Augustino Ramadhani: Chaguo la system

Augustino Ramadhani: Chaguo la system

Huyu ni Mtu Kutoka Nchi Jilani au Marafiki Zetu Wazanzibar Kwa Maana Zanzibar ni Nchi. CCM wakimleta Huyo Waandike Maumivu Kwa Maana Huyu ni Mzanzibar na Zanzibar ni Nchi Kama ilivyo Burudi au Rwanda.

Rais wa Tanganyika Hapigiwi Mizinga Zanzibar Kama Tulivyoona kwenye Sherehe za Uhuru wa Zanzibar. Hapana Ndani ya CCM leteni Mtaganyika na UKAWA Wataleata Mtanganya.

Zanzibar wenyewe wamesema hawamtambui mchungaji Ramadhani na hawamuungi mkono.
 
Huyu alivyokuwa Jaji Mkuu, RUSHWA ILITAMALAKI SANA KTK MAHAKAMA ZOTE...!!!

Rushwa ndio ilikuwa kama haki ktk mahakama karibu zote wakati huyu alikuwa Jaji Mkuu.... hafai...!!! na hatuchaguliwi viongozi... tunajua tunamtaka nani... huyu kaletwa tu kama kondoo fulani hivi...!!!

Lowassa ndio kila kitu...full stop...!!!

Wapi Lowassa... mutu inayoagiza mvua kutoka Thailand...
 
kweli je watu vijijini wanamfaamu ambako ndo wapinga kura waliko,mimi nawashauri wafanye kama kwa kikwete,
1,magufuli-rais
2,ramadhani-makamu

hii timu itashinda kwa kishindo na inakubalika na itasaidia wabunge wa ccm,ia tutapata baraza la mawazri bora.

Tanzania hatuhitaji vishindo bali tunahitaji mfumo mpya ambao sio ccm kwasababu ccm yote imeoza.
 
rais wa tanzania mzanzibar
rais wa zanzibar mzanzibar

kweli!! ebu lione hili ccm

Haya ndo mambo ya kulazimisha serikali 2, zikiwa 3 hii conflict haipo. Maana Zanzibar kutakua na rais, Tanganyika atakuwepo na yule wa muungano (Tanzania) atatoka pande yoyote kulingana na matakwa ya wakati huo.
 
Ktk dini hilo lipo. History imeandika hivyo. But hili la zamu litakuwa halina mantiki kipindi. Muhimu tuangalie population na umuhimu wa Tanganyika ktk Muungano wa CCM.
 
Mh Red CJ hakujiandaa kuomba nafac yeyote ya Uongozi.
Uongozi wa kuchaguliwa ni maandalizi yenye ushawishi kutoka nafsin. Tukumbuke 1985 - 1990 Mh Late Znz Pres. Abdulwakili alipokuwa Rais wa Znz kipindi kile cha siasa za visiwan kuwa na ushindani wa makundi... Je aliweza kuiongoza Znz kw mategemeo ya wengi?
Labda pawepo na agenda ya kuja kuachia ngazi baada ya muda, kw sababu maalum. Mh VP yule anaetakiwa achukue nchi.
Haifikiriki Red CJ atie nia ghafla ktk kipindi cha mvutano wa makundi ndani ya CCM kipindi hiki cha kuelekea gen election 2015.
 
Tetty
Kikwete hawezi kuweka mtu atakayetishia maslahi yake na ya CCM. Halafu kuna kitu kingine labda watu wengine hawajui. Jaji Ramadhani ni chanda na pete na Mkapa. Ni marafiki kweli kweli. Lakini mimi bila kuangalia KAMA ataweza au hapana nimefurahishwa na kitu kimoja ambacho Kikwete anakaribia kukifanya: Tanzania fomula ilishakuwa UKITAKA URAIS (hata kama huna sifa).. basi 1. Andaa fedha nyingi 2. tengeneza mtandao kwa kununua watu kadiri uwezavyo 3. Tengeneza mazingira ya kuonyesha unakubalika kwa kununua wapambe, media, kura za maoni, vyama na vikundi mbalimbali huku ''ukiwachafua'' wapinzani wako kwa kila namna na mwisho nunua wajumbe karibu wote wa NEC na mkutano mkuu. Sasa hapa Kikwete anakwenda kuonyesha kuwa hii fomula ni fake na japokuwa yeye aliweza kuitumia lakini ilikuwa bahati tu hivyo WATU WENGINE WASIJARIBU! Ahaa... shikamoo mheshimiwa Kikwete! Mwaka huu ni wachumia tumbo wengi wamewekeza kwenye DECI ya kisiasa! Ni kuvuna mabua kwa kwenda mbele!

Kula TANO!

cc. Ritz1
 
Mtazamo wangu mimi naona prof muhongo angefaa zaidi, kwa sababu zifuatazo,
1) haogopi mtu ana maamuzi magumu na amri.
2) Amekaa serikalin miaka miwili tu aliyoyafanya kila mtu anayakubali ukilinganisha na waliokaa rangi miaka ya sabini. pia hawa wengine ambao wapo mwaka leo.
3) Umri unamruhusu ukilinganisha na hawa vijana je miaka kumi ikiisha watafanya kazi gani? ndy yaleyale unakutana na raisi mstaafu disco!!
4) Si rahisi kudanganywa anajua vitu vingi na anazijua nchi zote africa.
- ukinipinga toa na ushahidi wa maandishi.
 
Naona dhambi aliyosema marehemu JKN,imeanza,kesho utasikia achana na wachaga,achana na wanyakyusa, achana na wapemba,achana na wahaya,achana na wakurya... eeh rais anatakiwa awe atakae tufanikishia MAHITAJI yetu WATANZANIA,na si kwamba katoka wapi.HITIMISHO nchi si ya kidini! nyie mnaoleta mgawanyiko wa kidini,mungu awalambe na moto!

Mkuu na wewe umeliona hilo hii dhambi ya ubaguzi haitatubakiza salama.
 
Back
Top Bottom