Oportunist2012 nadhani umetoroka wodi ya vichaa Milembe,thread yako inavutia lakini ujumbe wake pumba tupu.Unaposema Bukoba,na ukasema tusipoipa cdm madaraka tumekwisha,je mikoa ya Dodoma,Singida mbona magamba full na huko vp,acha mawazo ya kichaa km una ishu na Wahaya sema ila siyo longolongo
wewe mlopokaji tu,kwanza huko Bukoba kunaishi watu makini wewe hapakufai kabisa.. Bukoba hakuko hivyo..wanyamaanga ni neno la kawaida tu
kyasaka!
ahsante kwa ufafanuzi wako,lkn ndugu zako wanatumia neno wanyamahanga vibaya.wanahusisha na kutokuwa mhaya yaan wakuja ambaye hana thaman bukoba.
mimi mbona mhaya nikienda bukoba nikongea kihaya na kujifanya mjuaji naitwa mnyamahanga na bibi yangu?Na kuhusu mwanza,dar kuendelea mbona wahaya tumewekeza sana hiyo mikoa tajwa hahaha.wahaya sio wabaguzi labda wengine wako arrogant.sema tumesoma sana unamuona mama tibaijuka kichwa chake hadi kwa wakorea hawamuwezi!
Naunga mkono hoja kwa 100%We jipange upya! Walimu wangapi wantenda hayo uloyasema Tanzania hii? N-way, najua huna data za kutosha, tuulizeni sisi nasi tulio nje ya nyumbani. Tabia ya mtu mmoja usiihamishie mkoa mzima na tena ukome kabisa! Unajua huko CDM (japo ni chama langu) kuna mtu, tena mbunge anahutubia watu akisema anataka Kaskazini iwe nchi, JE TUSEME CDM WOTE WALIKUWA HIVYO? Wizarani (karibia zote) unaposikia kila kukicha kwamba wako mabila flani flani, Polisi inaposemekana vyeo vyote ni vya kabila na dini flani, NSSF tulipoambiwa kuna ....... flani.
Hilo jina ulilolinyumbua, si la leo Bukoba, tangu zamani za mababu wasiojua kiswahili cha kujua kwa EBIGUNJU ndo wanaitwa wanyama, walilitumia kuongelea yeyote ambaye alionekana kutoka nje ya mkoa huo na hajui kuongea lugha yao.
Je, umefuatilia kuona makabila na mikoa mingine wanasemaje kuhusu wageni, au etc. (end of thinking capacity) yako imeishia BK?
CHADEMA ni chama chetu lakini tusiingie kwa hasira za kutaka kulipiza visasi katika mabaya yalotendwa na wengine, hapo tutashindwa. Bali tufikirie zaidi ni jinsi gani tutaweza kuivusha nchi kwenda kwenye TANZANIA TUITAKAYO:israel:
Nyinyi watu mbona hamtaki kubadilika?..najua kasumba ya ubaguzi ipo kwenye damu zenu lakini jirekebisheni..kwa nini hutaki kukubali ukweli kwamba nyinyi ni wabaguzi? wenyewe kwa wenyewe mnabaguana kimaeneo..mhaya wa Kiziba anambagua wa Karagwe,wa Karagwe anambagua wa Maruku,wa Maruku naye anambagua wa Muleba...hivi nyinyi ini mtaacha kasumba hii ya ukabila?...vichwa vingi haviko Bukoba...viko maeneo yenye tija...Bukoba kuna vilaza tu.Hata wasomi wenye asili ya mkoa wa Kagera wameukimbia wanasema kuna kila aina ya unafiki hata wewe unaeleta kiherehere haupo huko Bukoba....I tell you facts and not opinions...acha hizo...GAMBA MKUBWA WEWE!!
Kuna kila sababu sisi ijana na Watanzania wote tukipe ridhaa CHADEMA kiunde serikali mwaka 2015. CCM ni chama muflisi kilichoshinda kuzuia ubaguzi wa aina zote.
Hata vurugu za ZNZ ni matokeo ya kuwa na serikali legelege yenye usalama wa Taifa wanaolinda viongozi na kuwaacha raia wakiharishiwa maisha yao na wahuni wachache.
Yaliyotokea ZNZ hata Bukoba yaweza tokea. Watanzania wasio wazawa wanabaguliwa kana kwamba wanyama.Wamepachikwa majina mbalimbali yanayodharirisha utu wao, mfano wanaitwa WANYAMA ANGA yaan wanafananishwa na ndege.Hali ipo hata ktk ajira.
Mfano halisi ni idara ya elimu sekondari ambapo afisa ana sera ya kuwapendelea walimu wazawa wa Bukoba na kuwabagua walimu wa mikoa mingine.
Imeshawahi kutokea mkuu wa shule wa Rutunga alimshitaki mwalimu mkorofi kwa afisa elimu,afisa elimu baada ya kujua yule mwalimu ni mhaya alimlaumu yule mkuu wa shule kwa nin amemshitaki huyu mwalimu.asema lazma tuwalinde vijana wetu angekuwa si mhaya tungemuadhibu, hii ndio serikali ya CCM yenye watendaji wabaguzi huku ikibariki ubaguzi huo.
TUSIPOIWEKA CDM MADARAKANI 2015 TUTAZIDI KUJUTA!!
Mwaka 2006 kama siyo 2007 Kikwete akiwa ameambatana na waziri wa viwanda na bishara wakati huo Nazir Karamagi, katika mkutano wake na watanzania waishio Oslo, Norway mama mmoja kutoka Bukoba alimuuliza Kikwete swali kuhusu uhaba wa madaktari huko Bukoba. Kikwete hakujibu swali lile akamsukumia mbunge wao Karamagi ajibu swali lile. Karamagi alijibu kwa kifupi tu kuwa "Tatizo letu wahaya tunawakataa madaktari wanaopangiwa kazi huko kwetu ambao siyo wahaya hivyo inawalazimu kuondoka". Kwa maana nyingine analiyoyasema mtoa hoja hapa yana ukweli ndani yake.
Kwani Karamagi alikuwa ni mwakilishi wa Wahaya katika ziara hiyo?
Opportunist, umetoa tafsiri isiyo sahihi. Wahaya wanawaita wageni kutoka ng'ambo ya ziwa Victoria "abanya mahanga". Neno "mahanga" lina maana ya nchi ya mbali, ng'ambo hasa kuvuka ziwa Victoria. Mhaya akisafiri ng'ambo ya ziwa Victoria wanasema "agile omu mahanga"; ikiwa na maana "ameenda nje", "ameenda ng'ambo". Kwa hiyo, neno "banyamahanga" halina maana ya "ndege" kama unavyotaka wanaJF waamini. Aidha, inabidi ujue kuwa kila kabila lina namna ya kuwaita wageni wa kabila hilo; kwa mfano Wasukuma wanawaita "jogoli", Wapare wanawaita "wanyika", n.k.na hilo halina maana ya ubaguzi wa rangi. Ina maana ukimwita mzungu "foreigner" unakuwa unambagua?
Vile vile haipendezi tabia ya Mhaya mmoja lichukuliwe ni tabia ya Wahaya wote (stereotyping).