Ramea
JF-Expert Member
- Mar 19, 2015
- 2,146
- 4,054
Kuna tatizo lilinipata ambalo mizizi yake ni kutokana na mfumo wa maisha ya sasa yaliyosababishwa na huyu ndugu yetu wa Chato.
Kwanza kabisa Mimi naamini sana Mungu kwakuwa nilipitia malezi hayo katika familia na baadae shule za seminari za kikatoliki na hata wenzangu nilosoma nao wengi sasa ni mapadre.
Mwezi uliopita nilipatwa na tatizo kubwa na miongoni mwa watu walionishauri na kunipa pole ni Mzee mmoja ambaye ni mteja wangu na ananiamini kama akipata huduma toka kwangu nikiwa kwa office.
Mzee huyu alinishauri tuangalie mbadala wa jambo husika kwa kuonana na Sangoma ambaye alifanikisha hata mambo yake binafsi, nilisita lakini baadae nikamkubalia.
Majira ya sa9 alasiri tuliambatana hadi kwa Fundi/mganga na mambo yalikuwa hivi;
Mganga alijifunika kitenge kichwani, akatoa chupa chenye vitu vyekundu ndani yake na kuanza kupandisha mapepo. Kisha akaanza kusema matatizo yangu kabla sijamweleza chochote, alipatia kwa 70% na maswali nilimpiga.
Badae akasema kwa tatizo langu lazima liambatane na kafara! Nilistuka na kuogopa kumbe alihitaji tu jogoo anayeanza kuwika, nikaona sio kesi atafutwe na kisha akamchinja na damu nikaikinga kwenye kile chupa alichokuja nacho mwanzo....akakata miguu ya kuku akanipa na ile damu akaniambia ile miguu niichimbie mahali fulani(ilinipasa niende usiku) kwani ni mbali na ninakoishi na si vema jamii ikiniona. Na ile chupa ya damu niipasue palepale nilipochimbia miguu nikiipiga kwenye jiwe.
Cha ajabu, maneno ambayo nilipaswa kuyasema wakati napasua chupa hicho ni ya Kimungu "Mwenyezi Mungu kama kweli upo, Tuma malaika wako watatue tatizo hili la (sitolitaja)" na aliniahidi ndani ya Siku 3 mambo yatakuwa Shwar ingawa Siku Tatu zimepita ila matumaini yapo japo kwa mbali.
SHIKAMOO BABA MAGUFULI... HUKU MTAANI VYUMA VIMEKAZA, LEGEZA KIDOGO.
Kwanza kabisa Mimi naamini sana Mungu kwakuwa nilipitia malezi hayo katika familia na baadae shule za seminari za kikatoliki na hata wenzangu nilosoma nao wengi sasa ni mapadre.
Mwezi uliopita nilipatwa na tatizo kubwa na miongoni mwa watu walionishauri na kunipa pole ni Mzee mmoja ambaye ni mteja wangu na ananiamini kama akipata huduma toka kwangu nikiwa kwa office.
Mzee huyu alinishauri tuangalie mbadala wa jambo husika kwa kuonana na Sangoma ambaye alifanikisha hata mambo yake binafsi, nilisita lakini baadae nikamkubalia.
Majira ya sa9 alasiri tuliambatana hadi kwa Fundi/mganga na mambo yalikuwa hivi;
Mganga alijifunika kitenge kichwani, akatoa chupa chenye vitu vyekundu ndani yake na kuanza kupandisha mapepo. Kisha akaanza kusema matatizo yangu kabla sijamweleza chochote, alipatia kwa 70% na maswali nilimpiga.
Badae akasema kwa tatizo langu lazima liambatane na kafara! Nilistuka na kuogopa kumbe alihitaji tu jogoo anayeanza kuwika, nikaona sio kesi atafutwe na kisha akamchinja na damu nikaikinga kwenye kile chupa alichokuja nacho mwanzo....akakata miguu ya kuku akanipa na ile damu akaniambia ile miguu niichimbie mahali fulani(ilinipasa niende usiku) kwani ni mbali na ninakoishi na si vema jamii ikiniona. Na ile chupa ya damu niipasue palepale nilipochimbia miguu nikiipiga kwenye jiwe.
Cha ajabu, maneno ambayo nilipaswa kuyasema wakati napasua chupa hicho ni ya Kimungu "Mwenyezi Mungu kama kweli upo, Tuma malaika wako watatue tatizo hili la (sitolitaja)" na aliniahidi ndani ya Siku 3 mambo yatakuwa Shwar ingawa Siku Tatu zimepita ila matumaini yapo japo kwa mbali.
SHIKAMOO BABA MAGUFULI... HUKU MTAANI VYUMA VIMEKAZA, LEGEZA KIDOGO.