Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,100
- 136,724
Watu wanaosoma dini kwa undani wengi wanagundua kwamba ni uongo.
Hata wanaoamua kubaki kwenye Imani wanabaki humo si kwa sababu wanaamini Mungu yupo, wanabaki kwenye Imani kwa sababu wanaamini Imani ina uwezo mkubwa na mzuri wa kuwafanya watu waishi kwa order.
Watu wengi wakijua ukweli kwamba Mungu hayupo watashindwa kuishi maisha ya order.
Hilo ndilo linafanya wengi waliosoma dini/ theology wabaki kwenye Imani.
Si ajabu Papa akawa haamini Mungu yupo, ila anaamini kwamba kuna umuhimu wa kusema yupo.
Na hata wasomi wa fani zingine nao hivyo hivyo.
Wapo ninaowafahamu mimi ambao wanakubali kabisa kuwa hayo mambo ya mungu ni hekaya tu kama za Abunuasi.
Lakini pia wanakubali dini zina baadhi ya vitu ambavyo ni vizuri na kama mtu akijitahidi kwa kadri ya uwezo wake kufuata hayo yaliyo mazuri, mtu huyo ataishi maisha ya uadilifu.
Huwa natolea mfano zile amri 10 za mungu [kwa hisani ya mshua].
Usiue, usiibe, usizini, usiseme uongo....yote hayo ni mambo mema ambayo watu tunapaswa kuyafuata.
Ubaya wa kuyafuata hayo ni upi kwa mfano? Mimi siuoni!
Naona ni mambo mema kabisa.