Mimi ni Daktari wa hospitali moja kubwa binafsi hapa Dar es salaam mzaliwa wa kanda ya ziwa na huu ni mwaka wangu wa pili kazini. Nilikua na rafiki yangu sana ambae sasa ni marehemu. Huyu rafiki yangu tulipendana sana kwa vile tulikua majirani na hata wazazi wetu walikua marafiki pia. Tulisoma wote shule ya msingi hadi A level mkoani Mtwara.
Baada ya kumaliza kidato cha sita sote tulifaulu vizuri na kubahatika kujiunga na masomo ya elimu ya juu hapa hapa Dar kusomea udaktari. Tukiwa mwaka wa kwanza rafiki yangu alibadilika sana na alinishtua sana aliponiambia kua ameamua kuhairisha masomo amepata kazi kwenye kampuni ya kuuza magari. Nilimshauri na kumsihi aendelee na masomo lakini hakubadilisha uamuzi wake.
Alianza kusafiri sana nje ya nchi, mara Afrika kusini, India, China, Brazil, Marekani n.k. Nilienda kuishi nae kwake baada ya kupanga nyumba nzima. Alinipeleka chuo kwa gari lake na kunirejesha kila alipopata nafasi. Niliishi maisha mazuri kiasi ingawa ilikua siri nyumbani hawakujua kama rafiki yangu alisitisha masomo. Skuwahi kupajua anapofanya kazi, kila nilipomwambia anipeleke hakukubali.
Sku moja usiku wa manane nikiwa mezani najisomea na yeye akiwa chumbani kwake alipigiwa sim na mtu ambae walijibizana sana huku kaka akisistiza kua amechoka kusafirisha dawa za kulevya anaacha. Niliogopa sana, niliondoka taratibu na kwenda kulala chumbani kwangu ili asigundue kua namsikiliza. Skupata usingizi kabisa. Asbuhi alionekana mwenye mawazo na hasira nyingi tofauti na siku zote. Nilimuuliza kulikoni akanambia ana mgogoro na bosi wake, nilmuuliza kwani huyo bosi anaishi hapa nchini akasema ndio na kunionesha picha yake kwenye sim.
Kama kawaida alinipeleka hadi chuo, aliponishusha na kuondoka nikachkua taksi na kuanza kulifuata gari lake kwa nyuma, Nilidhamiria kupajua anapofanyia hizo kazi zake. Sku hiyo ndio siku niliposhuhudia rafki yangu akipigwa risasi na mtu aliyekua amepakizwa kwenye pikipiki (Ni yule nilooneshwa na rafki yangu kwenye picha), na kufariki hapohapo. Baada ya kifo cha rafiki yangu yalitokea mambo mengi sana ikiwa ni pamoja na mimi kuachishwa masomo kutokana na kua sehemu ya washukiwa, kuparaganyika kwa familia zetu n.k.
Usiku wa kuamkia leo hapa hospitalin ameletwa mtu yuleyule aliyemuua rafiki yangu na kusababisha misukosuko mingi katika maisha yangu akiwa hoi kwa presha ya kupnda. Sijawahi kufikiria kuua katika maisha yangu ila kwa sasa dhamira inanituma nimchome sindano ya sumu, nimtundike dripu ya glucose, nimuoverdose au ninyonge kabisa.