Juzi na jana, vyombo vya habari vimeripoti juu ya harambee iliyofanyika huko Yombo Dovya kwa ajili ya ujenzi wa taasisi moja ya kidini (dhehebu la Anglikana). Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa ni Mh. Edward Lowassa, aliyekuwa Waziri Mkuu na sasa Mbunge wa Monduli.
Katika hotuba yake, mbali ya kumuomba Mh. Lowassa kurejesha shule za madhehebu ya dini zilizokuwa zimetaifishwa na serikali atakapokuwa rais, alitumia fursa hiyo kumsafisha Lowassa na kumuelezea kwamba asitishwe na kelele zisizo na msingi kuhusu tuhuma za ufisadi dhidi yake.
Kauli hii ya kushangaza sana, imetolewa na mmoja wa viongozi wa dini wanaoheshimika sana nchini na mtu aliyekuwa mstari wa mbele kukemea vitendo vya ufisadi nchini na hata kuichagiza serikali kuchukua hatua dhidi ya wale wote wanaotuhumiwa kwa vitendo vya ufisadi. Ni huyu huyu baba Askofu aliyepongeza hatua za kujivua gamba kama zilivyoasisiwa na rais Kikwete. Sasa leo, anapokuwa katika shughuli ya kumtakasa kinara mkuu wa mafisadi, tena baada tu ya kufanikisha kuendesha harambee yenye mafanikio (na yeye binafsi kuchangia milioni 20) anatueleza nini? Je, ana maana kwamba ghafla Lowassa amekuwa si yule aliyemshutumu sana na kushinikiza hatua dhidi yake? Au kwake baba Askofu Mokiwa, ufisadi unatafsiriwa tofauti hasa pale fisadi huyo anapokuwa na mchango katika kile anachokipigania yeye baba Askofu?
Kwa maoni yangu, Baba Askofu amepotoka na tafsiri yake ya ufisadi imejaa makengeza na hata kumuondolea imani ya kiroho (moral authority) ya kukemea maovu katika jamii, ufisadi ukiwa moja katika maovu hayo.
Katika hotuba yake, mbali ya kumuomba Mh. Lowassa kurejesha shule za madhehebu ya dini zilizokuwa zimetaifishwa na serikali atakapokuwa rais, alitumia fursa hiyo kumsafisha Lowassa na kumuelezea kwamba asitishwe na kelele zisizo na msingi kuhusu tuhuma za ufisadi dhidi yake.
Kauli hii ya kushangaza sana, imetolewa na mmoja wa viongozi wa dini wanaoheshimika sana nchini na mtu aliyekuwa mstari wa mbele kukemea vitendo vya ufisadi nchini na hata kuichagiza serikali kuchukua hatua dhidi ya wale wote wanaotuhumiwa kwa vitendo vya ufisadi. Ni huyu huyu baba Askofu aliyepongeza hatua za kujivua gamba kama zilivyoasisiwa na rais Kikwete. Sasa leo, anapokuwa katika shughuli ya kumtakasa kinara mkuu wa mafisadi, tena baada tu ya kufanikisha kuendesha harambee yenye mafanikio (na yeye binafsi kuchangia milioni 20) anatueleza nini? Je, ana maana kwamba ghafla Lowassa amekuwa si yule aliyemshutumu sana na kushinikiza hatua dhidi yake? Au kwake baba Askofu Mokiwa, ufisadi unatafsiriwa tofauti hasa pale fisadi huyo anapokuwa na mchango katika kile anachokipigania yeye baba Askofu?
Kwa maoni yangu, Baba Askofu amepotoka na tafsiri yake ya ufisadi imejaa makengeza na hata kumuondolea imani ya kiroho (moral authority) ya kukemea maovu katika jamii, ufisadi ukiwa moja katika maovu hayo.