Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,161
- 10,877
Kwa majigambo makubwa juzi raisi Donald Trump wa Marekani alitangaza kutoka ikulu ya Marekani juu ya kurudishwa kwa uhusiano baina ya Israel na taifa la Sudan.
Hata hivyo tangazo hilo limepingwa vikali na wananchi kupitia vyama vikuu vya kisiasa.Anayeongoza kupinga uhusiano huo ni Sadik El Mahdi aliyewahi kuwa waziri mkuu wa nchi hiyo ambaye kwa sasa anaongoza chama kikuu cha upinzani nchini humo cha Popular Congress Party.Kuonesha kukasirishwa kwake na tangazo hilo la serikali ya mpita Sadik El Mahdi ameacha kuhudhuria mkutano mkubwa wa viongozi wa dini uliokuwa ufanyike leo.
Katika tamko lake Sadik El Mahdi amesema urudishwaji wa uhusiano huo unapingana na sheria za nchi ya Sudan na ni kama cheche za kuanzisha vita vyengine vya wenyewe kwa wenyewe.Kiongozi mwengine wa chama hicho Kamal Omar amesema serikali ya mpito na ambayo haijachaguliwa na wananchi haina mamlaka ya kurejesha uhusiano na Israel.
Tamko kutoka chama cha FFC nalo limesema msimamo wa watu wa Sudan bado ni kuunga mkono ndugu zao wa Palestina ili warejeshewe haki zao.
Hapo Ijumaa mamia ya wananchi waliandamana kupinga tangazo la Serikali kuhusiana na tangazo la kurejeshwa uhusiano na Israel.
‘Ignition of new war:’ Sudan political parties reject Israel deal
Hata hivyo tangazo hilo limepingwa vikali na wananchi kupitia vyama vikuu vya kisiasa.Anayeongoza kupinga uhusiano huo ni Sadik El Mahdi aliyewahi kuwa waziri mkuu wa nchi hiyo ambaye kwa sasa anaongoza chama kikuu cha upinzani nchini humo cha Popular Congress Party.Kuonesha kukasirishwa kwake na tangazo hilo la serikali ya mpita Sadik El Mahdi ameacha kuhudhuria mkutano mkubwa wa viongozi wa dini uliokuwa ufanyike leo.
Katika tamko lake Sadik El Mahdi amesema urudishwaji wa uhusiano huo unapingana na sheria za nchi ya Sudan na ni kama cheche za kuanzisha vita vyengine vya wenyewe kwa wenyewe.Kiongozi mwengine wa chama hicho Kamal Omar amesema serikali ya mpito na ambayo haijachaguliwa na wananchi haina mamlaka ya kurejesha uhusiano na Israel.
Tamko kutoka chama cha FFC nalo limesema msimamo wa watu wa Sudan bado ni kuunga mkono ndugu zao wa Palestina ili warejeshewe haki zao.
Hapo Ijumaa mamia ya wananchi waliandamana kupinga tangazo la Serikali kuhusiana na tangazo la kurejeshwa uhusiano na Israel.
‘Ignition of new war:’ Sudan political parties reject Israel deal