Azam TV acheni usanii

Azam TV acheni usanii

Lussadam

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2007
Posts
1,423
Reaction score
998
Hawa jamaa naona wameanza usanii fulani,

Mimi ni mteja wa Azam TV na nimekuwa nikilipia kifurushi cha TZS 23,000. Huwa natizama zaidi Channel moja tu INVESTIGATION DISCOVERY. Sasa hapa juzi bei imeshuka kwenda TZS. 20,000.Nimelipa lakini nimeshindwa kuipata hiyo channel, kabla ya kukitekeleza king'amuzi chao,nikataka nipate maelezo toka kwao.

Nimepiga simu kuulizia kama hiyo channel ipo aliyepokea simu kanieleza ndiyo ipo kifurushi cha TZS20000 na akaniambia subiri mpaka simu ilipokatika. Baada ya hapo simu zao either zinadai network bussy au inaishia pale Foe English place One for Kiswahili place Two. Ukipiga usiku wa saa 5 inakueleza kuwa muda wa kazi ni mpaka saa nne usiku.

Nimeandika hapa baada ya kuona sipati majibu kwani nimeandika na Email sijajibiwa ingawa siku nyingine email zinajibiwa kwa haraka.
 
Hata mimi kile cha 18 kimekua. 13 lakini azam sports 1&2 Hamna. Sawa hivi bora niangalie channel ya mapishi tu.
 
Mkuu hamia dstv ulipe 44,000 utavipata hivyo unavyovitaka
 
Mimi waliniudhi walivyoondoa channel ya FightSport wakati ndo ilinishawishi kununua king'amuzi
 
Acheni kulalamika, wiki mbili zilizopita niliweka Post ikisema Azam wanatuuzia vifurushi ndani ya mifuko myeusi ya plastiki, mligoma kuchangia hapo nilisema viwepo vipeperushi ili kabla ya kulipia kifurushi tukijue kilichomo ndani yake, sasa haya ndiyo madhara ya kununua kifurushi ndani ya mfuko mweusi wa plastiki.
 
Ili kuipata place 2 hapo nimecheka kinyama
 
Sahivi mambo yao yashaanza kuwa meusi
 
Hamia DSTV. Japo Bei zake ujipange sio Kama huko ulipo. Beberu hanaga shobo
 
Back
Top Bottom