Askofu Tendwa aonya wanaolalamikia utawala wa Magufuli

Majs

JF-Expert Member
Dec 21, 2012
229
485
Askofu Msaidizi wa Kanisa Anglikana Dayosisi ya Katanga katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Elisha Tendwa amesema baadhi ya Watanzania ambao wamekuwa wakitoa malalamiko juu ya utawala wa Rais John Magufuli siku moja wangefika Congo wasingethubutu kutoa lawama hizo.

"Mimi nafanya kazi ya umishenari kule DRC, nimetumwa na Kanisa Anglikana Tanzania, ni mojawapo ya njia ya kueneza amani duniani, nina miaka mitano tangu niende huko na nimetembelea majimbo mengi nimejionea nchi ile ni tajiri na yenye rasilimali nyingi lakini watu wake wanaishi kwa hofu ya vita ni wakimbizi ndani ya nchi yao, huwezi kulinganisha na nchi kama Tanzania," amesema.

Amesema kuwa ni vema kabla ya watu kutoa lawama kwa Serikali juu ya mambo mbalimbali ni vema wakalinganisha na kufanya tathmini juu ya hali ilivyo kwa nchi nyingine ikiwemo nchi ya DRC.

"Kwanza naishukuru Serikali ya Tanzania ambayo imekuwa ikitoa mchango wake kwa hatua mbalimbali ili kurudisha amani kule Kongo na naamini ipo siku amani ya kudumu itarejea kule Congo," amesema.

Amesema kuwa hali ya maisha ya Tanzania ukilinganisha na DRC ni tofauti kwa maeneo mengi ikiwemo amani na hali ya shughuli za kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja.

Naye Ofisa Habari na Mawasiliano wa Kanisa Anglikana Dayosisi ya Dar es Salaam, Yohana Sanga alisema kutokana na mchakato wa uchaguzi wa kumpata Askofu wa Dayosisi ya Dar es Salaam unaoendelea, ni vema waumini wa kanisa hilo wakaacha kujiingiza kwenye makundi yenye nia mbaya.
 
Congo Siyo Sawa Na Tanzania
Na Matatizo Yao Yanajulikana
Baadhi Hawataki Democracy
Wanataka Watawale Wao
 
Huyu Askofu, anataka kusema nini hasa?

Tunatakiwa kujilinganisha na waliofanikiwa siyo na walioshindwa. Tujilinganishe na Botswana. Congo wapo katika vita, sisi tupo katika vita na nani? Rwanda walikuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe. Kenya walikuwa na vita uchaguzi uliopita. Uganda wamekuwa wakiongozwa na madikteta miongo mingi. Mozambique na Angola wamekuwa katika vita kwa miaka mingi.

Katika demokrasia tulipiga hatua kiasi, tulitakiwa kupiga hatua kwenda mbele siyo kurudi nyuma kama ilivyo sasa. Katika uwekezaji tulipiga hatua mpaka kufikia 26.8% lakini sasa tumeanguka mpaka 3.4%. Katika nidhamu ya utumishi serikalini, tulikuwa chini sana, safarini nadhani tumepanda kwa kiasi fulani, hata kama ni kwa woga.

Ukiangalia kwa ujumla, katika utawala huu, tumefanikiwa kupiga hatua katika jambo moja lakini tumerudi nyuma karibia kwa mambo yote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii sera ya ndiyo silaha ya mwisho ya CCM kuwapata wamama na wazee waipigie kura.
"CCM imepigania uhuru,CCM imetunza amani tangu uhuru mpaka leo ,mkichagua chama pinzani ni sawa na kuchezea amani yetu"
Sera hii kwa bahati mbaya hutolewa mbele ya non-educated persons na hawaitolei maelezo.
Very rubbish. Sasa tumekuwa tunataka maendeleo na demokrasia ya kweli na si sera za amani. Amani Italy kaileta Nyerere au Magufuli?
 
Kimsingi huyu anaeitwa Askofu alipaswa anyooshe kidole kwa pande zote hasa Wanasiasa ambao ndio mara nyingi hutanguliza maslahi yao mbele kuliko Utaifa.

Awaambie wa chama tawala waache kukandamiza wenzao,kuwe na uwanja sawa kufanya kazi zao za kisiasa

Serikali iache kuingilia mihimili mingine.

Kama wakiendeleza ubabe wao ndio watakaotupeleka pabaya, wananchi hatuna matatizo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Askofu Msaidizi wa Kanisa Anglikana Dayosisi ya Katanga katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Elisha Tendwa amesema baadhi ya Watanzania ambao wamekuwa wakitoa malalamiko juu ya utawala wa Rais John Magufuli siku moja wangefika Congo wasingethubutu kutoa lawama hizo.

"Mimi nafanya kazi ya umishenari kule DRC, nimetumwa na Kanisa Anglikana Tanzania, ni mojawapo ya njia ya kueneza amani duniani, nina miaka mitano tangu niende huko na nimetembelea majimbo mengi nimejionea nchi ile ni tajiri na yenye rasilimali nyingi lakini watu wake wanaishi kwa hofu ya vita ni wakimbizi ndani ya nchi yao, huwezi kulinganisha na nchi kama Tanzania," amesema.

Amesema kuwa ni vema kabla ya watu kutoa lawama kwa Serikali juu ya mambo mbalimbali ni vema wakalinganisha na kufanya tathmini juu ya hali ilivyo kwa nchi nyingine ikiwemo nchi ya DRC.

"Kwanza naishukuru Serikali ya Tanzania ambayo imekuwa ikitoa mchango wake kwa hatua mbalimbali ili kurudisha amani kule Kongo na naamini ipo siku amani ya kudumu itarejea kule Congo," amesema.

Amesema kuwa hali ya maisha ya Tanzania ukilinganisha na DRC ni tofauti kwa maeneo mengi ikiwemo amani na hali ya shughuli za kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja.

Naye Ofisa Habari na Mawasiliano wa Kanisa Anglikana Dayosisi ya Dar es Salaam, Yohana Sanga alisema kutokana na mchakato wa uchaguzi wa kumpata Askofu wa Dayosisi ya Dar es Salaam unaoendelea, ni vema waumini wa kanisa hilo wakaacha kujiingiza kwenye makundi yenye nia mbaya.

tatizo uyu askofu anazani amani ile kaileta uyu jamaa wasasa ivi nataka ni mwambie askofu JPM anachafua nchi kwa matendo yake ndio maana watu wanapiga kelele, amani iliyokuwepo inapotea kidogo kidogo kwa sababu yake ndio maana watu wanapaza sauti anakoelekea sio pazuri, Mfano Mkonda anacheti fake na anavamia ofisi za watu na bunduki lakini anamkingia kifua, mbunge wa chato ni mhusika mkuu wa issue za madini ila kamkaushia, JPM kila siku anaenda kinyume na katiba ya nchi watu wanapiga makofi ,aisee wa askofu fanya utafiti vizuri amani yetu JPM ndio tishio hakuna mwingine
 
Hawa hawajui chochote kuhusu maisha no kuwapuuza tu
mimi ninamawazo tofauti na wewe.Hata kama unaona alikosea katika hili haiwezi kukupa conclusive statement ya kwamba maaskofu hawajui kitu katika maisha.
Angemsifia yule mzee nadhani usingesema hivi.
 
Back
Top Bottom