fikirikwanza
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 7,452
- 3,073
Ukimwona samaki anaogelea kwenye beseni au kalai, ujue kawekwa humo, haiwezekani kuwa alizaliwa humo.
Kwa hiyo ile single ya kapuya imeishaje?????????????????????????Naunga mkono hoja!
Kikwete amkabidhi Mh Lema hayo majina ASAP! watanzania wana haki ya kufahamu ukweli. Wauza unga wanawaharibu sana vijana wetu.
Jana mbunge wa Arusha mjini mhe. Godless Lema alimtaka mbunge wa Kigoma Kazikazini mhe. Zitto Zuberi Kabwe kuwa ampatie majina ya watu walioficha mabilion nchi uswiss wakati Lema akisubilia majina kutoka kwa Zitto, gafla AG Werema aliibuka kusiko julikana na kuweka wazi kuwa zitto kwa kiapo hana majina wala account za walioficha mabilion huko uswiss.
Sasa basi ni wakati mwafaka kwa Mbunge Godbless Lema kuomba majina ya wauza unga ambao Kikwete alishawahi kusema anayo lakini leo mwaka wa saba hatujawahi kutajiwa licha ya Lukuvi nae kuthibitisha kuwa siku majina yakitajwa hakuna mbunge atakae baki salama.
Kwa kauli hiyo bungeni tumejaza wauza sembe na watimiaji wa sembe yaani madawa ya kulevya na Kikwete anawajua.
Ni wakati mwafaka sasa tutajiwe majina hayo au Werema atoe kauli kama ya jana kuwa kwa kiapo Kikwete hana majina ya wauza unga.
Asanteni naomba michango yenu.
hivi unaweza kumfananisha rais kikwete na mtu kama lema? mkuu Crashwise ata kama unafilisika kifikra si kwa kiwango hiki,kutuletea thread za kitoto. Zitto alikuwa anahojiwa na kamati iliyochaguliwa na bunge kwa kiapo, sasa mnataka from no where rais nae afanye hivyo kwa misingi gani? tuweke itikadi pembeni tujadili mada
Hivi majina yakijulikana nini huwa kinafuata?. Mwakyembe alitaja wahusika wa Richmond, Slaa alitaja wahusika kwenye List of Shame..... hata hao wenye Fedha chafu Uswis wakitajwa inakuaje?
au adhabu ya Fisadi Bongo ni kutajwa hadharani?
Who is LEMA TO JK