Baadhi ya wanaume wa Dar tatizo ni nini?

Baadhi ya wanaume wa Dar tatizo ni nini?

From Sir With Love

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2010
Posts
2,076
Reaction score
3,827
Nina miezi kadhaa sipo Dar kwa sababu ya majukumu ya kikazi.

Niliporudi, juzi kati tulienda sehemu na mama watoto, nikawa natoa hela kwenye mtandao. Kuna wazee walikuwa wamekaa pembeni kama kawaida nikawasabahi na nikaendelea na yangu.

Baada ya kutoka pale mama watoto akaniuliza. Hivi watu siku hizi wakoje? Nikamuuliza kwani vipi? Akaniambia wale wazee walikuwa wanatuzungumzia sisi. Nikamuuliza kivipi? Akasema walikuwa wanaulizana kama sisi ni mke na mume kwa sababu wanaona tunafanana. Nikamuuliza uliwasikia kweli? Akajibu ndiyo.

Dah nikamwambia wife siku hizi watu hawakuteti nyuma ya nyumba kama zamani siku hizi watu wanakuteta huku unasikia ili ujibu mapigo wapate sababu.

Wiki hii nipo Dar. Leo nikawa nimeenda sehemu katika kuongea na simu nikawa nafuatilia issue moja ya kikazi. Kumbuka kwa sasa nipo mkoani kwa hivyo nilivyokuwa naongea na jamaa nikamweleza mimi ni fulani kutoka mkoa fulani ili anielewe. Basi tukaongea tukamaliza.

Wakati naondoka yule dereva pembeni yangu ambaye alikuwa amebeba wanawake kwenye gari akawa anawauliza kama kweli nafanya kazi mkoa niliotaja kwenye simu, kwa sababu nilimsikia nikamtizama kama dakika tatu hivi lakini akawa amekauka kama sio yeye aliyewauliza wale akina dada.

Dah nilimumaind sana yule jamaa. Sana sana tu. Ila nikasema moyoni shetani hawezi kunishauri cha kufanya.

Nikaondoka kwa sababu sihitaji kumdhibitishia mtu kwamba nasema ukweli. Na wakati mwingine maneno huwa hayatoshi kufikisha ujumbe. Na ziada ya maneno ni vitendo na gharama yake ni kubwa ukizingatia muda utakaopoteza.

Ni swali tu kwa baadhi ya wanaume wa Dar. Nini kimewakuta. Mbona mnakuwa kama wanawake. Kuna wanaume wengine humu JF wanaadika " wewe muongo" lakini wao hawana ukweli. Hawana data.

Amua tu kuwa dume au jike mbona operation zipo. Kama unahamu ya kuhamia upande mwingine amua tu na kama huwezi tuliza hizo pu*** zako zisizo z**.

Dume zima unaafuatilia mambo ya watu. Nikiongeza matatizo yangu kwako utaweza wewe?

Tutafute maendeleo. Achana na mambo ya watu.
 
We unesemwa hadharani na wewe umekuja kuwasema mafichoni hamna tofauti wote wewe na hao ni wanafki na wambea
 
Utakuwa unamsema GENTAMYCINE kijanja maana mada zake mmmmhh ni aina ya wanaume wa Dar unaowazungumzia
 
Kama umepanic iv bro kwanini hayo maneno usingemchana uyo jamaa hapo hapo sidhan kama humu ni sehem sahihi ya kufikisha hisia zako!!!
Brobiz lengo na nia ni kuuliza mbona wanaume wa zamani hatukuwa hivyo na hatupo hivyo.

Ningemkabili jamaa nisingeishia na maneno. Vitendo vingeongea. Na mwisho wake usingekuwa mzuri.

Kuondoka ndiyo suluhisho.
 
Utakuwa unamsema GENTAMYCINE kijanja maana mada zake mmmmhh ni aina ya wanaume wa Dar unaowazungumzia

Humu JF ili ujulikane upesi au utambulike kuwa na Wewe leo ume log in ni lazima ama umfuate fuate GENTAMYCINE au umtaje tu na zaidi ya hapo hutoweza kujulikana. Najiona mshindi sana kwani nawachezesheni mziki ninaoupenda kila siku na mnaufuata vilivyo. Akhsante Mwenyezi Mungu kwa aina hii ya upako na tunu ya mvuto uliyonipa.
 
Wanaume siku hizi ni wambea balaa. Sio mwambao wa pwani wala mikoani. Wote ni wambea balaa. Yote ni sababu ya ukosefu wa kazi za kufanya na ugum wa maisha. Sidhan kama mwanaume mwenye shughuli zake anaweza kumdiscuss mtu. Na sehemu zinazoongoza kwa umbea wa wanaume ni vijiwe vya kahawa na vijiwe vya bodaboda. Sio siri wanakera sana.
 
Wanaume wa mkoani bwana...full kulalamika masikini! Njooni Dar mpepese macho kidogo Jijini
 
Back
Top Bottom