Aweso ahitimisha ratiba ya kikazi Umoja wa Mataifa New York, atoa shukrani kwa Kaimu Mwakilishi wa Kudumu

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Jan 5, 2013
666
835
IMG-20230327-WA0271(1).jpg


Waziri wa Maji ameshiriki kikao cha Shukrani na kuagana na watumishi wa Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Umoja wa Mataifa, New York. Watumishi hao wameongozwa na Mhe. Balozi Dkt. Suleiman Haji Suleiman, Kaimu Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Umoja wa Mataifa, New York.

Katika kikao hicho amewashukuru kwa maandalizi na kufanikisha ushiriki wa Tanzania kwenye Mkutano wa Maji wa Umoja wa Mataifa yaani the United Nations 2023 Water Conference uliofanyika kuanzia tarehe 22 hadi 24 Machi 2023 Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York.

IMG-20230327-WA0272(1).jpg


Amesema Kupitia sapoti ya ubalozi wetu tuliweza kuwasilisha hotuba ya taifa kueleza namna Tanzania ilivyopiga hatua katika kuwapatia huduma ya maji wananchi wake pamoja na mipango mbalimbali iliyopo katika kuendeleza sekta ya maji nchini kama sehemu ya utekelezaji wa Lengo namba 6 la Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa. Hotuba hiyo ilitolewa kwenye Baraza kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 22 Machi 2023.

IMG-20230326-WA0640(1).jpg

Vilevile, amemshukuru Mhe Balozi na timu yake kwa kufanikisha kufanya mazungumzo na wabia mbalimbali wa maendeleo ili kujadiliana namna wabia hao wanaweza kuisaidia Tanzania kutekeleza progamu yake ya maji ya mwaka 2023 - 2030 inayotarajiwa kuzinduliwa mwezi Mei 2023.
 

Attachments

  • IMG-20230326-WA0639(1).jpg
    IMG-20230326-WA0639(1).jpg
    158.2 KB · Views: 3
  • IMG-20230327-WA0273(1).jpg
    IMG-20230327-WA0273(1).jpg
    295.4 KB · Views: 3
View attachment 2567272

Waziri wa Maji ameshiriki kikao cha Shukrani na kuagana na watumishi wa Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Umoja wa Mataifa, New York. Watumishi hao wameongozwa na Mhe. Balozi Dkt. Suleiman Haji Suleiman, Kaimu Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Umoja wa Mataifa, New York.

Katika kikao hicho amewashukuru kwa maandalizi na kufanikisha ushiriki wa Tanzania kwenye Mkutano wa Maji wa Umoja wa Mataifa yaani the United Nations 2023 Water Conference uliofanyika kuanzia tarehe 22 hadi 24 Machi 2023 Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York.

View attachment 2567273

Amesema Kupitia sapoti ya ubalozi wetu tuliweza kuwasilisha hotuba ya taifa kueleza namna Tanzania ilivyopiga hatua katika kuwapatia huduma ya maji wananchi wake pamoja na mipango mbalimbali iliyopo katika kuendeleza sekta ya maji nchini kama sehemu ya utekelezaji wa Lengo namba 6 la Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa. Hotuba hiyo ilitolewa kwenye Baraza kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 22 Machi 2023.

View attachment 2567270
Vilevile, amemshukuru Mhe Balozi na timu yake kwa kufanikisha kufanya mazungumzo na wabia mbalimbali wa maendeleo ili kujadiliana namna wabia hao wanaweza kuisaidia Tanzania kutekeleza progamu yake ya maji ya mwaka 2023 - 2030 inayotarajiwa kuzinduliwa mwezi Mei 2023.
Maji hakuna mitaani yeye kiherehere na mapacha ya wazungu,tuna viongozi wa hovyo sana kipindi hiki

USSR
 
Tunataka tuletewe maji kutoka marekani kwa msaada wa watu wa marekani.
 
Maendeleo Africa yataletwa na WaAfrica sio Wazungu wa Ulaya na America.

Maendeleo ya Tanzania yataletwa na watanzania kwa kufanya kazi kwa bidii, nguvu na maarifa mengi na sio kutegemea misaada na ushauri wa weupe wa ulaya na america.

Ulaya na America wao Africa wanamini ni shambani kwao na muda wowote wanaweza kuingia na kulima.
Muarabu na Mhindi wanaamini waAfrica ni watumwa wao na tupo kwa ajili ya kuwatumikia.

WaAfrica tusimame tuijenge Africa na kupendana wenyewe, WaAfrica tuwakatae vibaraka wa wakoloni ambao tuko nao na wapo wanamtumikia mkoloni kuendelea kutukoloni.
 
Vyanzo vya maji tunavyo vyakutosha kila mahala, nguvu kazi tunayo, hela tunayo tunaichezea hovyohovyo.
 
Back
Top Bottom