Upepo wa maandamano. Unaandamana na ma Tamko. Na kabla ya Tamko kuna habari za kiintelijensia. Wanaotoa taarifa za kiintelijensia kwa sasa ni Polisi...Who cares.
Nimeuona upepo huu ukitokea Afrika ya Kaskazini, walao kwa mwaka huu. Watu wanaandamana (Tunisia, Algeria) na kuna dalili kama hizo Sudan na Ivory Coast...Who cares.
Wana CCM na wana CHADEMA wanatoa ma TAMKO. Mimi najiuliza, je, ma TAMKO yatatusaidia? Je, maandamano yatajenga nchi? Who cares.
Nilikuwa napata hofu zamani kuwa Mwl Nyerere akifariki, nani atakuwa Rais...kumbe ikawezekana. Nilimwamini sana. Na onyo lake leo juu ya kuvunja muungano ninalizingatia; kwamba mkivunja mwungano hamtaishia hapo....mtasema sisi ni wazanzibara,....lakini wanasayansi nao wanatuambia, haya mabara tuliyonayo leo, yamepitia historia ndefu; kuna wakati yalikuwa pamoja (kama PANGEA), baadaye yakaachana na kuungana kule na kuachana huku, nk. kumbe kuungana na kutengana ni jambo la kawaida...Who cares.
Hofu yangu mimi, ni pale Polisi watakapoandamana kama ilivyotokea Afrika kusini; je, itatokea nini? Mimi sitaki kuongelea nini kitatokea, lakini niongelee INTELIJENSIA. Je, nani atatupatia taarifa za kiintelijensia? Wo cares?
Mimi natoa TAMKO, maana ni mwaka wa ma TAMKO, kwamba wanaosababisha uchungu wa maisha hadi watu waandamane, tunataka WAJIUZURU MARA MOJA. Je, wasipojiuzuru? Who cares!
Nimeuona upepo huu ukitokea Afrika ya Kaskazini, walao kwa mwaka huu. Watu wanaandamana (Tunisia, Algeria) na kuna dalili kama hizo Sudan na Ivory Coast...Who cares.
Wana CCM na wana CHADEMA wanatoa ma TAMKO. Mimi najiuliza, je, ma TAMKO yatatusaidia? Je, maandamano yatajenga nchi? Who cares.
Nilikuwa napata hofu zamani kuwa Mwl Nyerere akifariki, nani atakuwa Rais...kumbe ikawezekana. Nilimwamini sana. Na onyo lake leo juu ya kuvunja muungano ninalizingatia; kwamba mkivunja mwungano hamtaishia hapo....mtasema sisi ni wazanzibara,....lakini wanasayansi nao wanatuambia, haya mabara tuliyonayo leo, yamepitia historia ndefu; kuna wakati yalikuwa pamoja (kama PANGEA), baadaye yakaachana na kuungana kule na kuachana huku, nk. kumbe kuungana na kutengana ni jambo la kawaida...Who cares.
Hofu yangu mimi, ni pale Polisi watakapoandamana kama ilivyotokea Afrika kusini; je, itatokea nini? Mimi sitaki kuongelea nini kitatokea, lakini niongelee INTELIJENSIA. Je, nani atatupatia taarifa za kiintelijensia? Wo cares?
Mimi natoa TAMKO, maana ni mwaka wa ma TAMKO, kwamba wanaosababisha uchungu wa maisha hadi watu waandamane, tunataka WAJIUZURU MARA MOJA. Je, wasipojiuzuru? Who cares!