BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,013
Rais JPM anajitahidi kufufua shirika letu la ndege lakini namna linavyojiendesha ni tatizo. Tusipopiga kelele litakufa tena na juhudi za kulifufua zitakuwa zimehujumiwa.
Muhula wa masomo China umemalizika. Wanafunzi waliohitimu wanarudi makwao. Nchi nyingi zinachukua wanafunzi wake kwa ndege zao or any other chattered flights.
Serikali yetu imeamua kuchukua watu wake kwa ndege yetu ya Dreamliner ambayo imeondoka leo saa kumi jioni (one way, kutoka Guanzhou mpaka JNIA, Dar)
_
Lakini zoezi hili limekuwa na kasoro nyingi. Moja ni gharama kuwa juu karibu mara mbili kulinganisha na mashirika mengine. Lakini wamelazimika kulipa kwa sababu serikali imezuia kurudi kwa ndege nyingine isipokua ATCL kwa kile kinachoitwa Uzalendo.
Pili, mwezi mmoja uliopita wahitimu walitakiwa kutuma nakala za passport zao ili waandaliwe tiketi. Wakatuma na wakawa wanasubiri itinerary ili kupewa tiketi.
Juzi wakapokea ujumbe kutoka Ubalozi wetu China, kwamba ATCL imefanya makosa mengi kwenye tiketi. Wamekosea spelling, Lulu Kicheere ameitwa Lulu Kicheche. Wamekosea jinsia, John kaandikwa Female na Prisca Male. Wamekosea tarehe za kuzaliwa. Kuna waliozaliwa 1890 kabla ya vita vya Majimaji. Wamekosea mpangilio wa majina na makosa mengine mengi.
ATCL walipotakiwa kufanya marekebisho walidai muda uliobaki usingetosha kurekebisha makosa yote. Kama walipewa mwezi mzima wakafanya makosa mengi hivi, wangewezaje kurekebisha kwa siku mbili.
Kwahiyo ubalozi wetu China ikabidi uandae orodha ya majina itakayotumiwa na wasafiri. Jana Ubalozi umesema ticket za ATCL hazitatumika kama kigezo pekee cha kusafiri bali abiria watahakikiwa kupitia orodha ya majina iliyoandaliwa na ubalozi huo.
Jiulize, hivi tupo serious na biashara ya usafiri wa anga? Kama mwezi mzima ATCL wameshindwa kuandaa tiketi, tena kwa safari moja, je safari zikiwa kila siku itakuaje? Tumebaki kusifu idadi ya ndege, kumbe hatuna uwezo hata wa kuandaa tiketi? Leo watu wanapanda ndege kama daladala? Hakuna hata boarding pass, unakaa siti yoyote iliyo wazi kama mabasi ya Bukene Nzega. Aibu gani hii?
Kumbuka Nyerere aliacha shirika likiwa na ndege nyingi sana, lakini likafilisika kwa sababu ya management mbovu. Sasa tunarudi kulekule?
Malisa GJ
Muhula wa masomo China umemalizika. Wanafunzi waliohitimu wanarudi makwao. Nchi nyingi zinachukua wanafunzi wake kwa ndege zao or any other chattered flights.
Serikali yetu imeamua kuchukua watu wake kwa ndege yetu ya Dreamliner ambayo imeondoka leo saa kumi jioni (one way, kutoka Guanzhou mpaka JNIA, Dar)
_
Lakini zoezi hili limekuwa na kasoro nyingi. Moja ni gharama kuwa juu karibu mara mbili kulinganisha na mashirika mengine. Lakini wamelazimika kulipa kwa sababu serikali imezuia kurudi kwa ndege nyingine isipokua ATCL kwa kile kinachoitwa Uzalendo.
Pili, mwezi mmoja uliopita wahitimu walitakiwa kutuma nakala za passport zao ili waandaliwe tiketi. Wakatuma na wakawa wanasubiri itinerary ili kupewa tiketi.
Juzi wakapokea ujumbe kutoka Ubalozi wetu China, kwamba ATCL imefanya makosa mengi kwenye tiketi. Wamekosea spelling, Lulu Kicheere ameitwa Lulu Kicheche. Wamekosea jinsia, John kaandikwa Female na Prisca Male. Wamekosea tarehe za kuzaliwa. Kuna waliozaliwa 1890 kabla ya vita vya Majimaji. Wamekosea mpangilio wa majina na makosa mengine mengi.
ATCL walipotakiwa kufanya marekebisho walidai muda uliobaki usingetosha kurekebisha makosa yote. Kama walipewa mwezi mzima wakafanya makosa mengi hivi, wangewezaje kurekebisha kwa siku mbili.
Kwahiyo ubalozi wetu China ikabidi uandae orodha ya majina itakayotumiwa na wasafiri. Jana Ubalozi umesema ticket za ATCL hazitatumika kama kigezo pekee cha kusafiri bali abiria watahakikiwa kupitia orodha ya majina iliyoandaliwa na ubalozi huo.
Jiulize, hivi tupo serious na biashara ya usafiri wa anga? Kama mwezi mzima ATCL wameshindwa kuandaa tiketi, tena kwa safari moja, je safari zikiwa kila siku itakuaje? Tumebaki kusifu idadi ya ndege, kumbe hatuna uwezo hata wa kuandaa tiketi? Leo watu wanapanda ndege kama daladala? Hakuna hata boarding pass, unakaa siti yoyote iliyo wazi kama mabasi ya Bukene Nzega. Aibu gani hii?
Kumbuka Nyerere aliacha shirika likiwa na ndege nyingi sana, lakini likafilisika kwa sababu ya management mbovu. Sasa tunarudi kulekule?
Malisa GJ