Trust None
JF-Expert Member
- Feb 12, 2018
- 1,260
- 4,415
Kukiwa na tukio linaloteka nyoyo na hisia za watu basi huyu jamaa huja na "kituko" kama utani vile kwa lengo la ku-'divert ideas' za watu na kuwasahaulisha kabisa kile walichokuwa wakijadili.
Sasa upepo umembadilikia.... Fuatilia...
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amezitaka mamlaka husika kuchukua hatua za kisheria kwa anayehusika na uhalifu wa kimtandao wa kutumia jina lake kwenye ukurasa wa Twitter.
Makonda ametumia ukurasa wake wa Instagram kukanusha kuhusika na taarifa inayosambazwa katika mtandao huo juu ya wanaolaghai wanawake na kudai kuwa hana akaunti kwenye mtandao wa Twitter wala Facebook isipokuwa Instagram kwa jina la Baba Keagan.
“Naomba kuutaarifu umma kwa mara nyingine tena. Mimi Paul Makonda Mkuu wa Mkoa sina A/c TWITTER hata FACEBOOK. Mtu anaetumia jina langu ana malengo mabaya tena Kwa faida iliyojaa uovu.”
“Naziomba mamlaka zinazohusika kuchukua hatua kwani kunasiku atatoa kauli itakayoleta taharuki katika jamii. A/c pekee ni nayo tumia ni ya Instagrame tena Kwa jina la baba_keagan.”
Lengo ni lilelile kuwatoa watu kwenye reli.
Sasa upepo umembadilikia.... Fuatilia...
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amezitaka mamlaka husika kuchukua hatua za kisheria kwa anayehusika na uhalifu wa kimtandao wa kutumia jina lake kwenye ukurasa wa Twitter.
Makonda ametumia ukurasa wake wa Instagram kukanusha kuhusika na taarifa inayosambazwa katika mtandao huo juu ya wanaolaghai wanawake na kudai kuwa hana akaunti kwenye mtandao wa Twitter wala Facebook isipokuwa Instagram kwa jina la Baba Keagan.
“Naomba kuutaarifu umma kwa mara nyingine tena. Mimi Paul Makonda Mkuu wa Mkoa sina A/c TWITTER hata FACEBOOK. Mtu anaetumia jina langu ana malengo mabaya tena Kwa faida iliyojaa uovu.”
“Naziomba mamlaka zinazohusika kuchukua hatua kwani kunasiku atatoa kauli itakayoleta taharuki katika jamii. A/c pekee ni nayo tumia ni ya Instagrame tena Kwa jina la baba_keagan.”
Lengo ni lilelile kuwatoa watu kwenye reli.