Baadhi ya Watanzania wanashangaza sana

mtingi1

JF-Expert Member
Mar 21, 2020
945
923
Wasalaam wana JF!

MOLA tuepushe na janga la Corona Amina.

Kuna watu huwa wanasema wakiwataja baadhi ya wanasiasa hususani wapinzani, kwamba watukomboe dhidi ya utawala uliopo wakimaanisha CCM.

Huwa najuliuliza huwa wanamaanisha kitu gani hasa? Kwa kuwa wanaotawala ni Watanzania wenzetu, wenye familia na mfumo wa maisha kawaida kabisa na sisi.

WanaCCM, WanaCHADEMA, wana CUF, ACT na vyama vyote, wote ni Watanzania wenye akili tofauti, imani tofauti, mitazamo tofauti, chama chochote kinachopata nafasi kutuwala kitawatumia watanzania hawahawa katika administration yake.

Hakuna chama kitakuja na brand ya Watanzania tofauti na sisi tuliopo, kitatawala na hawahawa tuliopo.

Wezi watakuwepo, mafisadi watakuwepo, waadilifu watakuwepo pia.

Binafsi sioni chama ambacho mtu atanishawishi kusema eti kitaleta ukumbozi, ni uongo!

USHAURI WANGU:

Ikiwa tutakuwa na KATIBA ambayo itaweka malengo ya Tanzania mbele kwamba chama chochote kitakacho tawala, basi kielekeze katika malengo MAMA.

Tusitegemee ILANI ZA VYAMA pekee, So kama taifa tufikiri katika kuboresha katiba YETU.

Tujiwekee malengo ya muda mrefu kama taifa, KATIBA bora ndio dili kwa mtazamo wangu.

JITAHIDI KUWA MWAMINIFU KWA NAFASI YEYOTE UNAYOPATA KUTUMIKA, SIKU MOJA UTATOA HESABU KWA MUNGU. USILAUMU MTU, WEWE KATIKA NAFASI ULIOPO NI MWAMINIFU KIASI GANI?

KILA MMOJA WETU AKIWA MWAMINIFU TUTALIJENGA TAIFA LETU PAMOJA

Hata hivyo naukubali utendaji wa mh John P. Magufuli.

Ni hayo tu....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama ni hivyo kwanini CCM wananajisi uchaguzi chini ya Magufuli ili waendelee kubaki madarakani? Kwanini wasiheshimu matakwa ya wananchi ili wapishe watanzania wengine nao watawale? Hiyo katiba bora kikwazo ni hao ccm, huku Magufuli unayemkubali akiwa kikwazo namba moja wa katiba bora.
 
Mkuu nisome tena tafadhali
Kama ni hivyo kwanini CCM wananajisi uchaguzi chini ya Magufuli ili waendelee kubaki madarakani? Kwanini wasiheshimu matakwa ya wananchi ili wapishe watanzania wengine nao watawale? Hiyo katiba bora kikwazo ni hao ccm, huku Magufuli unayemkubali akiwa kikwazo namba moja wa katiba bora.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu nisome tena tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu kulikuwa na rasimu ya Warioba, wananchi walitoa maoni yao, lakini ccm kwa wingi wao wakachakachua maoni ya wananchi. Basi haidhuru hiyo rasimu ilichakachuliwa, kulikuwa na katiba pendekezwa iliyokuwa imefikia hatua ya kura za maoni, lakini hata hiyo Magufuli aliikataa. Sasa naona unamkubali mtu asiyetaka katiba bora, bali anataka hii hii ili ubovu uendelee. Kwa maneno marahisi unataka CCM iendelee kukaa madarakani, maana unadhani wengine wote watakaokuja watakuwa kama hawa CCM uliowazoea.
 
Wasalaam wana JF!

MOLA tuepushe na janga la Corona Amina.

Kuna watu huwa wanasema wakiwataja baadhi ya wanasiasa hususani wapinzani, kwamba watukomboe dhidi ya utawala uliopo wakimaanisha CCM.

Huwa najuliuliza huwa wanamaanisha kitu gani hasa? Kwa kuwa wanaotawala ni Watanzania wenzetu, wenye familia na mfumo wa maisha kawaida kabisa na sisi.

WanaCCM, WanaCHADEMA, wana CUF, ACT na vyama vyote, wote ni Watanzania wenye akili tofauti, imani tofauti, mitazamo tofauti, chama chochote kinachopata nafasi kutuwala kitawatumia watanzania hawahawa katika administration yake.

Hakuna chama kitakuja na brand ya Watanzania tofauti na sisi tuliopo, kitatawala na hawahawa tuliopo.

Wezi watakuwepo, mafisadi watakuwepo, waadilifu watakuwepo pia.

Binafsi sioni chama ambacho mtu atanishawishi kusema eti kitaleta ukumbozi, ni uongo!

USHAURI WANGU:

Ikiwa tutakuwa na KATIBA ambayo itaweka malengo ya Tanzania mbele kwamba chama chochote kitakacho tawala, basi kielekeze katika malengo MAMA.

Tusitegemee ILANI ZA VYAMA pekee, So kama taifa tufikiri katika kuboresha katiba YETU.

Tujiwekee malengo ya muda mrefu kama taifa, KATIBA bora ndio dili kwa mtazamo wangu.

JITAHIDI KUWA MWAMINIFU KWA NAFASI YEYOTE UNAYOPATA KUTUMIKA, SIKU MOJA UTATOA HESABU KWA MUNGU. USILAUMU MTU, WEWE KATIKA NAFASI ULIOPO NI MWAMINIFU KIASI GANI?

KILA MMOJA WETU AKIWA MWAMINIFU TUTALIJENGA TAIFA LETU PAMOJA

Hata hivyo naukubali utendaji wa mh John P. Magufuli.

Ni hayo tu....

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni Hadi tutakapo pata utaratibu wa kuwafunga viongozi wakitoka madarakani kama walivo wenzetu ndio tutakuwa na maendeleo,Kinga ya kutoshtakiwa tutasubiri Sana huku tukiendelea kuvuna mabua miaka 60 ya Uhuru bado tunavuna mabua tu.
 
Mkuu kulikuwa na rasimu ya Warioba, wananchi walitoa maoni yao, lakini ccm kwa wingi wao wakachakachua maoni ya wananchi. Basi haidhuru hiyo rasimu ilichakachuliwa, kulikuwa na katiba pendekezwa iliyokuwa imefikia hatua ya kura za maoni, lakini hata hiyo Magufuli aliikataa. Sasa naona unamkubali mtu asiyetaka katiba bora, bali anataka hii hii ili ubovu uendelee. Kwa maneno marahisi unataka CCM iendelee kukaa madarakani, maana unadhani wengine wote watakaokuja watakuwa kama hawa CCM uliowazoea.
Kwa katiba hii chakavu still wakiingia wengine wasio wa upande wao watalimia meno.Mfumo wetu mfumo ukishakutupa huna chako unaweza fanywa chochote na waliopo Sasa kama ulitupa mawe kwenye vioo vya wenzako jiandae nawe kutupiwa
 
Usitudanganye wewe Ccm huwa inawakilisha aina flan ya watu walio kata tamaa kama ilivyo wewe na mawazo ya kizee zee
Ila vyama safi kamaa Act vina fikra ya ukombozi
 
Ni Hadi tutakapo pata utaratibu wa kuwafunga viongozi wakitoka madarakani kama walivo wenzetu ndio tutakuwa na maendeleo,Kinga ya kutoshtakiwa tutasubiri Sana huku tukiendelea kuvuna mabua miaka 60 ya Uhuru bado tunavuna mabua tu.

Wow, nimewahi kusema hiki kitendo cha rais kuwa juu ya katiba na kutoshitakiwa akiwa au ametoka madarakani, ndio chanzo halisi cha maovu yote ya kimfumo ndani ya nchi hii. Siku tutatakapotoa hicho kifungu, zile amri za nyuma ya pazia ziitwazo amri toka juu itakuwa ndiyo mwisho. Kwa sasa hivi amri toka juu ina nguvu kuliko katiba na sheria. Na kimsingi amri hii toka juu ndio inayoagiza mambo yote machafu hapa nchini, na mwanya huo hupatikana kupitia madaraka ya urais.
 
Wow, nimewahi kusema hiki kitendo cha rais kuwa juu ya katiba na kutoshitakiwa akiwa au ametoka madarakani, ndio chanzo halisi cha maovu yote ya kimfumo ndani ya nchi hii. Siku tutatakapotoa hicho kifungu, zile amri za nyuma ya pazia ziitwazo amri toka juu itakuwa ndiyo mwisho. Kwa sasa hivi amri toka juu ina nguvu kuliko katiba na sheria. Na kimsingi amri hii toka juu ndio inayoagiza mambo yote machafu hapa nchini, na mwanya huo hupatikana kupitia madaraka ya urais.
Mwafrika yeyeto usipomuwekea mfumo wa kumdhibiti hawezi kuwa na tija ni lzm ataumiza wenzake.Check South Africa, Zimbabwe,Congo nk mobutu,zuma,bokasa, mugabe walijijengea makasri mahekalu kwa wizi wa Kodi za umma utadhani awatokufa.Lkn huwezi sikia watawala wa kikoloni mfano kina Ian Smith,Pita Botha,de Clark waliiba Kodi za umma wakajimilikisha na kujenga mahekalu popote duniani,isipokuwa hawa wakoloni weusi ni Sababu hawana mfumo wa kuwabana katiba zinawaruhusu kufanya chochote wajisikiacho kuuwa,kuiba,kuuwa uchumi, kuleta umasikini,nk huku wakipewa Kinga,hii iko Africa pekee thus hatuwezi endelea tofauti na wenzetu viongozi wao hawana room ya kuchezea katiba zao huwezi unakwenda jela wanaweka mwingine thus wanasonga.
 
Naamini mzee Magufuli nimuelewa, approach iwe nzuri tu. Ata take action I believe
Mkuu kulikuwa na rasimu ya Warioba, wananchi walitoa maoni yao, lakini ccm kwa wingi wao wakachakachua maoni ya wananchi. Basi haidhuru hiyo rasimu ilichakachuliwa, kulikuwa na katiba pendekezwa iliyokuwa imefikia hatua ya kura za maoni, lakini hata hiyo Magufuli aliikataa. Sasa naona unamkubali mtu asiyetaka katiba bora, bali anataka hii hii ili ubovu uendelee. Kwa maneno marahisi unataka CCM iendelee kukaa madarakani, maana unadhani wengine wote watakaokuja watakuwa kama hawa CCM uliowazoea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuwe na approach vizuri tu, mzee Magufuli anaweza kufanya maamuzi sahihi yatakayopelekea kuwa na KATIBA bora. Busara inahitajika katika hili, tuachane na mihemko ya kisiasa, tuwe na mtazamo wa kuijenga nchi yetu
Ni Hadi tutakapo pata utaratibu wa kuwafunga viongozi wakitoka madarakani kama walivo wenzetu ndio tutakuwa na maendeleo,Kinga ya kutoshtakiwa tutasubiri Sana huku tukiendelea kuvuna mabua miaka 60 ya Uhuru bado tunavuna mabua tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio maana nikasema tungekuwa na KATIBA bora, ndio suluhisho pekee, hata leo akija Mbowe akawa Rais, nothing will change, wakati huu mzee Magufuli ameonyesha uthubutu tumtumie vizuri, tumwamini anaweza kuleta mabadiliko
Mwafrika yeyeto usipomuwekea mfumo wa kumdhibiti hawezi kuwa na tija ni lzm ataumiza wenzake.Check South Africa, Zimbabwe,Congo nk mobutu,zuma,bokasa, mugabe walijijengea makasri mahekalu kwa wizi wa Kodi za umma utadhani awatokufa.Lkn huwezi sikia watawala wa kikoloni mfano kina Ian Smith,Pita Botha,de Clark waliiba Kodi za umma wakajimilikisha na kujenga mahekalu popote duniani,isipokuwa hawa wakoloni weusi ni Sababu hawana mfumo wa kuwabana katiba zinawaruhusu kufanya chochote wajisikiacho kuuwa,kuiba,kuuwa uchumi, kuleta umasikini,nk huku wakipewa Kinga,hii iko Africa pekee thus hatuwezi endelea tofauti na wenzetu viongozi wao hawana room ya kuchezea katiba zao huwezi unakwenda jela wanaweka mwingine thus wanasonga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naamini mzee Magufuli nimuelewa, approach iwe nzuri tu. Ata take action I believe

Sent using Jamii Forums mobile app

Inaonekana ww ni muabudu sanamu, unataka kumgeuza kuwa yeye ndio mwenye ruhusa ya kupatikana kwa katiba. Kwahiyo mpaka hapo alipo hajaafiki kwakuwa hajafanyiwa approach nzuri? Hatuhitaji hisani yake ili kupata katiba mpya, hata tusipoipata chini ya utawala wake, tutaipata tu. Kama ww unahitaji hisani yake kamuombe kwa hiyo approach yako nzuri. Sisi tunataka katiba mpya kwa amani, ikishindikana kwa njia ya amani, tutaipata kwa njia nyingine.
 
Mkuu, watathimini hao wanaACT, halafu uniambie ni nani unamuwekea tumaini lako

Sent using Jamii Forums mobile app

Yeye ana imani na chama cha ACT, ila ww una imani na mtu! Miaka hii dunia inaoongozwa na mifumo, ww bado uko kwenye dunia ya kusujudia mtu! Mkuu endelea kuvuta shuka kwenye huo usingizi wa kuamini katika nguvu ya mtu. Alaaniwe amtegemeaye mwanadamu.
 
Back
Top Bottom