Nguvu ya pesa! Hiyo ndo nguvu ya mkoloni pekee aliyekataa kuondoka baada ya wakoloni wnegine kurejea kwao. Mkoloni huyu atapata mateka wengi sana kuelekea 2015 na wale tuliowaamini sana wataendelea kutushangaza. Ilianza kwa waandishi, wakaja wahariri na wamiliki wao, sasa ni zamu ya viongozi wa dini mmoja mmoja na baadae itakuwa ni zamu ya wadilifu kurushiwa mawe na kuonekana ndo wachafu na kudhalilishwa. Mwisho itakuwa ni ile hadithi ya kijana aliyekwenda kijiji fulani kule singida na kukuta watoto wa rika lake wote wakikojoa damu kwa sababu ya kichocho na wale wakawa wanamcheka yule kijana na yeye kuonekana ndiye mgonjwa. Hatimaye kijana yule alifanya hila zote ili aambukizwe kichocho na alipofanikiwa alifurahi sana! Ndiyo Tanzania tunayoijenga kwa msaada wa wachungaji wa kondoo wetu!