Baada ya Machali nani anafuata?

Baada ya Machali nani anafuata?

zzk ndio atafuata, eti mpango wa kutikisa kabisa upinzani na kuuzika.
 
Tundu Lissu, Mbowe, Maalim Seif, n.k. mmoja wao akirudi ccm basi Itakuwa ndiyo mwisho wangu mimi kupenda demokrasia, nitaachana kabisa na ushabiki wa kisiasa
Wewe ipo siku uliamini Dr. Mihogo angerudi ccm?
 
For sure huyu jamaa Ana laana ya wanakigoma kwani Kuna baadhi ya wazee walimlaumu sana pale walipompigania kama kijana wao ili akawawakilishe lkn nipale tu alipoupata ubunge akahama mtaani akaenda kula maisha mjini na kuwatosa kabisa timu yake pamoja na dharau hapo sasa nao wakafanya kazi yao kuhakikisha hashindi hata kama kaamia Kwenye Chama cha role model wao... Kiujumla ni mlafi wa madaraka na kwa Mujibu wa lecturers wake, alikuwa mtu wa kubebwa lkn huwa anasahau alipotoka.
 
Moses Machali Ni Kweli Kaenda Kuungana Na Ng'ombe Wengine Waliokatika Mikia,
 
Kwa kuwa Magufuli hana fedha za kufadhiri matawi ya CCM baada ya Machali anayefuata ni Zitto mwenyewe kwa kuwa njaa ndiyo inayowakimbiza,
 
Mungu mwema. Naona dalili za Msindi (afande) kurudi!
 
Kwa kuwa Magufuli hana fedha za kufadhiri matawi ya CCM baada ya Machali anayefuata ni Zitto mwenyewe kwa kuwa njaa ndiyo inayowakimbiza,
Laana ya usaliti inawatesa, tulisema na kuwatahadarisha hawa wanasiasa Vijana waliopata umaarufu mkubwa kuwa ktk mafanikio waliyokuwa wamepata walipaswa kutulia na kuwafanyia Wananchi waliyowakubali kazi, wao wakaanza kung'ang'ania madaraka... Langu jicho tutasikia mengi
 
Ila wanasiasa wa kutoka Kigoma wana matatizo. hawaaminiki kabisa
 
Tundu Lissu, Mbowe, Maalim Seif, n.k. mmoja wao akirudi ccm basi Itakuwa ndiyo mwisho wangu mimi kupenda demokrasia, nitaachana kabisa na ushabiki wa kisiasa
usikate tamaa hata kama wakirudi, demokrasi ni sawa na ushabiki kama wa simba, yanga, liverpool, arsenal, n.k. hata kama club itafungwa mabao mengi au kushindwa kutwaa kombe kwa miaka 50 watu wanabaki upande huohuo tu. Ninachoamini mimi wajinga wanazidi kupungua na warevu wanaongezeka kila siku nchini kutokana na matukio mbalimbali nchini na kimataifa.
 
...kila mtu anayo haki kamili ya kujiunga na chama cha siasa atakacho lakini ni kweli Machali anaipenda CCM au kuna kitu kilichomsukuma kurudi CCM? ni kitu gani hasa hicho?. Hakuna asiyebandikwa bei mgongoni!!
lowasa kashahama jana usiku.
 
Back
Top Bottom