Kimsingi Serikali inafanya usimamizi wa kina wa shughuli za uzalishaji na Biashara ya madini kupitia kazi nzuri inayofanywa na Wakala wa Ukaguzi wa Madini nchini (TMAA).
TMAA ni Wakala ya serikali yenye wataalamu waliobobea katika kusimamia na kukagua shughuli zote zinazohusiana na uwekezaji, uchimbaji na biashara ya madini kiujumla. Ieleweke kuwa kabla Serikali haijaanzisha chombo hiki, Serikali ilikuwa ikitumia taarifa zilizokuwa zikitolewa na wawekezaji ili iweze kupata stahiki zake mbalimbali ikiwa ni pamoja na kodi ya mapato, ambapo kwa kutumia utaratibu huo Serikali haikuwa inapata taarifa/takwimu sahihi za madini yaliyokuwa yakizalishwa na kuuzwa na hivyo kutokupata stahiki zake sahihi ikiwa ni pamoja na kutokupata kabisa mapato yatokanayo na kodi ya mapato.
Tangu kuanzishwa kwa TMAA Serikali imekuwa ikipata takwimu sahihi za madini yanayozalishwa na hapa nchini ikiwa ni pamoja na kupata stahiki zake zote zinazotokana na biashara ya madini hapa nchini.
Katika kuhakikisha haya yote yanawezekana, Serikali kupitia Wakala imeweka wakaguzi katika maeneo yote yenye uzalishaji wa madini ambao pamoja na mambo mengine wanachukua sampuli za madini (kwa migodi mikubwa ya dhahabu) sampuli ambazo hufanyiwa uchunguzi katika Maabara ya Wakala (ISO 17025 Accredited Laboratory) ili kuweza kubaini ubora wake (madini yaliyopo ndani ya sampuli husika) na kisha kuthaminisha na bei ya madini hayo kwa siku husika katika soko la madini ya metali duniani (LME).
Pamoja na hayo, Wakaguzi wa Wakala hukakiki gharama za uwekezaji na uendeshaji wa shughuli za uzalishaji wa madini kwa lengo la kuepusha uwezekano wa wachimbaji kuipatia Serikali taarifa zisizokuwa sahihi kwa kukusudia au kutokukusudia, taarifa ambazo hupelekea kuonesha hasara na hivyo kuikosesha Serikali mapato yake kama kodi ya mapato. Ukaguzi huu umeiwezesha Serikali kuweza kukusanya mabilioni ya pesa (Zaidi ya bilioni 850) kama kodi ya mapato pesa ambazo hazikuwahi kukusanywa kabla ya Wakala kuanzishwa.
Sambamba na hayo ni jukumu la Wakala kuhakiki kiasi cha fedha kilichotengwa na migodi kwa ajili ya utunzaji na ukarabati wa mazingira katika maeneo ya migodi hiyo ili kupunguza athari za uharibifu wa mazingira sambamba na kutathmini iwapo makampuni ya uchimbaji wa madini yameweka dhamana ya kutosha kwa Serikali ya kugharamia shughuli za utunzaji na ukarabati wa mazingira ya maeneo ya mgodi wakati wa uhai wa mgodi na baada ya shughuli za mgodi kufungwa. Nimepitia taarifa ya mwaka 2015 ya Wakala nimeweza kuona mambo mengi kweli ambayo sikuwahim kuyajua kabla. BIG UP TMAA, Big up Serikali.
http://www.tmaa.go.tz/uploads/TMAA_Annual_Report_2015-4.pdf
Nikirudi kwenye uzi " AUDIT KUBWA MIGODINI"
Binafsi nafikiri ni vyema Serikali iendelee kutumia vyombo vyake mbalimbali katika kusimamia maliasili na ustawi wa jamii ya watanzania.
Ikumbukwe kwamba hatuwezi kusema tunafuta jeshi la polisi na Magereza kwa sababu tuna jeshi la Wanchini Tanzania. Hivyo vyombo mbalimbali vya Serikali vitaendelea kwa mujibu wa sheria kutekeleza majukumu yao kwa mbinu mbalimbali lakini zote zenye lengo la kujenga.
Ni mchango wangu kwa yale niyajuayo juu ya ukaguzi migodini.