William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,584
- 10,466
- Thread starter
-
- #21
Azimio la Arusha was a living document iliyobeba dira na 'definition' ya taifa tulilokuwa tunataka kujenga. Iliweka misingi na taratibu za kiutawala pamoja na mahusiaono ya kijamii. Azimio la Arusha lilibeba 'mipaka' na 'barabara' za kupita ili tupate aina ya taifa tulilotaka.
Kwa mtazamo wangu a living document inaweza kufanyiwa update kutokana na mabaliko ya lazima ambayo yanaigusa jamii husika. Lakini sisi tulilifuta Azimio la Arusha kimoja bila mbadala ya maana! Sasa hivi William unaweza kusema Tanzania ni nchi ya aina? Au tuna-aspire kuwa Taifa gani? Na kama unajua aina ya taifa linalojengwa kwa sasa nini misingi ya ujenzi huo?
Ni rahisi sana kuona Azimio la Arusha si chochote kama hujalisoma kwa makini na kuelewa logic yake. Na kwa bahati mbaya au nzuri sasa hivi tunaishi post-Azimio la Arusha, hivyo tunaweza kutofautisha kabisa pande mbili hizi za shilingi. Kulaumu kwamba hali tuliyonayo imesababishwa na Azimio la Arusha ni dalili ya uelewa mdogo wa Azimio lenyewe. With Azimio la Arusha tusengekuwa tunamumunya maneno kuhusu mawaziri wananen waliovurunda!
Azimio la Arusha lilikuwa linahimiza kutafuta majibu ya matatizo yetu kama nchi from within na sio ku-import solutions! Hakuna nchi iliyoendelea kwa kutegemea wawekezeji huku asilimia kubwa ya population yake ikiwa iko outside the system! CCM ya sasa hawatataka kulisikia Azimio la Arusha kwa sababu wamejipa 'hati miliki' ya nchi. Watalisema vibaya kwa ujumla wake bila kuangalia kipengele kimoja kimoja na kufanya marekebisho pale inapobidi. Wanafaidika moja kwa moja na hii nyumba isiyokuwa na msingi na incase inaanguka tayari wameshajiwekea mpango wa dharura kama kuwa na account visiwa ya Jersey huko Uingereza!.
Well, heshima mbele sana JF,
- Ninaomba kusema tena na tena, we were Dead wrong na idea za Azimio La Arusha, infact ndilo limetufikisha hapa tulipo yaani tumekwama hili taifa, hatujui tunakokwenda wala tulikotoka. Halafu wanatokea wasomi wanaodai eti turudi kwenye Azimio, hilo Azimio limetushinda mwanzoni kwa nini kuna wanaoamini tutaliweza sasa?
- Recently, nimeona wale wengi walioachwa kwenye uongozi wa juu yaani kwenye mlo, wakililia Azimio, halafu ninachukizwa sana ninapoona media inawapa free lunch hawa waliokosa mlo, sijawahi kuwasikia wakisema Azimio liliwahi kumfunga kiongozi gani wa juu mwizi, sijawasikia wakisema Azimio lilifanya nini cha maaana mpaka wanalilia!
- Mwalimu, yes was the greatest ever, lakini Mwalimu alikuwa na mapungufu makubwa mawili, hakujua;- !. Uchumi 2. Sheria, hivi vitu viwili Mwalimu simply hakuvijua kama alivijiua basi hakuvitilia maanani, na ndivyo vinavyolitafuna taifa letu sasa akiwa hayupo!
- WA-TANZANIA, KAMA TUNATAKA KUSONGA MBELE NA KIJIREKEBISHA TUACHANE NA MANENO YA AZIMIO LA ARUSHA, KWA SABABU NDILO HASA LIMETURUDISHA NYUMA SANA, LISIRUDI, LIENDE ZAKE, NA TUSILIJADILI MAANA NI SHETANI LILILOTURUDISHA NYUMA SANA, SASA TWENDE MBELE NA UBEPARI NA UTAWALA UNAOHESHIMU SHERIA NDIO THE BEST WAY MBELE!
RESPECT PEOPLE!
Mr. Willie @DSM City!
- Living document ni ile Constitution ya USA tu, maana siku zote ina majibu ya maswali magumu ya taifa kila yanapozuka, wanaikimbilia inawapa majibu unajua Why ni kwa sababu ilijikita kwenye Sheria zaidi, kuliko miiiko ya uongozi. A living document inatakwia itoe mwanga panapokuwa giza sio kutoa impossible theories kama za Aazimio la arusha, kwanza haikuweza kufanaya anything muanzilishi wake akiwa hai, sasa hivi kweli kuna aliyetegeema itatusaidia akiwa hayupo?
- I have a lot of respect na Mwalimu, as individual na siku zote ninatenganisha Azimio na yeye kama kiongozi, kwenye maneno ya Azimio la Arusha, hakututendea haki taifa hili na ninasikitika sana kwamba wasomi wanaotakiwa kutusiadia na wao hawana majawabu ya matatizo tuliyonayo sasa wamejikita kujificha kwenye maneno ya Azimio la arusha!
William.
- Prof. Shivji ndio wale wale hana hoja hana jipya, toka enzi za Mwalimu kazi yake ni kilalamika tu sijawahi kusikia akitoa hoja za kisasa zinaendana na maisha ya sana, Mwalimu alipokuwepo alikuwa kaimponda sana, sasa amegeuka kwua mtetezi wa siasa zake, ukweli ni kwamba hana jipya!
- Azimio limetufikisha hapa tulipo, lime-create tabaka katika jamii yetu, limetufanya tumekuwa wanafiki wa kutupwa hatuna msimamo, kazi kulia lia tu bila kusema what is the alternative, huwezi kujenga uchumi na miiiko ya uongozi, unajenga uchumi kwa regulate wanaosimamia uchumi. na huwezi ku-regulate uchumi kama huna sheria kali.
- Wa-Tanzania mpaka tutakapokubali kwamba Azimio ndilo limetumaliza ndio tutaanza kufikiria kuendelea, ama sivyo tutakuwa tunazunguka hapa hapa tulipo!
William.
vipi kuhusu Nape Maana nae analihitaji azimio hilo lirudi,unamweka ktk kundi la Prof Shivji?
lakini mwalimu alisema
kaeni chini na mlisome vyema azimio la arusha na mseme wapi panatatizo ili pafanyiwe kazi,cha kushangaza mkakimbila Zanzibar na kuanzisha azimio la zanzibar ambalo liliwapa mwanya wa kugawana kile kilicho anzishwa na azimio la arusha,uchumi ukamilikiwa na wachache,kikundi cha watu kika anza kunyonya waliowengi
sijui kama unayaona hayo mkuu
- Living document ni ile Constitution ya USA tu, maana siku zote ina majibu ya maswali magumu ya taifa kila yanapozuka, wanaikimbilia inawapa majibu unajua Why ni kwa sababu ilijikita kwenye Sheria zaidi, kuliko miiiko ya uongozi. A living document inatakwia itoe mwanga panapokuwa giza sio kutoa impossible theories kama za Aazimio la arusha, kwanza haikuweza kufanaya anything muanzilishi wake akiwa hai, sasa hivi kweli kuna aliyetegeema itatusaidia akiwa hayupo?
- I have a lot of respect na Mwalimu, as individual na siku zote ninatenganisha Azimio na yeye kama kiongozi, kwenye maneno ya Azimio la Arusha, hakututendea haki taifa hili na ninasikitika sana kwamba wasomi wanaotakiwa kutusiadia na wao hawana majawabu ya matatizo tuliyonayo sasa wamejikita kujificha kwenye maneno ya Azimio la arusha!
William.
Mkuu William Malecela,
Unaposema Azimio la Arusha ndio kiini cha matatizo yanayotukabili leo kama taifa, una maana gani hasa, kwani azimio la arusha per se ni pana sana. Ungefunguka kidogo tungeweza pata mjadala mzuri zaidi.
Kwenye red: Ni wazi huelewi nini maana hasa ya a 'living document', na hapo ndipo pa kuanzia. Tofautisha na 'biblical' document.
Willie! What is your angle in this? what is your altenative at all?
Kamanda, jamaa huwa anchukua maneno bar na kwenye vijiwe na kuleta bila fact wala research
Muulize amelisoma azimio la arusha?? na chanzo ni document au implementation au change of our own policies??
Mkuu wangu baharia mbona unaturudisha nyuma kiasi hicho.. Wewe Azimio la Arusha ndilo limekusomesha bure na ukajisifia kwa kumpa sifa zote Nyerere leo unaliponda.. Nyerere hakujuja Uchumi vipi?..Ni Azimnio la Arusha lilojenga reli ya Tazara, Azimio la Arusaha lkililojenga viwanga vya matairi General tyre, UFI, viwanda vya nguo, saruji, nguvu za umeme ukayarudi disco la Mbowe hata siku moja umeme haukukatika, leo unaliponda wakati ndio kwanza tulijenga vitu hivyo tukashindwa kuviendesha sisi wenyewe kama walivyoshindwa China na Russia..
Au mwenzetu una maana tofauti ya Uchumi? maana kuwa na wazo zuri ukashindwa kufanikiwa haina maana hata wazo lenyewe halikuwa na maana. Leo hii umetaka kugombea Ubunge wa EA na ukashindwa je tuseme wewe huna maana tena kwa sababu umeshindwa huko..Tafadhali mkuu wangu Azimio la Arusha lilikuwa na mapungufu yake kimfumo hasa pale tulipochagua serikali kumiliki uchumi lakini haina maana hakuna kitu hicho ktk somo la Uchumi. Asiyejua Uchumi atafanya jambo ambalo halipo ktk somo la Uchumi lakini ukifanya ikashindikana haina maana hujui uchumi..
Na unaposungumzia Sheria ni sheria gani?..ati kwa nini Nyerere aliendelea kuwatumia viongozi wabovu, hivi nikuulize tulikuwa na wasomi wangapi? angembadilisha mzee Malecela akamweka nani ikiwa wote walikuwa wabovu. Wewe hapo ulipo nambie mtu hata mmoja ambaye wewe ulimwoina kingozi mzuri Nyerere angemtumia na hakumtumia. Haya leo hii pamoja na kuwa nao kibao na tumebadilisha mfumo mbona ndio kwanza tunatokomea zaidi shimoni tuna excuse gani?
- sihitaji kusoma anything, ninahitaji kuangalia tu kwa macho yangu na kuamua kwamba Azimio was dead kabla hata halijaanza, wewe soma halafu njoo hapa useme tulifikaje hapa tulipo hili taifa kama sio Azimio lilokufa!
William.
Only and if only, this is possible....!!!!!????- Tuanze upya na utawala wa sheria na uchumi mbele, that is all! hakuna short cut!
William.
- Mkuu wangu please with all due respect, naomba tuongelee marekebisho ya katiba mpya sio Azimio la Arusha, tumekwama kwa sababu hatujui sheria, hatujui uchumi tulifikiri Serikali ndio inatakwia kufanya kila kitu, kumbe sio zile zilikua dead theories za Azimio la Arusha, sasa tunatka mapinduzi ili twende wka mbele lazima tucahane na mambo ya kizamani.
William.
- sihitaji kusoma anything, ninahitaji kuangalia tu kwa macho yangu na kuamua kwamba Azimio was dead kabla hata halijaanza, wewe soma halafu njoo hapa useme tulifikaje hapa tulipo hili taifa kama sio Azimio lilokufa!
William.