Mafyangula
JF-Expert Member
- Jan 16, 2025
- 505
- 887
Jeshi la Polisi limesisitizwa kusimamia ipasavyo Sheria ili kuhakikisha zoezi la Uchaguzi Mkuu linafanyika kwa amani, usalama na kuaminika katika jamii kwani wao ni wadau wakubwa katika kufanikisha zoezi hilo.
Mjumbe wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Mhe.Awadh A. Said, aliyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku moja kwa Maafisa wa Jeshi la Polisi wa Wilaya zote za Unguja katika ukumbi wa Jaji Mstaafu Hamid Mahmoud Hamid uliopo Makao Makuu ya ZEC Maisara, Wilaya ya Mjini Unguja.
Alisema Uchaguzi ni mchakato wa kitaifa unaogusa hisia na matarajio ya wananchi na mustakabali mzima wa nchi hivyo lina jukumu la kuhakikisha mazingira ya usalama yanaimarika nchi nzima.
Mjumbe wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Mhe.Awadh A. Said, aliyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku moja kwa Maafisa wa Jeshi la Polisi wa Wilaya zote za Unguja katika ukumbi wa Jaji Mstaafu Hamid Mahmoud Hamid uliopo Makao Makuu ya ZEC Maisara, Wilaya ya Mjini Unguja.
Alisema Uchaguzi ni mchakato wa kitaifa unaogusa hisia na matarajio ya wananchi na mustakabali mzima wa nchi hivyo lina jukumu la kuhakikisha mazingira ya usalama yanaimarika nchi nzima.