye lile Boma au nyumba anayoishi kwa ushawishi wa Mama mpya aliyemleta!
Kiujumla sisi watoto wote ni watu wazima kila mmoja anajitegemea na hakuna tunachoitaji kutoka kwa Baba mzazi ila hatupo tayari kuungana na Mama wa kambo ili tumfurahishe Baba
Maana watoto tunaonekana wabaya kwasababu tu tunaonekana tupe upande wa Mama
Wakuu wangu,nahitaji ushauri wenu kwani naamini wengi humu mmenizidi kwa vingi ..
Jeh! niungane na Baba kwenye maamuzi yake ili anipe Mali au niendelee kuketi upande wa Mama kwasababu bado naona Mama hakutendewa haki
Najua fika mimi ni Mwanaume na sinui nitadondokea wapi ila naheshimu utu kuliko kitu ...!!
Kwa heshima zote ndugu zangu naomba kuwasilisha japo uwandishi wangu sio wakuridhisha ila natumai nimeeleweka ...
Nianze kwakusema Baba alimuacha Mama na kuamua kuwa kijana wa Mambo mengi
Katika maangaiko yake kwa bahati mbaya akapata maambukizi ya VvU na kupelekea kuugua sana
Alipoenda kucheki afya aligundua tayari ni muadhirika wa UKIMWI
Ilhali Mama hakuwa na Maambukizi yoyote
Kipindi cha kwanza aliugua sana
Mama hakumuacha ila alimuuguza Mume wake mpaka alipopata nguvu
Kwa kumbukumbu zangu Baba alilala kitandani kama miaka saba (7) akiwa mgonjwa na kipindi chote hichi aliugizwa na Mke wake ambae ndio Mama mzazi
Balaa lilianza pale Baba alipopata nguvu na kutaka kuendelea na Mama ilhali alimuacha Mama kipindi akiwa mzima
Mama akagoma katu katu
Kila mmoja akawa na chumba chake japo wakawa wanaishi nyumba moja
Wachungaji wakajaribu kutatua mgogoro bila mafanikio
Ndugu nao wakajaribu bila mafanikio
Kwakuwa kulikuwa na ugomvi wa kila siku basi sisi watoto tuliamua Mama aishi nyumba tofauti japo kwenye boma moja
Baba akaamua kuleta Mwanamke mwingine
Mbaya zaidi yule Mama aliyeletwa kawa adui wa Mama pamoja na sisi watoto wake
Mpaka yale maeneo ambayo mzee alitugaia kama sehemu tutakazojenga makazi yetu nayo akabatilisha na kusema watoto tumeungana na Mama ili kumuangamiza yeye
Baba anataka Mama aondoke kabisa kwenye lile Boma au nyumba anayoishi kwa ushawishi wa Mama mpya aliyemleta!
Kiujumla sisi watoto wote ni watu wazima kila mmoja anajitegemea na hakuna tunachoitaji kutoka kwa Baba mzazi ila hatupo tayari kuungana na Mama wa kambo ili tumfurahishe Baba
Maana watoto tunaonekana wabaya kwasababu tu tunaonekana tupe upande wa Mama
Wakuu wangu,nahitaji ushauri wenu kwani naamini wengi humu mmenizidi kwa vingi ..
Jeh! niungane na Baba kwenye maamuzi yake ili anipe Mali au niendelee kuketi upande wa Mama kwasababu bado naona Mama hakutendewa haki
Najua fika mimi ni Mwanaume na sinui nitadondokea wapi ila naheshimu utu kuliko kitu ...!!
Kwa heshima zote ndugu zangu naomba kuwasilisha japo uwandishi wangu sio wakuridhisha ila natumai nimeeleweka ...