Baada ya kumkataa mtoto eti sasa tuonane

Baada ya kumkataa mtoto eti sasa tuonane

huggies

Member
Joined
Jul 1, 2014
Posts
54
Reaction score
1
Huyu bwana alinipa mimba na aka mkataa mtoto wake.Amenikatia sana simu kila nilipomtafuta na mengine mengi mengi nisiwachoshe kwa kuwasimulia.

Muda wa miezi kadhaa sasa umepita toka katoto kazaliwe na yeye akatae nimeshazoea maisha yangu napambana kumlea mwanangu peke yangu as a single mom na msaada pia kutoka kwa ndugu.

Sasa baba wa mtoto kanitafuta ananiambia tuonane akirudi kwa sasa yupo safari.

Naomba mnipe mawazo, je akirudi nimskilize anasemaje au niachane naye kama alivyonitendea yeye kipindi chote cha ujauzito mpaka nilivyojifungua.

Nakumbuka wakati namwambia mtoto tayari alichonijibu ni i don't want it and I have nothing to do with it.
 
Tukushauri nini hapo? Amua tu kama ni mbwai ni mbwai tu. Mpelekee mtoto akamwone, mwoneshe mtoto mpaka asubuhi na mchana mmoja. Atakuwa ameyasafisha maziwa ya mtoto, utapata nguvu mpya kumnyonyesha mtoto wenu. We vip??
Mwezi ujao njoo hapa kutueleza unavyo tapika.
Hivi ulijisikiaje alipo kuambia mwonane baada ya mitusi yoote alokupa. Ama kweli, kipenda roho hula nyama mbichi. Unapataje ujasiri hata wa kuandika hapa kuomba msaada?? Mjibu MAKAVU; Sikujui kabisa.
 
Kubali mlee mtoto, tatizo siku hizi wanaume wanabambikiwa sana mimba....hapo ukute kashaambiwa mtoto kafanana naye ndo maana kajirudisha...

Ila usikubali haraka haraka....pozi muhimu mtoto wa kike, hakikisha na yeye anaonja joto ya jiwe hata kidogo.
 
Msikilize anataka kusema nini? Miezi sita sio mingi. Yawezekana akili ilimruka ya woga wa majukumu, au kuhisi kuwa umembambikiza baada ya yeye kusikia/kuhisi mambo fulani kuhusu wewe wakati huo, sasa akili imemrudi. Hajachelewa bado. Angekuwa kamzira mtoto mpaka anafikia miaka kama tano na kuendelea, ingekuwa ngumu kumuelewa. Umepitia changamoto kwa huo muda toka ujauzito mpaka sasa, hivyo kama na mzazi mwenzio atataka kukusaidia kwa kutambua wajibu wake, mkubalie. Ila sijui anachotaka kukwambia!
 
Kama unampenda mtoto na una uhakika kuwa yeye ndiye baba wa mtoto msikilize anachotaka kusema, kama alivyosema barafuyamoto, na ikiwa yuko tayari kurudiana na wewe itakuwa ni vyema pia kwa mtoto mumlee kama familia.
 
Last edited by a moderator:
Yani watu siku hizi tuna roho mbaya! Lakini siwezi kumjaji jamaa kwa sababu inategemea uhusiano wenu ulikuwaje na whether alikuamini ama unaaminika( kutokana na kuibiwa sana huwezi aminiwa kirahisi hadi mtoto amuone kama anamfanania). Anyway, hukustahili kutendewa hivyo. Pole sana na Hongera sana kwa kumpata na kumlea mtoto.

Msikilize tu baba wa mtoto huna jinsi (If not for him basi for your beloved child). Hata kuwe na father figure kwenye maisha ya mtoto. Japo ndo vile ila ndo binadamu wa sasa tulivyo tena. Yani kama mwanaume alikuwa ni integer lazima awe whole lakini kwa sasa tutaomba kuwe na theluthi mwanaume, nusu mwanaume na robo mwanaume na kwa wanawake vilevile


Huyu bwana alinipa mimba na aka mkataa mtoto wake.Amenikatia sana simu kila nilipo mtafuta na mengine mengi mengi nisiwachoshe kwa kuwasimulia.Muda wa miezi kadhaa sasa umepita toka katoto kazaliwe na yeye akatae nimesha zoea maisha yangu napambana kumlea mwanangu peke yangu as a single mom na msaada pia kutoka kwa ndugu.Sasa baba wa mtoto kanitafuta ananiambia tuonane akirudi kwa sasa yupo safari.Naomba mnipe mawazo je akirudi nimskilize anasemaje au niachane naye kama alivyo nitendea yeye kipindi chote cha ujauzito mbaka nilivyojifungua.Nakumbuka wakati namwambia mtoto tayari alicho nijibu ni i don't want it and I have nothing to do with it
 
Wadada wamekuwa na kasumba mbaya ya kubambikia watu mimba. Wakati mwingine mtu ana nia nzuri lakini anahisi kubambikiwa. Aweza kuwa mtu mstaarabu lakini kwa dunia ya Leo ni lazima kuwa mwangalifu.

Kwa kipindi cha urafiki kabla ya ujauzito ulikuwa nao wangapi???
 
Huyu bwana alinipa mimba na aka mkataa mtoto wake.Amenikatia sana simu kila nilipo mtafuta na mengine mengi mengi nisiwachoshe kwa kuwasimulia.Muda wa miezi kadhaa sasa umepita toka katoto kazaliwe na yeye akatae nimesha zoea maisha yangu napambana kumlea mwanangu peke yangu as a single mom na msaada pia kutoka kwa ndugu.Sasa baba wa mtoto kanitafuta ananiambia tuonane akirudi kwa sasa yupo safari.Naomba mnipe mawazo je akirudi nimskilize anasemaje au niachane naye kama alivyo nitendea yeye kipindi chote cha ujauzito mbaka nilivyojifungua.Nakumbuka wakati namwambia mtoto tayari alicho nijibu ni i don't want it and I have nothing to do with it

We dada acha ujinga,kama kweli huyo mzazi mwenzio Yuko serious hakuna cha kumlipiza kisasi,usijiangalie peke yako,jaribu kumpa haki za Msingi mwanao ikiwemo haki ya kumjua biological father na pia kupata matunzo na mapenzi ya wazazi wote,jaman mi nimelelewa na mama peke yake,nimekosa mengi sana tofauti na waliolelewa na baba na mama,kama kuna chance ya motto kuishi na wazazi wote then why not?maisha ni safari ndefu,chukua uamuzi sahihi ila papuchi ibanie kwanza had akuchukue kwanza na mwanao asije akawa anakujaribu!
 
Yani watu siku hizi tuna roho mbaya! Lakini siwezi kumjaji jamaa kwa sababu inategemea uhusiano wenu ulikuwaje na whether alikuamini ama unaaminika( kutokana na kuibiwa sana huwezi aminiwa kirahisi hadi mtoto amuone kama anamfanania). Anyway, hukustahili kutendewa hivyo. Pole sana na Hongera sana kwa kumpata na kumlea mtoto.

Msikilize tu baba wa mtoto huna jinsi (If not for him basi for your beloved child). Hata kuwe na father figure kwenye maisha ya mtoto. Japo ndo vile ila ndo binadamu wa sasa tulivyo tena. Yani kama mwanaume alikuwa ni integer lazima awe whole lakini kwa sasa tutaomba kuwe na theluthi mwanaume, nusu mwanaume na robo mwanaume na kwa wanawake vilevile
Hawa wadada wewe unawaamini Sana eeeh!! Tafuta kuwafahamu vizuri, hadi jamaa kukataa huwezi jua. Kuna wadada ni hatari tena moto. Nimesikia kabisa mdada akisema " mimba sio yake lakini sins jinsi, hamna wa kunisaidia kulea". Hawa watu waone tu hivi.
 
Unaweza kurudiana nae ila ndo hivyo....usijipe mia kwa mia...tegemea chochote kutokea...
 
kuna sababu iliyopelekea hayo wala simlaumu coz nowdayz tunalea watoto ambao si wetu basi tu ukifikiria unatulia tu kwa kutumia ule usemi kitanda hakizai..............so kamsikilize na mkubaliane mumlee mtoto kvp
 
Back
Top Bottom