Baada ya huu mshikemshike, watakutana kweli?

Baada ya huu mshikemshike, watakutana kweli?

Ufisadi wa Chadema umewaathiri vipi Watanzania? Na hii Serikali haramu iliyojaa magaidi inashindwa vipi kuwakamata majambazi ndani ya Chadema na kuwafungulia kesi za ujambazi badala yake inaishia kuwabambikia kesi FEKI!? Acha kuonyesha ujuha wako hadharani.

Ni wapi hamna ufisadi TZ hii? Huko kwenye vyama vyenu ndiyo majambazi yamejificha. Kama siyo mzee wa kiumri basi ni mzee wa jf (ref lini ulijiunga)
 
Binafsi nilihisi CDM walitaka kumpima huyu mama kama ana ubavu, yule kijana Mdude aliyeachiwa kutoka gerezani kauli yake binafsi ilinikera sana, nilianza kuhisi harufu ya kutaka kumjaribu mama, yanayoendelea kwa sasa tuliyatarajia baada ya kuona kasi ile.....la kustaajabisha huyu mama alionekana muungwana sana ila wanaume wakataka kumshika makalio....sasa nadhani tunakoelekea si penyewe yetu macho.....
 
Akilihutubia bunge, Rais Samia aliahidi kukutana na vyama vya siasa, si chama kimoja au kiongozi wa chama fulani. Katika hivyo vyama kuna CCM, CHADEMA, CUF, SAU, ADC, nk.; na hakutaja siku, tarehe, mwezi wala mwaka wa kukutana.

Atakapoitisha kukutana na vyama hivyo, yeyote atawakilisha, si lazima awe kiongozi wa chama ngazi ya juu.

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Rais alianza kazi kwa kuonesha upendo na uungwana wa hali ya juu. Kitendo hili likatafsiriwa na chadema kama unyonge na wakaanza kumtolea lugha ya dharau. Alianza Mdude, akaja Mbowe kwa kumpangia Rais akutane nao haraka! . Choko mchokoe pweza
 
Hoja yako, Nyani, unataka wasikutane au unashangilia kwamba mkutano huo hautakuwepo?! Ni sawa kwa wapigania legacy mkutano ule ungepunguza punguza! Usicheke mapema lakini, kesho tu wanasiasa wanaweza kukushangaza!
 
Tatizo Mbowe alikuwa na haraka sana ya kukutana naye..."mama" alivyoanza kuupiga mwingi akaona yeye na wenzake wanapoteza relevancy wakabadili gia angani na kuanza kudai katiba mpya kwa ubabe huku akijua kabisa matokeo yake.
CHADEMA wanamdharau sana Rais SSH kwa kuwa ni mpole, wanataka afuate matakwa yao. Hapana akifanya hivyo atakuwa siyo Rais wa Tanzania. Freeman Mbowe yeye mwenyewe hachezewi hivi akiwa Mwenyekiti wa CHADEMA.

Tumemuona alivyolinda kiti chake cha UENYEKITI mpaka kwa kumwaga damu. Kwa nini wasimsikilize Rais SSH aliposema Katiba isubiri kwanza ajenge uchumi?

Mbona waliufyata kwa Mwendazake ambaye alikuwa katili kupitiliza? Wananchi watawachoka kwa kuwa chama cha harakati na matukio. Kajipangeni namna ya ku-deal na Rais SSH. Wananchi wanamkubali anavyochukua hatua kupanga uchumi.

Na Katiba hajakataa, kasema nipeni muda.

Lakini akina Mbowe wanataka wamuendeshe kama gari bovu? Anadhani Rais SSH ni kama akina Catherine Ruge wa BAWACHA?? HAPANA huyu ni Rais wa Tanzania na anayoyafanya tunayaona
 
Hahahahahajaha si mbowe alivyotoka msiban Moshi akaelekea Mwanza moja kwa moja akasema akamatwe yeye sasa 😂😂😂😂😂😂 mtoto akililia wembe mpe umkate

Angetulia tu kwanza maana nchi ina pitia mengi magumu yy kazi yake kutupigia kelele tu
 
Ulitaka Chadema wasikemee uvunjifu wa sheria kwasababu palikuwa na miadi ya kukutana na Rais?

Wacha ushamba.
Hivi mbowe na sabaya kwa sasa wana tofauti?
Mbona mmemsahau sabay na kesi inaendelea?
 
Hahahahahaha Katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi itainua nchi yetu sana. Watanzania kura zetu zitaanza kuheshimiwa na hivyo kuchagua Viongozi watakao bila chama chochote kile kupora uchaguzi.
Chama kilicho madarakani KIKIVURUNDA uchaguzi unaofuata kinaondolewa na kuwekwa kingine.
Katiba itaheshimiwa na yoyote atakayeidharau wa chama chochote kile cha moto atakiona.
Watanzania tutakuwa na uhuru na haki ya kuikosoa Serikali ya chama chochote kile bila hofu ya kutekwa na kupotea au kuuawa.
Mahakama zitakuwa huru kufanya kazi kwa haki na si ilivyo hivi sasa ambapo zinatumika na genge la wahuni wa maccm kubambikia kesi FEKI za ugaidi, uchochezi, uhujumu uchu
Vyombo vya habari vitakuwa na uhuru na haki ya kufanya mijadala yoyote ile hata kama itaikosoa Serikali bila hofu ya kufungiwa au kutekwa.
Ripoti za CAGs zitaheshimiwa na kufanyiwa kazi vile ipasavyo hivyo kumaliza wizi, ubadhirifu na ufisadi uliokithiri ndani ya taasisi mbali mbali za Serikali.
Heshima yetu kama Nchi ambayo sasa imepotea itarudi tena na Tanzania na Watanzania kuheshimiwa tena popote pale duniani.
Hii ndiyo Tanzania niitakayo mimi.

Weekend njema Mkuu kumbuka kuchukua hatia zote za tahadhari dhidi ya COVID-19 ikiwemo kuvaa mask 😷 🙏🏾
Buddah kenya kuna katiba mpya na tume huru ya uchaguzi ila what is always happening kwenye kila uchaguzi?
 
USIKURUPUKE kuja kuonyesha ujuha wako hadharani. Kama hujui kitu ULIZA!!!
Buddah kenya kuna katiba mpya na tume huru ya uchaguzi ila what is always happening kwenye kila uchaguzi?
 
Rais Samia yupo madarakani sasa kwa miezi minne.

Katika muda wake huo madarakani, amekutana na makundi kadhaa sasa: vijana, wazee, maaskofu, akina mama, nk.

Sina hakika kama keshakutana na Waislamu wenzake. Nadhani bado hajakutana nao. I wonder why…maana tayari keshakutana na Wakristo!!

Miezi mitatu iliyopita Mheshimiwa Freeman Mbowe wakati akihutubia taifa alisema kuwa wamemwandikia barua mheshimiwa Rais na kuomba wakutane naye.



Mpaka sasa Bi. Mkubwa hajakutana nao. Sijui amepanga kukutana nao lini.

Na baada ya kukamatwa kwa Mbowe na hizo tuhuma za ugaidi tulizoambiwa, sijui kama huo mkutano wao utakuja kutokea!

Maana itakuwa ni maajabu Rais wa nchi kukutana na ‘gaidi’ na kufanya naye mazungumzo.

Bi. Mkubwa anaupiga mwingi huku kazi ikiendelea.

Kashapoteza akili huyu bibi.
 
Back
Top Bottom