Baada ya Makete jana nimetua Bumbuli kwa Makamba

Baada ya Makete jana nimetua Bumbuli kwa Makamba

The oris

Member
Joined
Jan 4, 2017
Posts
91
Reaction score
167
Baada ya kumaliza Makete katika shughuli za kikazi leo nipo bumbuli kwa mbunge January makamba. Bumbuli ni kuzuri sana hali ya hewa ipo safi kabisa hakuna jua kabisa green city, wakazi wa Bumbuli ni wakarimu mno sio wachoyo.

Chakula bei chee kuna vyakula vingi sana, ukiwa na elfu 1000 unakula mpaka unasaza. Huduma za jamii zipo za kutosha kuna hospital kubwa kabisa Bumbuli Lutheran hospital utaiona kwenye picha.

Kuna vituo vya afya 8 zahanati ya Galambo, Mgwashi, Bumbuli, Kwehangala nk.
Kila nyumba ina bomba la maji pamojana umeme, huduma ya maji ni bure, shule za msingi na sekondari zipo za kutosha.

Tatizo kubwa la wasambaa bado hawajaelimika bado washamba wana asili ya uoga, bado wana ule u CCM.

Picha zinafuata
 
tmp-cam-1619100526.jpg

hapo ndio bumbuli town
 
Nilikaa hapo Bumburi mjini kwa siku Tano (2016) kuna baridi sio mchezo, ila upande wa vyakula bei nafuu sana pia matunda kama ndizi na parachichi na maembe bei chee sana
 
Mkuu, kufika leo tu umeshayajua yote hayo kuhusu Bumbuli? Taratibu Mkuu. Kama ni promo, fanya bila kututapeli na kutulaghai
Mkuu nimefika jana tu hayo yote nimeambiwa na wenyeji wazawa wa huko
kingine nimfanyie mtu utapeli au promo ili iweje? au nimefanya makosa kuanzisha thread?
 
Mkuu nimefika jana tu hayo yote nimeambiwa na wenyeji wazawa wa huko
kingine nimfanyie mtu utapeli au promo ili iweje? au nimefanya makosa kuanzisha thread?
Ungesema mwanzoni kabisa kuwa mambo hayo umeambiwa. Usijali Mkuu, enjoy your stay there!
 
Back
Top Bottom