Nakubaliana na wewe kudai haki na uhuru haina muda maalum, lakini naangalia kwa umakini njia waliyokuwa wanaitumia CHADEMA ilikuwa hailengi kudai haki wala uhuru, ilikuwa ziaidi kumtega Samia ili aonekane ana kandamiza demokrasia. CHADEMA walianza vizuri na shughuli zao za CHADEMA digital, na walifanikiwa kutembea mkoa kwa mkoa bila drama zozote, walitakiwa waelimishe wananchi kuhusu umuhimu wa katiba chini kwa chini kwanza...leo hii Mbowe amekamatwa, walitoa rai kwa wananchi aachiwe ikifika tarehe 22 vinginevyo wataitisha maandamano yasiyo na kikomo , nini kimetokea ?
Walisema 2020 baada ya matokeo ya uchaguzi wananchi waandamane nini kilitokea ?
Kama hawajifunzi kupitia makosa yao kamwe hawawezi kupata matokeo chanya kwenye mabadiliko ya uhuru na haki wanayoyataka.
View attachment 1865035