ATCL kuanza na kosa la kwanza

ATCL kuanza na kosa la kwanza

Msambichaka Mkinga

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2015
Posts
1,646
Reaction score
2,911
ATCL kama yalivyo mashirika mengine ya umma, kila mara imekuwa ikizaliwa na kufa kutokana na muundo wake usiokuwa wa kibiashara. TANESCO isiyo na mshindani yeyote, TTCL ambayo awali haikuwa na mshindani, na mengine mengi yaliyokwishakufa na yaliyouzwa, mashirika yote hayo yalikufa kwa sababu yalianzishwa, kuendeshwa na kusimamiwa kiserikali/kisiasa.

Serikali haijawahi kuendesha biashara ikafanikiwa. Tatizo linaanzia kwenye muundo wa haya mashirika/makampuni. Wanasiasa/viongozi wa serikali ambao kimsingi si wafanyabiashara ndiyo waliotengeneza muundo wa uendeshaji na ndiyo wenye kauli ya mwisho. Vigezo vya wajumbe wa bodi na watendaji wakuu wanavyo wao. Na siku hizi PhD imekuwa ni kigezo kikubwa sana ingawa kiuhalisia, kwa Dunia nzima, ni nadra sana kuwaona wenye PhD wakiwa wafanyabiashara wazuri na waliofanikiwa.

Juzi wakati Mh. Rais akizindua ujio wa ndege mpya alisema ATCL imezaliwa upya, ina ndege mpya, bodi mpya na uongozi mpya, sikusikia kama ina muundo mpya wa uendeshaji na usimamizi. Bado inaonekana ATCL itandeshwa kwa mkono wa serikali.

RAIS - 'ATCL ISITUMIE MAWAKALA WA KUKATISHA TIKETI'

Hili tayari ni agizo ambalo naamini ni agizo lisilo sahihi. Tayari serikali imeanza toka hatua za mwanzo kuingilia uendeshaji wa ATCL. Rais anapoagiza ATCL isitumie mawakala wa kukatisha tiketi inamaanisha ATCL iwe na wafanyakazi waajiriwa kila mahali nchini. Gharama za maelekezo hayo itakuwa kama ifuatavyo:
  • ATCL italazimika kuwalipa wakatisha tiketi mishahara, matibabu, posho, michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii, usafiri, n.k. ATCL italazimika kulipia gharama hizo zote bila ya kujali mkatisha tiketi anakatisha tiketi ngapi au kama amepata wateja au hakupata kabisa
  • ATCL italazimika kulipia ofisi na kuweka miundombinu ya ukatishaji ticket nchi nzima. Ifahamike kuwa ukitaka kuwa na ufanisi unalazimika kuwa na ofisi za ukatishaji tiketi hata mahali ambapo ndege haitui, kwaajili ya kuhudumia abiria wanaotoka maeneo hayo wanaotarajia kutumia usafiri wa ATCL kutokea uwanja ulio karibu
  • ATCL italazimika kuwapa mafunzo wakatisha ticket watakaotapakaa nchi nzima
Wakati ATCL watakapokuwa wanahangaika na kuwa na wakatisha ticket wao na ofisi zao, washindani wao wataendelea kuwa na wafanyakazi wachache, wakiwa na mawakala wengi wanaolipwa kutokana na idadi ya ticket na thamani ya ticket walizokatisha. Hawalipii ofisi, hawalipii matibabu, hawalipii michango ya hifadhi ya jamii, hawalipii likizo ya mfanyakazi. Mawakala wao wanalipwa kutokana na wanachozalisha, wasipozalisha hawalipwi chochote.

ATCL wanaanza na quandary ya kwanza, wafuate maagizo ya mwenye mali au kanuni za biashara? Je, hii ni ya mwanzo na ya mwisho au zitaendelea kuja na nyingine? Kwa kuwa tatizo la msingi la uendeshaji biashara zilizo chini ya serikali halijatatuliwa, haitakuwa jambo la ajabu ATCL kufuata projectile ya mashirika/makampuni ya umma.
 
Well said bro. Hizi ni fact. Maana ama aamue kufuata misingi ya kobiashara au angojee maagizo ya wanasiasa. Hapo hata aje nani atashindwa tu. Lazima amteue mtu na amwamini kwamba atafanya kazi nzuri amwache aendeshe shirika
 
Kaka,
Inasemekana ukitoa ushauri murua ka huu weye ni chocheziii kwa sababu umepinga maagizo au unasababisha watu wapinge maagizo. Lakini, umeeleza kiufasaha japo tofauti ni heading yako ila wenye akili wamesikia ujumbe.
Swali ni Je, kuna CEO atakayethubutu hata kujifanya kasahau maelekezo afuate ushauri wako murua?? Hapo sasa kwa sababu atakuwa ameokoa nyingi tu. Lakini huwezi kujua, pengine kuna mtu wangu au nyumba yangu nataka viufaidi mchezo huu kwa maagizo kufuatwa. Mkija ng'amua nimeshapata angalao nusu.
 
Kaka dunia imebadilika unaweza kata ticket ya ndege popote ulipo bila msaada wa mtu yeyote kilichopo nikuchukua nafasi zetu katika jamii kutoa elimu au kuwasaidia kupata elimu waendane na dunia ya sasa kuleta ukinzani katika kila jambo linalokuwa initiated na serikali haliwezi kukufanya ukawa na busara za kuongoza bali kutatua changamoto zilizoko katika jamii yako ndio ngazi itakayokupandisha daraja na kuwa kiongozi. Je unamkumbuka Marehemu Deo Filikunjombe vaa viatu vyake vikikutosha basi hayo mambo mengine hayatakusumbua. Hongera Magufuli kwa kuonyesha tofauti hata sisi tusio wanachama wa ccm tunaona mwanga kupitia wewe.

ATCL kama yalivyo mashirika mengine ya umma, kila mara imekuwa ikizaliwa na kufa kutokana na muundo wake usiokuwa wa kibiashara. TANESCO isiyo na mshindani yeyote, TTCL ambayo awali haikuwa na mshindani, na mengine mengi yaliyokwishakufa na yaliyouzwa, mashirika yote hayo yalikufa kwa sababu yalianzishwa, kuendeshwa na kusimamiwa kiserikali/kisiasa.

Serikali haijawahi kuendesha biashara ikafanikiwa. Tatizo linaanzia kwenye muundo wa haya mashirika/makampuni. Wanasiasa/viongozi wa serikali ambao kimsingi si wafanyabiashara ndiyo waliotengeneza muundo wa uendeshaji na ndiyo wenye kauli ya mwisho. Vigezo vya wajumbe wa bodi na watendaji wakuu wanavyo wao. Na siku hizi PhD imekuwa ni kigezo kikubwa sana ingawa kiuhalisia, kwa Dunia nzima, ni nadra sana kuwaona wenye PhD wakiwa wafanyabiashara wazuri na waliofanikiwa.

Juzi wakati Mh. Rais akizindua ujio wa ndege mpya alisema ATCL imezaliwa upya, ina ndege mpya, bodi mpya na uongozi mpya, sikusikia kama ina muundo mpya wa uendeshaji na usimamizi. Bado inaonekana ATCL itandeshwa kwa mkono wa serikali.

RAIS - 'ATCL ISITUMIE MAWAKALA WA KUKATISHA TIKETI'

Hili tayari ni agizo ambalo naamini ni agizo lisilo sahihi. Tayari serikali imeanza toka hatua za mwanzo kuingilia uendeshaji wa ATCL. Rais anapoagiza ATCL isitumie mawakala wa kukatisha tiketi inamaanisha ATCL iwe na wafanyakazi waajiriwa kila mahali nchini. Gharama za maelekezo hayo itakuwa kama ifuatavyo:
  • ATCL italazimika kuwalipa wakatisha tiketi mishahara, matibabu, posho, michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii, usafiri, n.k. ATCL italazimika kulipia gharama hizo zote bila ya kujali mkatisha tiketi anakatisha tiketi ngapi au kama amepata wateja au hakupata kabisa
  • ATCL italazimika kulipia ofisi na kuweka miundombinu ya ukatishaji ticket nchi nzima. Ifahamike kuwa ukitaka kuwa na ufanisi unalazimika kuwa na ofisi za ukatishaji tiketi hata mahali ambapo ndege haitui, kwaajili ya kuhudumia abiria wanaotoka maeneo hayo wanaotarajia kutumia usafiri wa ATCL kutokea uwanja ulio karibu
  • ATCL italazimika kuwapa mafunzo wakatisha ticket watakaotapakaa nchi nzima
Wakati ATCL watakapokuwa wanahangaika na kuwa na wakatisha ticket wao na ofisi zao, washindani wao wataendelea kuwa na wafanyakazi wachache, wakiwa na mawakala wengi wanaolipwa kutokana na idadi ya ticket na thamani ya ticket walizokatisha. Hawalipii ofisi, hawalipii matibabu, hawalipii michango ya hifadhi ya jamii, hawalipii likizo ya mfanyakazi. Mawakala wao wanalipwa kutokana na wanachozalisha, wasipozalisha hawalipwi chochote.

ATCL wanaanza na quandary ya kwanza, wafuate maagizo ya mwenye mali au kanuni za biashara? Je, hii ni ya mwanzo na ya mwisho au zitaendelea kuja na nyingine? Kwa kuwa tatizo la msingi la uendeshaji biashara zilizo chini ya serikali halijatatuliwa, haitakuwa jambo la ajabu ATCL kufuata projectile ya mashirika/makampuni ya umma.
 
hizo ndege mradi wake utafeli tu.wala sina haka ya kuelezea mpaka malaika mtoa roho aje aitoe roho JF
 
Ili uweze kukata ticket mahali popote ulipo ni lazima utumie mawakala. Haijalishi unakata ticket kwenye ofisi, simu au kwenye laptop yako, utatumia wakala. Kutaka kila kitu ufanye wewe mwenyewe ndiyo mbinu ya kizamani ya kuendesha biashara.

Hivi unajua hata unapokata ticket yako na kulipia kupitia mitandao kama Airtel, Vodacom na wengineo unatumia wakala? Hii niliyoitoa hapa ni sehemu ya elimu maana usiamini kuwa wanaohitaji elimu ni wale watu wa chini kabisa, kila mtu anahitaji elimu kwenye jambo fulani. Watawala na viongozi wa serikali wanahitaji elimu pia kwenye masuala ya biashara kama ilivyo kwa mfanyabiashara akiingizwa serikalini atahitaji elimu juu ya jinsi serikali inavyofanya kazi. Hakuna anayejua kila kitu, ndiyo maana ukifanya biashara kwa kutaka ufanye kila kitu wewe mwenyewe lazima uangukie pua.

Anayekuonesha mahali penye hitilifu ndiye anayekujenga kuliko anayekushangilia kila mahali. Ndiyo maana hata kwenye management performance assessment wewe uliye boss unatakiwa uwaombe direct reports wako wakueleze your weaknesses na siyo your strengths. Hayo ya Deo RIP ni out of context.

Kaka dunia imebadilika unaweza kata ticket ya ndege popote ulipo bila msaada wa mtu yeyote kilichopo nikuchukua nafasi zetu katika jamii kutoa elimu au kuwasaidia kupata elimu waendane na dunia ya sasa kuleta ukinzani katika kila jambo linalokuwa initiated na serikali haliwezi kukufanya ukawa na busara za kuongoza bali kutatua changamoto zilizoko katika jamii yako ndio ngazi itakayokupandisha daraja na kuwa kiongozi. Je unamkumbuka Marehemu Deo Filikunjombe vaa viatu vyake vikikutosha basi hayo mambo mengine hayatakusumbua. Hongera Magufuli kwa kuonyesha tofauti hata sisi tusio wanachama wa ccm tunaona mwanga kupitia wewe.
 
Umeeleza vyema.

Hata suala la lini na aina gani ya ndege zinunuliwe hapo baadae wangeachiwa ATCL wenyewe sababu ndiyo watakuwa field.

Wanasiasa watanunua ndege ili kuwaziba midomo wakosoaji wao tu.
 
Ili uweze kukata ticket mahali popote ulipo ni lazima utumie mawakala. Haijalishi unakata ticket kwenye ofisi, simu au kwenye laptop yako, utatumia wakala. Kutaka kila kitu ufanye wewe mwenyewe ndiyo mbinu ya kizamani ya kuendesha biashara.

Hivi unajua hata unapokata ticket yako na kulipia kupitia mitandao kama Airtel, Vodacom na wengineo unatumia wakala? Hii niliyoitoa hapa ni sehemu ya elimu maana usiamini kuwa wanaohitaji elimu ni wale watu wa chini kabisa, kila mtu anahitaji elimu kwenye jambo fulani. Watawala na viongozi wa serikali wanahitaji elimu pia kwenye masuala ya biashara kama ilivyo kwa mfanyabiashara akiingizwa serikalini atahitaji elimu juu ya jinsi serikali inavyofanya kazi. Hakuna anayejua kila kitu, ndiyo maana ukifanya biashara kwa kutaka ufanye kila kitu wewe mwenyewe lazima uangukie pua.

Anayekuonesha mahali penye hitilifu ndiye anayekujenga kuliko anayekushangilia kila mahali. Ndiyo maana hata kwenye management performance assessment wewe uliye boss unatakiwa uwaombe direct reports wako wakueleze your weaknesses na siyo your strengths. Hayo ya Deo RIP ni out of context.
mkuu sikuhizi systems zimebadirika! ulisafiri lini mala ya mwisho? I mean international freight? huwakilakitu kiko online na mawakala huwa makampuni mengi wanadiscourage! Ila ni hoja ukizingatia systems ya zamani hapo agents role yao ilikua kubwa
 
ATCL kama yalivyo mashirika mengine ya umma, kila mara imekuwa ikizaliwa na kufa kutokana na muundo wake usiokuwa wa kibiashara. TANESCO isiyo na mshindani yeyote, TTCL ambayo awali haikuwa na mshindani, na mengine mengi yaliyokwishakufa na yaliyouzwa, mashirika yote hayo yalikufa kwa sababu yalianzishwa, kuendeshwa na kusimamiwa kiserikali/kisiasa.

Serikali haijawahi kuendesha biashara ikafanikiwa. Tatizo linaanzia kwenye muundo wa haya mashirika/makampuni. Wanasiasa/viongozi wa serikali ambao kimsingi si wafanyabiashara ndiyo waliotengeneza muundo wa uendeshaji na ndiyo wenye kauli ya mwisho. Vigezo vya wajumbe wa bodi na watendaji wakuu wanavyo wao. Na siku hizi PhD imekuwa ni kigezo kikubwa sana ingawa kiuhalisia, kwa Dunia nzima, ni nadra sana kuwaona wenye PhD wakiwa wafanyabiashara wazuri na waliofanikiwa.

Juzi wakati Mh. Rais akizindua ujio wa ndege mpya alisema ATCL imezaliwa upya, ina ndege mpya, bodi mpya na uongozi mpya, sikusikia kama ina muundo mpya wa uendeshaji na usimamizi. Bado inaonekana ATCL itandeshwa kwa mkono wa serikali.

RAIS - 'ATCL ISITUMIE MAWAKALA WA KUKATISHA TIKETI'

Hili tayari ni agizo ambalo naamini ni agizo lisilo sahihi. Tayari serikali imeanza toka hatua za mwanzo kuingilia uendeshaji wa ATCL. Rais anapoagiza ATCL isitumie mawakala wa kukatisha tiketi inamaanisha ATCL iwe na wafanyakazi waajiriwa kila mahali nchini. Gharama za maelekezo hayo itakuwa kama ifuatavyo:
  • ATCL italazimika kuwalipa wakatisha tiketi mishahara, matibabu, posho, michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii, usafiri, n.k. ATCL italazimika kulipia gharama hizo zote bila ya kujali mkatisha tiketi anakatisha tiketi ngapi au kama amepata wateja au hakupata kabisa
  • ATCL italazimika kulipia ofisi na kuweka miundombinu ya ukatishaji ticket nchi nzima. Ifahamike kuwa ukitaka kuwa na ufanisi unalazimika kuwa na ofisi za ukatishaji tiketi hata mahali ambapo ndege haitui, kwaajili ya kuhudumia abiria wanaotoka maeneo hayo wanaotarajia kutumia usafiri wa ATCL kutokea uwanja ulio karibu
  • ATCL italazimika kuwapa mafunzo wakatisha ticket watakaotapakaa nchi nzima
Wakati ATCL watakapokuwa wanahangaika na kuwa na wakatisha ticket wao na ofisi zao, washindani wao wataendelea kuwa na wafanyakazi wachache, wakiwa na mawakala wengi wanaolipwa kutokana na idadi ya ticket na thamani ya ticket walizokatisha. Hawalipii ofisi, hawalipii matibabu, hawalipii michango ya hifadhi ya jamii, hawalipii likizo ya mfanyakazi. Mawakala wao wanalipwa kutokana na wanachozalisha, wasipozalisha hawalipwi chochote.

ATCL wanaanza na quandary ya kwanza, wafuate maagizo ya mwenye mali au kanuni za biashara? Je, hii ni ya mwanzo na ya mwisho au zitaendelea kuja na nyingine? Kwa kuwa tatizo la msingi la uendeshaji biashara zilizo chini ya serikali halijatatuliwa, haitakuwa jambo la ajabu ATCL kufuata projectile ya mashirika/makampuni ya umma.
Mkuu Msambichaka hivi wale akina Mkinga wa Mndindi ni ndugu zako?
 
ATCL kama yalivyo mashirika mengine ya umma, kila mara imekuwa ikizaliwa na kufa kutokana na muundo wake usiokuwa wa kibiashara. TANESCO isiyo na mshindani yeyote, TTCL ambayo awali haikuwa na mshindani, na mengine mengi yaliyokwishakufa na yaliyouzwa, mashirika yote hayo yalikufa kwa sababu yalianzishwa, kuendeshwa na kusimamiwa kiserikali/kisiasa.

Serikali haijawahi kuendesha biashara ikafanikiwa. Tatizo linaanzia kwenye muundo wa haya mashirika/makampuni. Wanasiasa/viongozi wa serikali ambao kimsingi si wafanyabiashara ndiyo waliotengeneza muundo wa uendeshaji na ndiyo wenye kauli ya mwisho. Vigezo vya wajumbe wa bodi na watendaji wakuu wanavyo wao. Na siku hizi PhD imekuwa ni kigezo kikubwa sana ingawa kiuhalisia, kwa Dunia nzima, ni nadra sana kuwaona wenye PhD wakiwa wafanyabiashara wazuri na waliofanikiwa.

Juzi wakati Mh. Rais akizindua ujio wa ndege mpya alisema ATCL imezaliwa upya, ina ndege mpya, bodi mpya na uongozi mpya, sikusikia kama ina muundo mpya wa uendeshaji na usimamizi. Bado inaonekana ATCL itandeshwa kwa mkono wa serikali.

RAIS - 'ATCL ISITUMIE MAWAKALA WA KUKATISHA TIKETI'

Hili tayari ni agizo ambalo naamini ni agizo lisilo sahihi. Tayari serikali imeanza toka hatua za mwanzo kuingilia uendeshaji wa ATCL. Rais anapoagiza ATCL isitumie mawakala wa kukatisha tiketi inamaanisha ATCL iwe na wafanyakazi waajiriwa kila mahali nchini. Gharama za maelekezo hayo itakuwa kama ifuatavyo:
  • ATCL italazimika kuwalipa wakatisha tiketi mishahara, matibabu, posho, michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii, usafiri, n.k. ATCL italazimika kulipia gharama hizo zote bila ya kujali mkatisha tiketi anakatisha tiketi ngapi au kama amepata wateja au hakupata kabisa
  • ATCL italazimika kulipia ofisi na kuweka miundombinu ya ukatishaji ticket nchi nzima. Ifahamike kuwa ukitaka kuwa na ufanisi unalazimika kuwa na ofisi za ukatishaji tiketi hata mahali ambapo ndege haitui, kwaajili ya kuhudumia abiria wanaotoka maeneo hayo wanaotarajia kutumia usafiri wa ATCL kutokea uwanja ulio karibu
  • ATCL italazimika kuwapa mafunzo wakatisha ticket watakaotapakaa nchi nzima
Wakati ATCL watakapokuwa wanahangaika na kuwa na wakatisha ticket wao na ofisi zao, washindani wao wataendelea kuwa na wafanyakazi wachache, wakiwa na mawakala wengi wanaolipwa kutokana na idadi ya ticket na thamani ya ticket walizokatisha. Hawalipii ofisi, hawalipii matibabu, hawalipii michango ya hifadhi ya jamii, hawalipii likizo ya mfanyakazi. Mawakala wao wanalipwa kutokana na wanachozalisha, wasipozalisha hawalipwi chochote.

ATCL wanaanza na quandary ya kwanza, wafuate maagizo ya mwenye mali au kanuni za biashara? Je, hii ni ya mwanzo na ya mwisho au zitaendelea kuja na nyingine? Kwa kuwa tatizo la msingi la uendeshaji biashara zilizo chini ya serikali halijatatuliwa, haitakuwa jambo la ajabu ATCL kufuata projectile ya mashirika/makampuni ya umma.
Mkuu Msambichaka, kwenye digital world, inawezekana kabisa kuuza tiketi online bila kuwatumia mawakala. Mawakala wanaozungumzwa hapa sio mawakala traveling agents, bali mawakala commissioned agents wana operate kama ofisi za
ATCL, badala ya kutumia mawakala, wanauza tickets on line. Fast Jet wana ofisi zao kule tuu mdege yao inakotua, na hawana wakala popote na mauzo yote ni online!, ila kwa mujibu wa sheria ya kimataifa ya shirika la kimataifa la wakala wa usafiri wa Anga, IATA, wakala yoyote aliyesajiliwa IATA kupitia mtandao wa Galileo, anaweza jyfanya booking yoyote ya ndege yoyote, hivyo abiria wa Tanzania yote watapata tiketi za ATCL popote kupitia traveling agents wengine, ila kule ATCL inatua, lazima wawe na agents for clearing.

Pasco
 
ATCL kama yalivyo mashirika mengine ya umma, kila mara imekuwa ikizaliwa na kufa kutokana na muundo wake usiokuwa wa kibiashara. TANESCO isiyo na mshindani yeyote, TTCL ambayo awali haikuwa na mshindani, na mengine mengi yaliyokwishakufa na yaliyouzwa, mashirika yote hayo yalikufa kwa sababu yalianzishwa, kuendeshwa na kusimamiwa kiserikali/kisiasa.

Serikali haijawahi kuendesha biashara ikafanikiwa. Tatizo linaanzia kwenye muundo wa haya mashirika/makampuni. Wanasiasa/viongozi wa serikali ambao kimsingi si wafanyabiashara ndiyo waliotengeneza muundo wa uendeshaji na ndiyo wenye kauli ya mwisho. Vigezo vya wajumbe wa bodi na watendaji wakuu wanavyo wao. Na siku hizi PhD imekuwa ni kigezo kikubwa sana ingawa kiuhalisia, kwa Dunia nzima, ni nadra sana kuwaona wenye PhD wakiwa wafanyabiashara wazuri na waliofanikiwa.

Juzi wakati Mh. Rais akizindua ujio wa ndege mpya alisema ATCL imezaliwa upya, ina ndege mpya, bodi mpya na uongozi mpya, sikusikia kama ina muundo mpya wa uendeshaji na usimamizi. Bado inaonekana ATCL itandeshwa kwa mkono wa serikali.

RAIS - 'ATCL ISITUMIE MAWAKALA WA KUKATISHA TIKETI'

Hili tayari ni agizo ambalo naamini ni agizo lisilo sahihi. Tayari serikali imeanza toka hatua za mwanzo kuingilia uendeshaji wa ATCL. Rais anapoagiza ATCL isitumie mawakala wa kukatisha tiketi inamaanisha ATCL iwe na wafanyakazi waajiriwa kila mahali nchini. Gharama za maelekezo hayo itakuwa kama ifuatavyo:
  • ATCL italazimika kuwalipa wakatisha tiketi mishahara, matibabu, posho, michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii, usafiri, n.k. ATCL italazimika kulipia gharama hizo zote bila ya kujali mkatisha tiketi anakatisha tiketi ngapi au kama amepata wateja au hakupata kabisa
  • ATCL italazimika kulipia ofisi na kuweka miundombinu ya ukatishaji ticket nchi nzima. Ifahamike kuwa ukitaka kuwa na ufanisi unalazimika kuwa na ofisi za ukatishaji tiketi hata mahali ambapo ndege haitui, kwaajili ya kuhudumia abiria wanaotoka maeneo hayo wanaotarajia kutumia usafiri wa ATCL kutokea uwanja ulio karibu
  • ATCL italazimika kuwapa mafunzo wakatisha ticket watakaotapakaa nchi nzima
Wakati ATCL watakapokuwa wanahangaika na kuwa na wakatisha ticket wao na ofisi zao, washindani wao wataendelea kuwa na wafanyakazi wachache, wakiwa na mawakala wengi wanaolipwa kutokana na idadi ya ticket na thamani ya ticket walizokatisha. Hawalipii ofisi, hawalipii matibabu, hawalipii michango ya hifadhi ya jamii, hawalipii likizo ya mfanyakazi. Mawakala wao wanalipwa kutokana na wanachozalisha, wasipozalisha hawalipwi chochote.

ATCL wanaanza na quandary ya kwanza, wafuate maagizo ya mwenye mali au kanuni za biashara? Je, hii ni ya mwanzo na ya mwisho au zitaendelea kuja na nyingine? Kwa kuwa tatizo la msingi la uendeshaji biashara zilizo chini ya serikali halijatatuliwa, haitakuwa jambo la ajabu ATCL kufuata projectile ya mashirika/makampuni ya umma.
We are cursed to repeat the same and expect different results.
 
Mkuu Msambichaka, kwenye digital world, inawezekana kabisa kuuza tiketi online bila kuwatumia mawakala. Mawakala wanaozungumzwa hapa sio mawakala traveling agents, bali mawakala commissioned agents wana operate kama ofisi za
ATCL, badala ya kutumia mawakala, wanauza tickets on line. Fast Jet wana ofisi zao kule tuu mdege yao inakotua, na hawana wakala popote na mauzo yote ni online!, ila kwa mujibu wa sheria ya kimataifa ya shirika la kimataifa la wakala wa usafiri wa Anga, IATA, wakala yoyote aliyesajiliwa IATA kupitia mtandao wa Galileo, anaweza jyfanya booking yoyote ya ndege yoyote, hivyo abiria wa Tanzania yote watapata tiketi za ATCL popote kupitia traveling agents wengine, ila kule ATCL inatua, lazima wawe na agents for clearing.

Pasco
Very well said Pasco
 
Ili uweze kukata ticket mahali popote ulipo ni lazima utumie mawakala. Haijalishi unakata ticket kwenye ofisi, simu au kwenye laptop yako, utatumia wakala. Kutaka kila kitu ufanye wewe mwenyewe ndiyo mbinu ya kizamani ya kuendesha biashara.

Hivi unajua hata unapokata ticket yako na kulipia kupitia mitandao kama Airtel, Vodacom na wengineo unatumia wakala? Hii niliyoitoa hapa ni sehemu ya elimu maana usiamini kuwa wanaohitaji elimu ni wale watu wa chini kabisa, kila mtu anahitaji elimu kwenye jambo fulani. Watawala na viongozi wa serikali wanahitaji elimu pia kwenye masuala ya biashara kama ilivyo kwa mfanyabiashara akiingizwa serikalini atahitaji elimu juu ya jinsi serikali inavyofanya kazi. Hakuna anayejua kila kitu, ndiyo maana ukifanya biashara kwa kutaka ufanye kila kitu wewe mwenyewe lazima uangukie pua.

Anayekuonesha mahali penye hitilifu ndiye anayekujenga kuliko anayekushangilia kila mahali. Ndiyo maana hata kwenye management performance assessment wewe uliye boss unatakiwa uwaombe direct reports wako wakueleze your weaknesses na siyo your strengths. Hayo ya Deo RIP ni out of context.
Sio kweli...

Siku hizi watu wanakata ticket online...Fastjet watu wanakata ticket online..Precision hivyohivyo...

Mashirika yote ya ndege ya nje KW, Emirates, Qatar, Etihad n.k wanakata ticket online...

Ukienda JNIA..KIA..Songwe na viwanja vingine unakata ticket bila kutumia Wakala.
 
  • Thanks
Reactions: MC7
Kaka dunia imebadilika unaweza kata ticket ya ndege popote ulipo bila msaada wa mtu yeyote kilichopo nikuchukua nafasi zetu katika jamii kutoa elimu au kuwasaidia kupata elimu waendane na dunia ya sasa kuleta ukinzani katika kila jambo linalokuwa initiated na serikali haliwezi kukufanya ukawa na busara za kuongoza bali kutatua changamoto zilizoko katika jamii yako ndio ngazi itakayokupandisha daraja na kuwa kiongozi. Je unamkumbuka Marehemu Deo Filikunjombe vaa viatu vyake vikikutosha basi hayo mambo mengine hayatakusumbua. Hongera Magufuli kwa kuonyesha tofauti hata sisi tusio wanachama wa ccm tunaona mwanga kupitia wewe.
We mtu umeona mwanga upi? , mwanga upi elezea? Watanzania tumekufa akili kabisa! Huyu mtoa hoja ameongea vitu ambavyo havihitaji elimu kubwa kuviona. Unapinga! Kisa mahaba
 
Kaka mambo yamebadilika sana wewe fanya uchunguzi na uchunguzi huo ukusaidie kutambua nafasi yako katika kutatua changamoto ya uelewa na weledi wa mambo yaendavyo katika karne hii. Unaweza kata ticket ya ndege hata basi bila wakala kokote duniani. Chamsingi sisi tunaoweza una kwa jicho la tatu tuwasaidie ndugu zetu kujitambue tumuunge mkono Rais Magufuli ili twende mbele kwa speed na fahamu kuwa binafsi sipingani na wewe katika suala la kukosoa lakini unapokosoa njoo na altenative solution ya tatizo lililopo. Ahsante

Ili uweze kukata ticket mahali popote ulipo ni lazima utumie mawakala. Haijalishi unakata ticket kwenye ofisi, simu au kwenye laptop yako, utatumia wakala. Kutaka kila kitu ufanye wewe mwenyewe ndiyo mbinu ya kizamani ya kuendesha biashara.

Hivi unajua hata unapokata ticket yako na kulipia kupitia mitandao kama Airtel, Vodacom na wengineo unatumia wakala? Hii niliyoitoa hapa ni sehemu ya elimu maana usiamini kuwa wanaohitaji elimu ni wale watu wa chini kabisa, kila mtu anahitaji elimu kwenye jambo fulani. Watawala na viongozi wa serikali wanahitaji elimu pia kwenye masuala ya biashara kama ilivyo kwa mfanyabiashara akiingizwa serikalini atahitaji elimu juu ya jinsi serikali inavyofanya kazi. Hakuna anayejua kila kitu, ndiyo maana ukifanya biashara kwa kutaka ufanye kila kitu wewe mwenyewe lazima uangukie pua.

Anayekuonesha mahali penye hitilifu ndiye anayekujenga kuliko anayekushangilia kila mahali. Ndiyo maana hata kwenye management performance assessment wewe uliye boss unatakiwa uwaombe direct reports wako wakueleze your weaknesses na siyo your strengths. Hayo ya Deo RIP ni out of context.
 
Mkuu Msambichaka, kwenye digital world, inawezekana kabisa kuuza tiketi online bila kuwatumia mawakala. Mawakala wanaozungumzwa hapa sio mawakala traveling agents, bali mawakala commissioned agents wana operate kama ofisi za
ATCL, badala ya kutumia mawakala, wanauza tickets on line. Fast Jet wana ofisi zao kule tuu mdege yao inakotua, na hawana wakala popote na mauzo yote ni online!, ila kwa mujibu wa sheria ya kimataifa ya shirika la kimataifa la wakala wa usafiri wa Anga, IATA, wakala yoyote aliyesajiliwa IATA kupitia mtandao wa Galileo, anaweza jyfanya booking yoyote ya ndege yoyote, hivyo abiria wa Tanzania yote watapata tiketi za ATCL popote kupitia traveling agents wengine, ila kule ATCL inatua, lazima wawe na agents for clearing.

Pasco
Pasco usibishe, muulize kwanza Msambichaka, agents wa vipi hawatakiwi? commissioned au travel agents!
 
ATCL kama yalivyo mashirika mengine ya umma, kila mara imekuwa ikizaliwa na kufa kutokana na muundo wake usiokuwa wa kibiashara. TANESCO isiyo na mshindani yeyote, TTCL ambayo awali haikuwa na mshindani, na mengine mengi yaliyokwishakufa na yaliyouzwa, mashirika yote hayo yalikufa kwa sababu yalianzishwa, kuendeshwa na kusimamiwa kiserikali/kisiasa.

Serikali haijawahi kuendesha biashara ikafanikiwa. Tatizo linaanzia kwenye muundo wa haya mashirika/makampuni. Wanasiasa/viongozi wa serikali ambao kimsingi si wafanyabiashara ndiyo waliotengeneza muundo wa uendeshaji na ndiyo wenye kauli ya mwisho. Vigezo vya wajumbe wa bodi na watendaji wakuu wanavyo wao. Na siku hizi PhD imekuwa ni kigezo kikubwa sana ingawa kiuhalisia, kwa Dunia nzima, ni nadra sana kuwaona wenye PhD wakiwa wafanyabiashara wazuri na waliofanikiwa.

Juzi wakati Mh. Rais akizindua ujio wa ndege mpya alisema ATCL imezaliwa upya, ina ndege mpya, bodi mpya na uongozi mpya, sikusikia kama ina muundo mpya wa uendeshaji na usimamizi. Bado inaonekana ATCL itandeshwa kwa mkono wa serikali.

RAIS - 'ATCL ISITUMIE MAWAKALA WA KUKATISHA TIKETI'

Hili tayari ni agizo ambalo naamini ni agizo lisilo sahihi. Tayari serikali imeanza toka hatua za mwanzo kuingilia uendeshaji wa ATCL. Rais anapoagiza ATCL isitumie mawakala wa kukatisha tiketi inamaanisha ATCL iwe na wafanyakazi waajiriwa kila mahali nchini. Gharama za maelekezo hayo itakuwa kama ifuatavyo:
  • ATCL italazimika kuwalipa wakatisha tiketi mishahara, matibabu, posho, michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii, usafiri, n.k. ATCL italazimika kulipia gharama hizo zote bila ya kujali mkatisha tiketi anakatisha tiketi ngapi au kama amepata wateja au hakupata kabisa
  • ATCL italazimika kulipia ofisi na kuweka miundombinu ya ukatishaji ticket nchi nzima. Ifahamike kuwa ukitaka kuwa na ufanisi unalazimika kuwa na ofisi za ukatishaji tiketi hata mahali ambapo ndege haitui, kwaajili ya kuhudumia abiria wanaotoka maeneo hayo wanaotarajia kutumia usafiri wa ATCL kutokea uwanja ulio karibu
  • ATCL italazimika kuwapa mafunzo wakatisha ticket watakaotapakaa nchi nzima
Wakati ATCL watakapokuwa wanahangaika na kuwa na wakatisha ticket wao na ofisi zao, washindani wao wataendelea kuwa na wafanyakazi wachache, wakiwa na mawakala wengi wanaolipwa kutokana na idadi ya ticket na thamani ya ticket walizokatisha. Hawalipii ofisi, hawalipii matibabu, hawalipii michango ya hifadhi ya jamii, hawalipii likizo ya mfanyakazi. Mawakala wao wanalipwa kutokana na wanachozalisha, wasipozalisha hawalipwi chochote.

ATCL wanaanza na quandary ya kwanza, wafuate maagizo ya mwenye mali au kanuni za biashara? Je, hii ni ya mwanzo na ya mwisho au zitaendelea kuja na nyingine? Kwa kuwa tatizo la msingi la uendeshaji biashara zilizo chini ya serikali halijatatuliwa, haitakuwa jambo la ajabu ATCL kufuata projectile ya mashirika/makampuni ya umma.

Hii moja ya post zenye hoja zenye mantiki sana. Big up mleta mada.
Hili la kuwatumia mawakala halikwepeki. Napenda kuamini Prof. Mbarawa anao uwezo wa kumpa taarifa sahihi Rais na akabadili mawazo yake.
 
Back
Top Bottom