Baada ya huu mshikemshike, watakutana kweli?

Baada ya huu mshikemshike, watakutana kweli?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,094
Reaction score
136,675
Rais Samia yupo madarakani sasa kwa miezi minne.

Katika muda wake huo madarakani, amekutana na makundi kadhaa sasa: vijana, wazee, maaskofu, akina mama, nk.

Sina hakika kama keshakutana na Waislamu wenzake. Nadhani bado hajakutana nao. I wonder why…maana tayari keshakutana na Wakristo!!

Miezi mitatu iliyopita Mheshimiwa Freeman Mbowe wakati akihutubia taifa alisema kuwa wamemwandikia barua mheshimiwa Rais na kuomba wakutane naye.



Mpaka sasa Bi. Mkubwa hajakutana nao. Sijui amepanga kukutana nao lini.

Na baada ya kukamatwa kwa Mbowe na hizo tuhuma za ugaidi tulizoambiwa, sijui kama huo mkutano wao utakuja kutokea!

Maana itakuwa ni maajabu Rais wa nchi kukutana na ‘gaidi’ na kufanya naye mazungumzo.

Bi. Mkubwa anaupiga mwingi huku kazi ikiendelea.
 
Tatizo Mbowe alikuwa na haraka sana ya kukutana naye..."mama" alivyoanza kuupiga mwingi akaona yeye na wenzake wanapoteza relevancy wakabadili gia angani na kuanza kudai katiba mpya kwa ubabe huku akijua kabisa matokeo yake.
Ulitaka Chadema wasikemee uvunjifu wa sheria kwasababu palikuwa na miadi ya kukutana na Rais?

Wacha ushamba.
 
Subra miaka yote! Bajeti ipi unasemea,kama bajeti ya kununua ndege haikuwepo na wamenunua hata katiba wafanye hivyo.
Pia wapunguze posho za wabunge kwa asilimia 70 pesa zitapatikana.
Katiba aliyoratibu JK ilifeli wapi?.

wapunguze posho unategemea kabisa watafanya hilo jambo?hata kama ingekua wewe?
 
Makamanda mmezira?
Sizitaki mbichi hizi🐇
images (77).jpeg
 
Mzazibari mwislam kumpa kesi ya ugaidi mkristo wa KKKT...ni lini na wapi duniani mkiristo akawa gaidi wakati dini yetu toka Sunday school tunafundiswa Upendo na kusamehe saba mara sabini..kama bwana wetu Yesu alivyowasamehe wale waliomtesa na kumuua....time.

Hi nchi inapelekwa siko...wakrito tusikubali kuwa sisi ni magaidi..
 
Inashangaza sana baada ya miezi minne tu samia kaamua kumpa Mbowe kesi mbaya sana ya Kigaidi eti alikuwa anapanga kuuwa Viongozi wa Serikali. Miaka mitano iliyopita Mbowe kafanyiwa udhalimu na dhuluma za kutisha sana lakini bado alikuwa anatoa kauli za kujenga mshikamano na kuwa na maridhiano

.

Wiki mbili tu zilizopita Samia alimtumia salaam za pole Mbowe kufuatia kifo cha Kaka yake Charles Mbowe. Inakuwaje gaidi ambaye Tangu mwaka jana ilionekana alikuwa ana panga kuwaua Viongozi wa Serikali atumiwe salamu za pole!?



Rais Samia yupo madarakani sasa kwa miezi minne.


Katika muda wake huo madarakani, amekutana na makundi kadhaa sasa: vijana, wazee, maaskofu, akina mama, nk.

Sina hakika kama keshakutana na Waislamu wenzake. Nadhani bado hajakutana nao. I wonder why…maana tayari keshakutana na Wakristo!!

Miezi mitatu iliyopita Mheshimiwa Freeman Mbowe wakati akihutubia taifa alisema kuwa wamemwandikia barua mheshimiwa Rais na kuomba wakutane naye.



Mpaka sasa Bi. Mkubwa hajakutana nao. Sijui amepanga kukutana nao.

Na baada ya kukamatwa kwa Mbowe na hizo tuhuma za ugaidi tulizoambiwa, sijui kama huo mkutano wao utakuja kutokea!

Maana itakuwa ni maajabu Rais wa nchi kukutana na ‘gaidi’ na kufanya naye mazungumzo.

Bi. Mkubwa anaupiga mwingi huku kazi ikiendelea.
 
Ulitaka Chadema wasikemee uvunjifu wa sheria kwasababu palikuwa na miadi ya kukutana na Rais?

Wacha ushamba.
Nguvu iliyokuwa inatumika ilikuwa sio kukemea kuvunjwa kwa sheria ila kudai katiba bila kusikiliza upande wa pili na lugha iliyokuwa inatumika ilikuwa "confrontational" , kwa nini nguvu hiyo na ubabe haukutumika wakati wa Magufuli ?
 
Kudai HAKI na UHURU hakuna muda maalum. Nchi hii ina mfumo wa vyama vingi kwa miaka 30 sasa. Je, tusubiri miaka mingine 30 ili kudai Katiba Mpya hasa ukitilia maanani yaliyojiri katika uchaguzi uliopita ambao mimi nauita UCHAFUZI!?
Tatizo ni timimg ya kuidai hiyo katiba na nguvu iliyokuwa inatumika, walijua walichokuwa wanakotafuta na wamefanikiwa kwa % kubwa.

Kwanini nguvu hii haikutumika kabla ya kuingia uchaguzi mkuu 2020?
 
Back
Top Bottom