Assault on Dr. Ulimboka: Who Did It?

Kuna mambo kadhaa ambayo yanakinyoshea kidole serikali kuhusika na utekaji wa Ulimboka. Maoni yangu hapa yanatokana na kitu tunachoita "profiling" ya mazingira ya incident ili ku-identify nani kahusika;

1. Utumiaji wa assault riffles - hizi bunduki za kivita zinapatikana kirahisi katika vyombo vya usalama vya serikali tu. Si rahisi watu binafsi wafanye mpango wa kumteka Ulimboka na watumie assault riffles. Kwanza hili nalo linaondoa kabisa dhana kwamba waliomteka ni ndugu wa walioathirika na mgomo wa madaktari.

2. Maswali aliyoulizwa "nani wako nyuma ya mgomo huu". Hili bila shaka ni swali kutoka ma-agent wa serikali ya CCM tu. Haiwezekani kikundi binafsi kikamteka na kuuliza swali kama hili. Kikundi binafsi kingekuwa kinatoa lawama kwa kusababisha vifo vya ndugu zao, sio kuuliza "nani yuko nyuma ya mgomo wenu". Kikundi binafsi kingekuwa kinamwagia Ulimboka shutuma za hasira, kama vile "ngoja na wewe tukukomeshe uone uchungu wa kuumwa", sio kuuliza maswali.

3. Kujiamini katika kumteka. Ulimboka ametekwa katika mazingira ya watu wenye kujiamini sana. Hawa ni professionals ambao inaonyesha wazi wamepitia mafunzo ya kikachero. Na pia "choreography" iliyofanyika hadi kumteka ni dhahiri watu wenye mafunzo ya ki-intelligence walihusika, na kwamba kulikuwa na "synchronised and orchestrated plan".

4. Kujiamini kuendesha gari isiyo na namba. Ina maana hawa watu walijua kwamba hata wangesimamishwa njiani na polisi walikuwa na uhakika wa kujieleza pamoja na vitambulisho. Mtu ambaye hahusiki na vyombo vy taifa vya usalama angetumia namba "feki" sio kuondoa namba za gari kabisa. Na watekaji binafsi wasingetaka kuendesha gari lisilo na namba muda mrefu hadi kule msituni. Na vyombo vya usalama vinapendelea magari meusi kwa operation za usiku.

5. Uteseji wa Ulimboka ambao ni wa ki-professional. Ulimboka alikuwa akiteswa kwa namna ambayo ingefanya aumie muda mrefu bila kufa. Mtu anayekupiga kwa kitako cha bunduki na anajua wapi akupige uli usife mapema kabla hajapata taarifa anayotaka, huyo ni mtu aliyefundishwa namna ya kutesa ili kupata habari - na huyo sana sana ni ofisa wa usalama wa taifa, wala sio polisi. Hata polisi hawana utaalamu huu, mara nyingi wakitesa mtu kwa ajili ya kupata habari wanaishia kuua, kwa sababu hawajui utaalamu wa kutesa bila kuua.

6. Utumiaji wa "safe house". Ulimboka alipelekwa kwenye "safe house" fulani kabla hajapelekwa msituni. Matumizi ya "safe house" ni ya vyombo vya usalama wa taifa, na ni kweli kwamba ni standard procedure kumfunika mtu uso wakati wanampeleka "safe house". Kwa mtekaji mwingine yeyote, si rahisi wateke mtu halafu kwanza wampeke "nyumbani", nyumba ambayo ni ya makazi binafsi. Uwezekano mkubwa ni kwamba walitaka ku-"minimize" muda wa kuwa na Ulimboka kule msituni na ilibidi watumie "safe house" ili kupata habari. Na pia ningependa kujua extent ya mateso aliyopata Ulimboka kabla ya kufikishwa "safehouse". Hilo litakuambia uamuzi wa kumuua ulifanyika wakati gani.

Kwa hiyo bwana, hata iweje, au muulize mtu yeyote aliyebobea mambo ya intelligence, atakuambia hii incident ya Ulimboka ina footprint kubwa sana ya chombo rasmi cha usalama cha serikali. In fact, kiongozi yeyote wa usalama aliyeidhinisha hili hakutumia busara, kwani suala zima limeacha footprint kwamba watu wa usalama wamehusika, na liko wazi kwa mtu yeyote yule anayejua mambo ya intelligence na counter intelligence.

Ni wazi kabisa kilichomwokoa Ulimboka ni watekaji kudhani alikuwa amekufa. Na hata ungeniambiaje hapa, uwezekano kwamba utekaji ulifanywa na watu professionals walioko serikalini ni zaidi ya asilimia 95%.

Labda JK anachohitaji kusema ni kwamba Ikulu haikuhusika, kwamba watu wa Usalama wa Taifa walifanya hivi on their own initiative.

Na pia, uwezekano kwamba hili lilifanywa na Usalama wa Taifa ni asilimia 90%, na kwamba lilifanywa na Polisi ni asilimia 60%. Uwezekano kwamba Polisi walishirikiana na Usalama wa Taifa ni asilimia 99%.

In fact, inaonekana hata Polisi Bunju waliona kila dalili ya kwamba chombo cha serikali kilihusika na huu utekaji, na kosa lilifanyika kumwacha hai wakidhani amekufa. Ninahisi kwamba kumwacha Ulimboka muda mrefu pale kituoni bila matibabu ilikuwa ni kujaribu kuona kama angekufa kabla hajapata msaada.
 
Post moja Rep-nill others nill kweli hii System CCM NAPE at work, pole umeisha fahamika, kama umelipwa kanywe supu ukalale!!!
 
Mzee! Unasema siku 5 zimepita bila action!? Kule Zanzibar wahuni walichoma makanisa zaidi ya wiki mbili sasa, serikali yetu sikivu haijaweza kuwashika hao wahuni! Waliomvamia Ulimboka naona nao ni wahuni! Serikali yetu haina uwezo wa kuwakamata/kuwashika WAHUNI!

Wana uwezo mkubwa wa kuwakamata wnaharakati!
 
Mkuu Gaijin,
"possibility" yako ya kwanza ingewezekana tu kama ingetumia "possibility b" - Hired Professional Assassins - au "possibility d" za MMM. Bado maswali yanabaki palepale. Ile 40% ya TISS haiwezi kung'amua mpaka sasa?

Sio ku"hire" professionals. Ni government agents working for the opposition parties. Watu wanapewa maagizo ya kufanya uhalifu kwa raia, bila ya kujua amri hizo zinatoka wapi.


Kama kweli 60 ni kubwa kuliko 40 wanashindwa nini kumuondoa JK madarakani kwa namna nyingi tu rahisi zaidi ya kuwatumia madaktari na hata "kuwaua" kikatili namna ya Dr. Ulimboka?

Kama ni chama kinachojinasibu na Demokrasia basi ni muhimu kwake kuingia madarakani kwa demokrasia. Kwa hiyo inachoweza kufanya ni kuchochea serikali ikataliwe ili ichaguliwe kwa kishindo kwa demokrasia

*btw, hata upinzani ukishika madaraka, TISS watakuwepo, na professional assassins watakuwepo. Labda wafanye kazi zao kwa siri zaidi tu



"Possibility" yako ya pili ndio hiyohiyo ya "possibility d" ya MMM. Au?

Hapana ni tofauti
 
1. hakuna mtu atakayekamatwa aliyetenda unyama huu zaid sana unaandaliwa uongo wa kuwaaminisha watanzania

2. viongozi wa juu wa serikali hawawezi kukwepa lawama juu ya maagizo waliyotoa juu ya kumshughulika dr ulimboka

3.kuna vikundi vingi vitajitokeza juu ya kulaani mgomo na kuwalaani madaktari kuwa wanaua raia waio na hatia na kuwamba wasitishe mgomo.

4. kwa sasa kinachoendelea ni uchonganishi kati ya madaktari na wananchi..na mchonganishi ni serikali.

5. mtaweka hisia zote juu ya nani yuko nyuma ya unyama huu lakini ukweli unajulikana aliye nyuma ya unyama huu ni serikali. baadae mtaelewa kwa nini nasema hivyo.ngoja kwanza tuone huo uchunguzi wanaofanya na kuwatafuta wahusika kama kweli wanafanya uchunguzi na kuwatafuta wahusika.



safari hii mpango ume back fire.
 
Watarudi na ID zingine bwana lazima wajichanganye, lakini taarifa wamepata!!!!
 

As if we don't have bigger roles and issues to deal with for our Beloved country...excessive force inayotumika kwenye petty issues is a sign that we dont take serious issues seriously.We have reduced ourselves well below our capacity and standards over time.
 
Mtoto wa jirani akinya kwenye uwanja wako si lazima utasema jirani watoto wake wamechafua uwanja wako??? Kwa hiyo kama ni serikali basi hakuna kubana maneno kwa sababu hata mhusika Dr alimyooshea kidole kuwa amechukua pochi na simu yake huyo polisi au agent wa serkali!!! Hapo upo au unazidi kutetea uozo, ikitokea akawa ndugu yako utasema je???

 
Wangeweza tu kupakua mazungumzo ya simu ya Dr Ulimboka na yule mtu wa ikulu kisha huyo mtu wa ikulu na waliokuja kumtesa. TCRA wanaweza kutoa hayo mawasiliano na wahusika wakakamatwa. Sioni namna nyingine rahisi ya kuwapata wahusika
 

Any divided kingdom shall never stand!
 
Well said mkuu..lakini kuna uwezekano pia walishindwa kukubaliana kufikia uamuzi wa kumuua ndio wakaamua kumtelekeza msituni. Sababu hata ndani ya system sio wote wanaoshabikia unyama huu.
Manake kama walidhamiria kuua kwa dhati nina wasiwasi hata kama maiti yake ingeonekana
 
kuna watu weng tu wanauwawa na watu hawakamatwi na wala raia hampgi kelele, maalbino wangapi wanauwawa kila kukcha? Iweje la dr ulimboka ndyo lipewe kipaumbele peke yake?
 
Bila kujali, aliyemtendea UNYAMA ulimboka. Serekali haikufaidi Unyama huo??

Unyama huo umeenda bega kwa bega na mgomo uliokuwa unaendelea. Unyama huo kwa namna moja au nyingine kwa kuwa umetuma ujumbe wa KIFO kwa wahusika unaonekana kuwa sehemu muhimu sana ya utatuzi wa tatizo la mgomo huo. Ikimaanisha woga wa Mateso ya kinyama na pengine kifo, Baadhi ya wahusika wanaweza kuogopa na kuchagua kukomesha mgomo. Au Wengine waliokuwa wana nia kama hiyo kusitisha zoezi hilo.

Ikiwa ni hivyo, Bila kujali kuwa serekali ilihusika au haikuhusika ukweli ni kuwa IMEFAIDI kwa kiwango kikubwa Unyama huo. Kuwa sasa KIFO na MATESO kabla ya KIFO ni CHOMBO cha Kutatulia Matatizo ya Jamii ya Mtanzania ni Hodi imebisha ... Na Mla Nyama ya Watu katu ... There is no end to it!! Hadi taifa kufikia Kuwa kama Syria.

TAFAKARI.

1. Serekali inaweza kudhibitisha kuwa katika kutatua tatizo la MGOMO unaondelea sasa, haikufaidi Unyama na Udhalimu ulio kinyume na UTU wa Bindamu aliofanyiwa Dr Ulimboka kama sehemu muhimu ya Utatuzi????

2 . Serekali inawadhibitishiaje Wanachi wake kuwa Mtindo wa Kungolewa Meno na Kucha hautakuwa adopted kama njia ya siku zijazo za kutatulia maswala magumu ya Taifa baada ya serekali kupoteza uwezo huo kwa njia ya UTU na Mantiki ya kibinaadamu?

3. Serekali ya Tanzania Bado inaamini kwenye Misingi ya kuongoza na kutatua Matatizo yake Kwa Misingi ya KI UTU na Si KINYAMA!!?
 
The first suspect angekuwa jamaa aliyetajwa na victim, sasa watu wenyewe wanaochunguza kesi inaonekana wanatafuta watu wanaowajua wao.Dhaifu tu na wao
 

Mtu akisema SIHUSIKI sio necessarilly kuwa HAHUSIKI. Vinginevyo asingekuwepo mtu hata mmoja jela.
 
Any divided kingdom shall never stand!
There's not such a thing as divided in the Dr. Ulimboka saga. If you find someone supporting the government look at their Usernames, propagandist type of names. The likes of WAKUZIBA, UKUBWA JIWE, MAMA POROJO. Those names should tell you something. They think we are stupid
 
Mtu akisema SIHUSIKI sio necessarilly kuwa HAHUSIKI. Vinginevyo asingekuwepo mtu hata mmoja jela.

Lakini sio mtu aseme "sihusiki" kisha sisi tuseme amesema anahusika.

Anaweza sana kuwa anahusika lakini hajasema kuwa anahusika

Ahsante
 

Reformer, uwezekano huo upo, lakini ni mdogo sana. Kumbuka kwamba Ulimboka wakati huo kimtazamo (physical appearance) alikuwa katika hali mbaya sana, na alikuwa amefungwa kamba miguu na mikono. Ikiwa kulikuwa na mwenye huruma asingeruhusu afikie katika hali ile, au kuachwa ndani ya msitu akiwa amefungwa kamba. Hali aliyoachwa nayo ilikuwa ya kifo, au ameshakufa, au atakufa wakati wowote na mwacheni hata mbwa au sisimizi au siafu wanaweza kummalizia.

Kama kulikuwa na mwenye huruma kati ya wale watesaji basi ambacho Ulimboka hajasema ni kwamba hakujikongoja kurudi barabarani yeye mwenyewe, bali mmojawapo wa watesaji alirudi kule msituni, akamfungua kamba na kumwamishia barabarani. Na kama mtu huyo yupo atakuwa aliwaambia wenzake Ulimboka ameshakufa tumwacheni. Na huenda walipotaka kummalizia kwa risasi akasema haina haja, watu wanaweza kusikia mlio wa risasi (kwa kusema hivi najua nahatarisha uhai wa huyo jamaa mwenye huruma, hivyo ni bora tu ajitokeze aweke kila kitu wazi!).
 

Well, it is also possible he survived by feigning death and got them fooled to believe that they accomplished their mission.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…