Baada ya kutoka bungeni - hii ndio post ya Julius Mtatiro... Vitisho makanishani

Kuna kitu watu hawajui kamwe maoni ya wengi hayawezi kuwa ya wachache kwenye demokrasia ya kweli wengi ndio wanashinda.

Warudishe pesa walizochukua hao
 
Kainerugaba msemakweli.. alitwambia Lukuvi ni darasa la saba na alisomea ualimu wa UPE.. Ni kilaza na bogus hasiyeweza kupima mambo..ukijumlisha UKILAZA WA LUKUVI+UCCM=UZUZU
 
hawa jamaa nilishawauri siku nyingi sana waungane! Watanzania wanahitaji ukombozi na uhuru kamili si kupitia utitiri wa vyama lakini kwa kuwaondoa ccm!

Ukawa mbaki vivyo hivyo hadi ccm waondoke! Muulizeni raila odinga mbinu alizotumia kuing'atusha kanu madarakani

ccm b + ccm c =?
 
Nawaomba chonde chonde, wana UKAWA, vaeni HELMET rudini bungeni.

Leo atakaewakilisha katika vikao vya uongozi aende akiwa na akili za kisayansi. ajitahidi kupanga maneno na waje na msimamo mzuri na matakwa mazuri.
 
mi najua jk aliitisha katiba ili wananchi akili yetu ilale huko yeye amalize muda wake vizuri kama angekuwa na nia ya kweli mbona kwenye ahadi zake raisi za mgombea hakuwai kuhaidi kwenye ilani ndo kabisa
 

Thursday April 16th 2014


Julius S. Mtatiro

TUMEJIONDOA RASMI KATIKA MCHAKATO WA KATIBA!!


Tumeamua kuwaachia CCM waendelee na mchakato wa katiba
wanayoitaka.


Kwa sababu wameyakataa maoni ya wananchi, na Sasa wameanza vitisho kwenye makanisa, ati wananchi wakipitisha serikali Tatu Wao CCM wataikabidhi nchi iongozwe kijeshi ni vema Sasa tuwaache.

Kwa nia njema kabisa, hatutaki kuwa sehemu ya matusi, kauli nzito
kabisa za ubaguzi na kila aina ya upuuzi.

Kama CCM walikuwa na katiba yao wacha waendelee kutengeneza.


Sisi tunarudi kwa wananchi.

Katiba mpya itapatikana tu pale kutakapokuwa na nia njema hasa kutoka kwa vyama kinachoongoza dola.


Mungu ibariki Tanzania!

Kwa hiyo walitaka "Mawazo ya Wachache" ndio yapite?
 
Thanks. Wapuuzi wanasema warudishe hela. Mimi nadhan wakurudisha hela ni waliobaki. Ambao wameenda kinyume na walochoagizwa kukifanya.
Ni kweli kabisa ulichosema, wanaopaswa kurudisha hela ni hao wajumbe wa CCM waliobaki.

Wakumbuke kuwa wajumbe wote wa Tume ya katiba waliteuliwa na Mwenyekiti wao wa CCM, Jakaya Kikwete, na Tume hiyo imetumia bilioni 60 za walipa kodi kukusanya maoni ya wananchi.

Iweje leo Tume hiyo iliyoteuliwa na Mwenyekiti wao wa CCM, na iliyokuwa na wajumbe wengi makada wa CCM, lakini kwa kuwa waliamua kuuvua unafiki na kusimamia maoni ya wananchi kwa uaminifu mkubwa, ndiyo wameonekana wasaliti!!
 
"Ndiyo maana, wachache wetu tulipendekeza tuwe na Bunge Maalum la kuchaguliwa na wananchi moja kwa moja. Lakini watawala wetu, pamoja na watawala watarajiwa na wengi wa wanaharakati, katika busara zao na kwa maslahi yao, hawakutilia maanani pendekezo letu. Tumepoteza nafasi ya kipekee ya kihistoria ya kuwa na Bunge Maalum la kuchaguliwa, jambo ambalo limetufikisha hapa tuliko" - Profesa Issa Shivji: Dhana na Maana ya Bunge Maalum la Katiba
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/608682-prof-shivji-ampa-darasa-mzee-warioba-wajumbe-wa-bunge-la-katiba-someni-ili-msiyumbe.html

Hayo ni mawazo ambayo Shivji aliyatoa wakati akiwa na akili nzuri kabla hajachakachuliwa na CCM. Alikuwa mtu mzuri sana ingawa leo hii sina hamu naye amemezwa na mafisadi
 
Ni hivi toka mwanzo wa utungaji wa sheria hii ya mabadiliko ya katiba mpya tuliona hila zilizokuwa zikifanywa na ccm. Walifikia mpaka mahali viongozi waandamizi wakasema hakuna haja ya katiba mpya rejea Kombani na mwanasheria mkuu. Kinachotokea sasa ni matokeo ya msingi mbovu wa sheria hii. Niliwahi kusema siku za nyuma kitendo cha kumfanya rais wa nchi kuwa juu ya katiba ni lazima kingeleta balaa mbele ya safari. Iweje rais ambaye ni tunda la katiba ageuke tena yeye kuwa juu ya katiba? Matokeo yake ndio hayo kujaza wanaccm ndani ya bunge la katiba na tunashuhudia watu wasio na mawazo huru ya nini wananchi wanakitaka. Ushahidi ni hapo wanaccm wote pamoja na wateule wengi wa rais kupingana na maoni yaliyoletwa kihalali na tume ya mabadiliko ya katiba mpya chini ya jaji Warioba.

Mimi nasema hivi ilitakiwa rais asiwe juu ya mchakato huu kabisa na ilitakiwa liundwe baraza huru ambalo ingewekwa sheria ambayo ingewazua wajumbe wote wa bunge hilo maalum la katiba kutokugombea tena nafasi yoyote ya uongozi mara baada ya kutunga katiba mpya ili kuepusha conflict of interest. Kinyume na hapo tutaishia kuona maoni ya wananchi kugeuzwa upuuzi na badala yake tulazimishwe eti hata Askofu Pengo na shehe mkuu wanataka serekali 2. Hivi hawa viongozi wa dini ndio mmeona ni wengi kuliko hata hayo maoni ya waumini wao ambao kwa wingi wao wanataka serekali 3?
 
Tatizo lilianzia kwa anayejiita rais wa nchi. Kikwete. He is not strategic. Anafikiri nchi inaongozwa kama familia? Huwezi ukajenga nchi na maadui zako ktk serikali kwa kuhonga vyeo eti uti ukiamini uko salama. Foolish leaders.
 
Hivi jumla ya ukawa wako wangapi? Zitto na yule rais wa walimu wamebaki au wamesepa?
 
Kwa uwelewa wangu mdogo nilijiuliza, hivi kwa utaratibu wa bunge hili kujaza wanasiasa (Wabunge) wote kujadili hii Rasimu ya katiba kupata Katiba Mpya, na kutaka mwisho kutumia utaratibu wa kupiga kura na tukijua fika wengi wape, mi naona kama kamuvi hivi maana mwisho wake tunajua, kwamba akifa adui muvi imekwisha, Naamini UKAWA wameliona hilo na wamechukua hatua coz wao ni wachache na hoja zao zinachukuliwa hazina mashiko Tusiwabeze wana hoja Ikiwezekana MH Rais asikilize ushauri wa upande wa pili avunje Bunge aunde Bunge la Kidemokrasia kuanza moja si ujinga Tunataka Katiba Bora.
 
Back
Top Bottom