Azam FC yamtimua kocha Omog

Azam FC yamtimua kocha Omog

Huyu kocha aliwapa ubinhwa,tatu zimewachanganya bana
 
hawana lolote Azam,wamemfukuza kwa lipi sasa..!?
 
mjini kila mtu anauliza kwanini alimtoa tchetche na kumuingiza morad...!? sasa sijui ndio hilo liliromuondoa.....!?
 
George best nsimbe sasa atachukua mikoba mpaka kocha mpya atakapopatikana
 
Wewe mtanzania kweli? Hata kutufariji wenzio kidogo unaona shida?
 
Kalimangonga alienda kuongeza elimu ya ukocha Uingereza. Kwa kutimuliwa kwacOmog, bila shaka Kali yuko njiani kurejea Azam.

Kali Ongara nae alitimuliwa wakasingizia anaenda kusoma,afadhali safari hii wamesema kabisa kuwa wamemtimua kocha
 
tatizo watu wa AZAM hususani watangazaji wao hawajikiti kubainisha mapungufu ya timu yao. muda wote wanasifia tuu mara ooh aishi manula anastahili kuchezea ulaya na blah blah nyingine. ukweli ni kwamba licha ya utajiri wao lakini wachezaji wao wana quality ya kawaida tu tofauti na wao wanavyovumisha. kitu pekee cha wao kupigania ni kushawishi TFF iruhusu usajili wa wachezaji wa kigeni kwa idadi isiyo na kikomo. kwa kufanya hivyo azam na timu nyingine za tz zitaweza kupambana kwenye michuano mikubwa
 
Omog ameonyesha kuishiwa mbinu. Mambo siku hizi ni performance based bana. Azamfc inaonyesha kiwango cha chini siku hizi. Timu ilifungwa na JKT Ruvu hapo Chamazi; halafu ikafungwa na Ndanda huko Mtwara: kama haitoshi Wajelajela waliofungwa bao 5 na simba, wakajipatia pointi mgongoni mwa Azamfc.
 
Namshukuru Mungu kwa kuwa utabiri wangu umetimia. Nilisema baada ya Maximo na Phiri anayefuata ni Omog wa Azam FC. Kipindi kile sikueleweka. Hongera Yanga, Simba na Azam kwa kuvaa sare moja ya kufukuza makocha.
 
Kocha kama kashindwa kazi lazima afukuzwe sisi tunataka maendeleo sio kelele

Ebu tuache masihara, Azam walikuwa na mategemeo ya kuchukua klabu bingwa? Au kuna mambo mengine? Hii ndo mara ya kwanza wanashiriki na kupata ushindi wa nyumbani kwa mara ya kwanza ilikuwa ni kitu cha kivunia dhidi ya timu yenye uzoefu ya El merreikh.
Azam wakianza siasa za simba na yanga, watatoweka taratibu kama harufu ya ushuzi maana hata fanbase wa ukweli hawana zaidi ya wa mikopo!
 
Tabia ya kufukuza makocha haijengi timu. Hata wachezaji hawawezi kuendeleza vipaji vyao kwasababu wanabadirishiwa makocha kila siku. Inabidi kujitathmini ili kujua sababu ya kufungwa ni nini sio kukurupuka kufukuza kocha. Fikiria shule inayobadirisha walimu inaweza kufaulisha kweli?
 
Back
Top Bottom