Ayatollah Khamenei ajitokeza hadharani kwa mara ya kwanza

Ayatollah Khamenei ajitokeza hadharani kwa mara ya kwanza

The Zanzibar Echo

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2025
Posts
490
Reaction score
836
Kiongozi Mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei amejitokeza hadharani kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa mzozo wa Iran na Israel, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya serikali.

Picha za runinga ya serikali zilimuonyesha akiwasalimia waumini kwenye msikiti siku ya Jumamosi kabla ya tamasha la waumini wa Kishia linalofahamika kama Ashura.

Mara ya mwisho Khamenei kuoneka ilikuwa katika hotuba iliyorekodiwa wakati wa mzozo na Israel, ulioanza tarehe 13 Juni na wakati ambapo makamanda wakuu wa Iran na wanasayansi wa nyuklia waliuawa.

Israel ilifanya mashambulizi ya kushtukiza katika maeneo ya nyuklia na ya kijeshi nchimi Iran. Hatua ilisababisha makabiliano makali baada ya Iran kulipiza kisasi kwa mashambulizi ya angani yaliyolenga Israel.

Wakati wa vita vya siku 12 na Israel, Khamenei alionekana kwenye TV katika ujumbe wa video na kulikuwa na uvumi kwamba alikuwa amejificha kwenye chumba chini ya ardhi.

Siku ya Jumamosi matangazo ya vyombo vya habari vya Iran yalitawaliwa na mwonekano wa Khamenei, huku wafuasi wakionyesha kufurahia kumuona kwenye televisheni.

Khamenei anaonekana akimgeukia kasisi mkuu Mahmoud Karimi, akimhimiza "kuimba wimbo wa taifa, O Iran".

Wimbo huo wa uzalendo ulipata umaarufu mkubwa wakati wa mzozo wa hivi majuzi na Israel.
1751795903363.png
 
Huyu mzee yupo imara japo amepooza mkono wake wa kulia
 
Mama anapokanyaga ardhi ya mataifa, anabeba heshima ya Tanzania, anatangaza amani, na anaonyesha uongozi wa hekima unaoheshimika kimataifa. Ziara yake ni ishara ya mshikamano wa kweli wa Afrika.
#KaziNaUtu
#TunasongaMbele
 
Sawa


Vita Imeisha, Amani Imetawala Sana Sana Lakini Aendelee Kujificha Wale Hawaaminiki
 
Mimi kama role model wake nampongeza kwa kukifanya taifa la Iran kuendelea kuwa kubwa na imara.

Ameniambia matamanio ya kuifuta Israel yako pale pale.
 
Back
Top Bottom