Baada ya mapenzi

Baada ya mapenzi

Hapo watu wanajaribu kuongea mambo ambayo yanaufariji moyo tu, ili asiumie sana kumuacha mwenzi wake...
 
Binafsi nafikiri ni kwamba kwa wanawake wengi huwa hawaoni kasoro za mwanaume au anaona ila anapotezea kwa makusudi ikiwa huyo mwanaume ana pesa na anamwezesha kwa mengi.

Kwa sisi wanaume mara nyingine unaweza kumpenda binti kwa muonekano au kigezo flan mfano mwenye "CHURA" la ukweli au mwenye sura nzuri kisha unamtumia kwa muda flan halafu unakuta anayemzidi viwango.

Sasa hapo kuna Wanaume wenye tabia ya kuwaponda hao maduu au wengine kukaa kimya tu.

Hatahivyo, hii tabia ipo zaidi kwa wanawake na sio tabia nzuri kiukweli.
Huku daslam huwa hatusemi tena chura, imesha expire
 
Hapo ulipouliza kuwa maneno yapi ya ukweli, kati ya wakati penzi limekolea au wakati penzi limechuja. Mimi naona hivi...

Maneno yote ni ya ukweli kwa nyakati zote hizo mbili (hapa nachukulia mtu mwenye utu, mkweli na asiyekuwa na hila moyoni mwake. Vinginevyo kusema mtu ana kibamia au bwawa wakati unajua kabisa hana ni kuidanganya nafsi).

Wakati penzi limekolea nia ya mtu inakuwa ni moja tu ya kumpenda mwenzi wake, hivyo hata yale mabaya atayachukulia positively ili tu penzi linoge, lisonge.

Sasa mkishaachana, hususan kama mmoja kaachwa, basi kuyaibua yale mapungufu yake inasaidia sana kumsahau na kuponya roho, kama ukiwa unayawaza repeatedly (wataalam wamethibitisha hilo).

Hivyo mimi naona ni kama survival strategy.

Afterall, ukweli ni kwamba, hakuna mtu asiyekuwa na mapungufu/mabaya yake.
 
Hiyo imewahi kunitokea na nilichogundua ni kuwa alikuwa anasem hayo maneno kwakuwa bado ananihitaji ila mimi sikutaka kurudi nyuma.
Alipoona anabwatuka tu lakini mimi nampuuza alijirudi mwenyew akaacha mana nilikuja kumwambia ukweli kuwa siwezi kuwa nae tena.
Mwaka wa tatu unaenda still tunawasiliana na tumebaki marafiki wa kawaida.
Mapenzi upofu mtu hata awe na kasoro unazivumilia tu.
Kibaya ni kuwa kuna watu mkiachana wanatokwa povu na kashfa kibao ila sio vizuri.
Mimi napenda nikiachana na mtu tuachane kwa amani hata tukikutana tunacheka sio mkikutana kama maadui hata hamsalimiani .
Wenye tabia hizi acheni hata kama alikutenda vibaya
 
Huo upofu hupona baada ya kuachana au?

Maana watu wakishaachana ndo utasikia kila lililo baya la mtu.
Huo upofu hupona baada ya kuachana au?

Maana watu wakishaachana ndo utasikia kila lililo baya la mtu.
Huo upofu hupona baada ya kuachana au?

Maana watu wakishaachana ndo utasikia kila lililo baya la mtu.
Huo upofu hupona baada ya kuachana au?

Maana watu wakishaachana ndo utasikia kila lililo baya la mtu.
naam hapo ndokila kitu huwa kinaonekana kwa uhalisia wake
 
mkibwagana ndo kila mmoja anaanza kutafuta na kugundua madhaif ya mwenzio, utaskia pampuchu yako mbaya mara unakibamia, uyu anasema we n kama gogo 2. Chakushangaza wanamiaka 3 kwenye mapenz yao. Tuachanage kiustaarabu maisha bado yanaendelea
 
Ndiyo maana Mimi huwa sins choice wala class, mwanamke ni mwanamke tu, mradi K iwepo!
Tukizinguana wala sitaona ubaya au uzuri wake, najiweka pemneni nabeba zigo langu la Maisha nasonga mbele.
 
Utakuta anakwambia mume/partner wangu ndiye anagharamia holiday zetu, ananinunulia gari, anafanya repair zote ndani ya nyumba. Unaomba na wewe uolewe kesho umpate wa kununulia gari. Wakiachana sasa utasikia gari si nilinunua mwenyewe hii
 
Nikuruhusu emotions zikuendeshee tu.

Haha..kuna binti mmoja tulimwagana. Alikuwa kaweka kichwani phone number yangu basi hasira zikimpanda ananirukia hewani ananitukaaaana akimaliza anakata simu analala

I never reacted or kumjibu matusi yake. Leo hii kawa rafiki yangu na misamahaa kibao.
Ha haaa hii style ya x wako ngoja nitaitumia for the future.... Umeuburudisha mchana wangu
 
Kwenye mapenzi, ukweli ukizidi sana yanapoteza mvuto haraka... na uongo ukizidi sana yanaharibika mapema...
 
Binadamu bana!

Watu wakiwa kwenye lindi la mapenzi huwa wanaonana wazuri sana.

Unakuta labda mdada anamsifia sana jamaa alivyo mzuri.

Anakuwa na majigambo ya hapa na pale. Kwamba hataki wadada wenzie waone hata picha zake kisa anahofia kuibiwa kwa sababu jamaa ni 'mzuri', kwa mujibu wake.

Sasa penzi likishachuja na wahusika kumwagana, ghafla yule alokuwa mzuri eti anageuka kuwa mbaya.

Utasikia 'oh mtu mwenyewe kwanza mbaya', 'mtu mwenyewe wala sio mzuri', mtu mwenyewe ana kibamia, mtu mwenyewe ana matege, mtu mwenyewe hivi, mtu mwenyewe vile.

Hilo limenipelekea niwaze hivi ni maneno yepi ambayo ndo huwa ya kweli?

Ya wakati penzi limekolea au ya wakati penzi linapochuja?

Pia kauli kama hizo ni moja ya uthibitisho kuwa mapenzi bila uongo uongo nayo hayataenda vizuri.

Wakati mwingine labda huwa inambidi mtu amdanganye mwenzake walau kidogo tu ili mapenzi yao yaweze kwenda bila mushkili.

Wadau nyie mnalizungumziaje hilo suala?

Mshawahi kuwa 'wazuri' pindi penzi limekolea lakini mkaja kuwa 'wabaya' baada penzi kuchuja au kuisha?
Una umri gani mkuu?
 
Ukitaka kuwafaidi warembo, kuwa muongo muongo, utawafaidi sana
 
Ha haaa hii style ya x wako ngoja nitaitumia for the future.... Umeuburudisha mchana wangu
Mmh...wewe utachezea ngumi aseeh...yale matusi yanahitaji uvumilivu wa kujiapizaa
 
Maneno ya mkosaji hayo! Wanaongea hivyo kujifariji
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom