Azim Dewji amemwambia Rais Samia: Rais Wetu Aliyepita(John Magufuli) Alikuwa na Nia Yake na Wewe (Samia Suluhu) Una Yako, Wasikufitinishe
Source : JamiiForums
========
Azim Dewji: Mama kila kitu inategemea kwenye nia, Rais wetu mpendwa aliepita alikuwa na nia yake na wewe sasa hivi una nia yako, wasikufitinishe wala wasikusumbue. Hawa wakorofi utatuachia sisi watu wa madhehebu tutawaombea na Mungu atawaangamiza alivyomuangamiza Firaun.
Tabia moja ya binadamu, sisi ni wasahaulifu sana na Mungu analijua hilo. Inasikitisha kuona kwamba sisi tunasahau mazuri yaliyofanywa na hayati Magufuli, kuna mambo mengi amefanya lakini mimi nitagusia moja.
Alisumbuka tangu uwaziri wake kujenga barabara kwenye nchi hii lakini wapo wanasiasa wamepauka au wamefilisika kisiasa wanakuja kusema barabara inasaidia nini!
Wanasahau kwenye nchi yetu moja tulitaka kwenda Bukoba ilibidi twende Kenya, tupite Uganda halafu ndio tufike Bukoba, ni miaka 10 tu kabla tulikuwa tunashindwa kwenda.
Kwenye miaka mitano ya Rais Magufuli sisi watu wa Dar es Salaam hatujawahi kusikia mlio wa bunduki, hatujawahi kupata shida ya umeme, siku hizi watu wameacha kuuza majenereta.