Baada ya kumkataa mtoto eti sasa tuonane

Baada ya kumkataa mtoto eti sasa tuonane

Usikatae wito...nenda msikilize alafu utaamua cha kufanya baada ya kujua nia alokuitia
 
wanaume wengi san uoga wa maisha unawasumbia japo tamaa mbele mauti nyuma. msililize tu maana inawezekana amaejifikiria na kuona ameacha gold nyuma akikimbilia mawe

wengi sana hawapendi majukumu angalia asikunyanganye mtoto
akajidai single dady
player!!!!!
 
Hakuna mwanaume anayetelekeza mtoto bila sababu ya maudhi au mashaka ya kubambikiwa kutoka kwa Mwanamke,tunawajua sana wanawake wa sasa wakoje,hatukatai wako waume wenye shida lakini kwa % kubwa husababishwa na wanawake wenyewe

Na wewe ni lazima mmoja wao. Kamchukue huyo mtoto ulio mkataa.
 
just go....maisha ni kupanda na kushuka,things might change for the best.also ni haki ya mwanao kuwa na baba na hili litapunguza matatizo mtoto atakapokuwa coz utamueleza baba alivyomkataa na vado ukampa chance ya pili ya kumsikiliza
 
Yote hayo usingeliyapata kama ungelifunga ndoa na kupata mtoto/watoto ndoani...

Kwa kawaida sisi wanadamu tunapoasi (tunapotenda dhambi) huwa tunafungulia mlango wa mambo mengine mabaya kuambatana nasi...

Na matokeo ya uasi wowote huwa ni adhabu, wewe mleta mada umeadhibiwa kwa jamaa kuukana mzigo wake bila shaka naye jamaa kuna adhabu kaipata huko alipokuwa...

Huu ni wakati wa kurekebisha kosa nambari moja ambalo nyote mlishirikiana kufanya...

Unapokataa mwanao asimjue babaye maana yake unajilazimu kushiriki kosa nambari mbili ambalo jamaa yako alilianzisha nalo ni mtoto wenu kuishi katika hali ya kukataliwa...

Ni wewe mwenye ufunguo wa ama mwanao aishi akimtambua mtu anayemuita baba au lah...

Siku zote kurudia kosa si kosa bali ni kuimarisha zaidi kosa...

Incredible
 
Huyu bwana alinipa mimba na aka mkataa mtoto wake.Amenikatia sana simu kila nilipo mtafuta na mengine mengi mengi nisiwachoshe kwa kuwasimulia.Muda wa miezi kadhaa sasa umepita toka katoto kazaliwe na yeye akatae nimesha zoea maisha yangu napambana kumlea mwanangu peke yangu as a single mom na msaada pia kutoka kwa ndugu.Sasa baba wa mtoto kanitafuta ananiambia tuonane akirudi kwa sasa yupo safari.Naomba mnipe mawazo je akirudi nimskilize anasemaje au niachane naye kama alivyo nitendea yeye kipindi chote cha ujauzito mbaka nilivyojifungua.Nakumbuka wakati namwambia mtoto tayari alicho nijibu ni i don't want it and I have nothing to do with it

mpotezee kabisa tena ikiwezekana badili no ya cm kabisaaa
 
wewe keshakuona zoba lake akienda huko akiachwa anarudi zake hakupaswa kukataa kwa matusi mimba hamna mtu mwenye mapenzi yakweli nawewe tangu una mimba hadi unajifungua roho isimuume hata kidogo. kiufupi hakupendi namkirudiana ulijue hatoona shida kukuacha tena
 
yupi huyo??
Halafu mtu mwenyew mbishi kama kama bata mchanga.
Kila nikikuambia nipe unabana muone hips

Aiseee hebu chunga hizo kauli zakoo....zina utata mimi na wewe huwa tunaombana nini
 
Wewe ndio unajua ukweli kwa nn jamaa alikataa wakat ule...kama ulikuwa ni mtu wakutokuwa muaminifu jamaa ana haki zote zakukimbia mimba na ana haki yakurudi sa hivi na unatakiwa umsikilize tena ikiwezekana na msamaha unaomba kabisa kwa wewe kutokuwa muaminifu wakat ule hadi yote yakatokea...maana kwa maisha haya kwa kweli wanawake mnabambikia sana watu..
 
Aiseee hebu chunga hizo kauli zakoo....zina utata mimi na wewe huwa tunaombana nini

haa! Ww vp kwan hujui? Inamaana ntawezaje kuikana mimba yako bila kuiomba njia ya kupitishia mimba?
 
Back
Top Bottom