Askofu: Rais Kikwete usivunjike moyo

Askofu: Rais Kikwete usivunjike moyo

MwanaDiwani

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2013
Posts
5,536
Reaction score
2,268
GO9G4189.JPG

Raia Kikwete akiwa na Askofu wa kanisa katoliki jimbo la Mbinga, Mhashamu John Ndimbo.
---------------------------------------------------------------------------------------

VIONGOZI wa dini wameendelea kumpa moyo Rais Jakaya Kikwete, wakati huu wa mchakato wa kupata Katiba mpya.

Juzi, Askofu wa Kanisa Katoliki, Jimbo la Mbinga, Mhashamu John Ndimbo, alimtaka kuendelea kuwa na moyo wa uvumilivu kwa watu wanaomkashifu.

Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake kuhusu msimamo wa baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wa kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kususia bunge hilo, Askofu Ndimbo alisema msimamo huo, unawanyima wananchi haki yao ya msingi.

"Kwanza nampa sana pole Mheshimiwa Rais wetu, Jakaya Kikwete, kutokana na tuhuma nyingi zinazoelekezwa kwake. Mimi ninachomuomba, aendelee kuwa na moyo wa uvumilivu kwa watu hao kwani mti wenye maembe, ndiyo unaopigwa mawe kila siku. Hizo ni chuki binafsi ambazo naamini haziwezi kumkatisha tamaa," alisema Askofu Ndimbo.

Askofu Ndimbo alisema kitendo cha wajumbe hao wa Ukawa, kukataa kuendelea na mchakato huo, ni dhambi kwa kuwa wanachofanya sicho walichotumwa na wananchi.

Askofu alisema kuendelea na msimamo huo, ni kunyima wananchi waliowatuma haki yao ya msingi. Aliwataka walegeze msimamo huo na kuhudhuria vikao hivyo, kwa kuwa msimamo huo, umeanza kukosa mantiki baada ya baadhi ya wajumbe kutoka umoja huo, kuanza kuhudhuria vikao hivyo vya Bunge Maalumu la Katiba.

Askofu Ndimbo amesema wajumbe hao, walitakiwa kuzungumza hoja zao ndani ya Bunge na ingewasaidia kueleweka kwa wananchi na kama hawataki, ni bora waachie ngazi ili wapatikane watu watakaokuwa tayari kushirikiana na wajumbe waliopo, kuandaa Katiba bora, itakayomaliza kero zilizopo.

Alisema kutokuwepo kwa wajumbe hao katika Bunge Maalumu la Katiba, kutachelewesha kupata Katiba mpya na hata ikipatikana, haitakuwa bora, kwa kuwa itakuwa imeundwa na wajumbe wachache.

Kiongozi huyo wa dini alionya kuwa Bunge Maalumu la Katiba, halipaswi kuwa chombo cha kutafuta umaarufu wala sehemu ya chama kufanya kampeni, bali sehemu ya kutimiza majukumu waliotumwa na wananchi, kwa kupanga mipango itakayowapunguzia mzigo wa umasikini na kupunguza pengo kati ya walionacho na wasionacho.

Alitaka vyama vya siasa, kutafuta maeneo mengine ya kufanyia mambo yao na wasitarajie kuungwa mkono na wananchi, kutokana na tabia zao za matusi na dharau wakiwa bungeni, kwani vitendo hivyo ni kinyume na madili na viapo vyao.

Alisema kumlaumu Rais kwa kila jambo ni kumuonea na lazima Watanzania waelewe kuwa matatizo yaliyopo, hayawezi kumalizwa kwa siku moja au na mtu mmoja, bali kwa kushirikiana kwa pamoja na kuvumiliana na hata kunapotakiwa kukosoana, basi watumie busara zaidi na siyo kutumia jazba na matusi kwa viongozi.

Aliwaonya Watanzania kuwa watulivu na kuacha kujiingiza katika mambo yatakayochelewesha maendeleo, kwani muda wanaotumia kufanya hivyo, ni vyema wautumie katika maendeleo ili kuongeza tija na kipato kwenye familia zao.

Pia, aliwataka Watanzania wasiruhusu wanasiasa kuwatumia kama ngazi ya kutaka kufanikisha mambo yao.

"Tusikubali kuwa ngazi ya wanasiasa, tutumie muda wetu kufanya kazi za maendeleo kwani bado tunakabiliwa na changamoto za kila aina katika Taifa letu," alisema.

Kauli hiyo ya Askofu Ndimbo, ni sehemu tu ya mfululizo wa kauli za viongozi wengi wa dini, kumpa moyo Rais Kikwete katika kusimamia mchakato huo, na kuwataka Ukawa kurudi bungeni. Pengine na ushauri huu wa mtu wa Mungu, nao ni vyema kuupa nafasi na kuutafakari.

Chanzo: Habarileo
 
haya askofu mwingine kasema, watu watakuja sema nae kalipwa.
 
...jamani si TEC wameshatoa msimamo?,sasa huyu anatoka wapi?.Kanisa katoliki inapoteza mwelekeo kabisa!.Ikiwa ni kweli Bishop huyu kasema hayo basi kanisa catholic inakosa uwajibikaji wa pamoja.Kanisa inatakiwa kuwa mpatanishi full stop.wamepotoka wengi sana kwa sb ya maslahi binafsi but Tanganyika itashinda.
 
haya askofu mwingine kasema, watu watakuja sema nae kalipwa.
Ndugu, usihangaike na watu tunaowaita ''debe tupu'' ambalo kelele ndiyo jadi yake.

Waache waendelee kusema lakini ukweli unaendelea kusimama kila siku.

Rais Kikwete amenukuliwa akisema, “Hatuwezi sisi kujiingiza katika shughuli ya kupoteza muda kwa kushiriki upuuzi na ujinga. Haya ni maneno ya kipuuzi yanayosemwa na watu ambao kazi yao usiku na mchana ni kuota jinsi ya kuyumbisha ajenda yetu ambayo imefanikiwa sana katika kubadilisha hali ya maisha ya Watanzania.’
 
kasema askofu, wapambe wa CDM wapo kimyaaaaaaaa hawathubutu hata kumkosoa.

Angesema mtu mwingine thread ingekuwa page ya 3 mdahuu.
 
Ndugu, usihangaike na watu tunaowaita ''debe tupu'' ambalo kelele ndiyo jadi yake.

Waache waendelee kusema lakini ukweli unaendelea kusimama kila siku.

Rais Kikwete amenukuliwa akisema, “Hatuwezi sisi kujiingiza katika shughuli ya kupoteza muda kwa kushiriki upuuzi na ujinga. Haya ni maneno ya kipuuzi yanayosemwa na watu ambao kazi yao usiku na mchana ni kuota jinsi ya kuyumbisha ajenda yetu ambayo imefanikiwa sana katika kubadilisha hali ya maisha ya Watanzania.’

Maisha ya watanzania yamebadilika!aseme maisha yake ndiyo yamebadilika kutokana na ubinafsi,upuuzi alianzisha mwenyewe kwa kutoa maoni wakati muda Wa kutoa maoni ulishaisha,akaweka msimamo kuwa,serikali Tartu mpaka yeye aondoke madarakani,ila kuna kitu anahofia,nafikiri kuna watu nyuma yake wana mdrive
 
kasema askofu, wapambe wa CDM wapo kimyaaaaaaaa hawathubutu hata kumkosoa.

askofu muoga ameacha kondoo wake waangamie na anadiriki kumpa moyo muangamizaji wa kondoo wake.
Ni aibu sana kumuona askofu anadiriki kuvaa sura ya unafiki huu ila round hii mtaumbuka.
 
Ndugu, usihangaike na watu tunaowaita ''debe tupu'' ambalo kelele ndiyo jadi yake.

Waache waendelee kusema lakini ukweli unaendelea kusimama kila siku.

Rais Kikwete amenukuliwa akisema, “Hatuwezi sisi kujiingiza katika shughuli ya kupoteza muda kwa kushiriki upuuzi na ujinga. Haya ni maneno ya kipuuzi yanayosemwa na watu ambao kazi yao usiku na mchana ni kuota jinsi ya kuyumbisha ajenda yetu ambayo imefanikiwa sana katika kubadilisha hali ya maisha ya Watanzania.’

Mkuu Haya uliyonukuu ni majibu aliyotoa kuhusiana na Mwanaye kuhusishwa na madawa ya kulevya......majibu haya hupaswi kuyageneralize mpaka kwenye ishu hii nyeti ya katiba.......
 
kasema askofu, wapambe wa CDM wapo kimyaaaaaaaa hawathubutu hata kumkosoa.

Angesema mtu mwingine thread ingekuwa page ya 3 mdahuu.

Teh teh teh teh.

Mkuu hapo umepiga pentagon.

Yaani hiki chama cha wakopeshanaji ni tabu mno.
 
GO9G4189.JPG

Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mhashamu John Ndimbo, Askofu wa Kanisa Katoliki, Jimbo la Mbinga.
=============================================================================

KIKWETE - VIONGOZI WA DINI WANAFANYA BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA
Picha hii inanifikisha mbali kwani ni siku Askofu Ndimbo wa Jimbo Katoliki Mbinga mkoani Ruvuma aliposimikwa ibada iliyohudhuriwa na maaskofu karibu wote kutoka majimbo mbalimbali ya Tanzania baada ya Askofu mtangulizi wake Emmanuel Mapunda kustaafu. Ibada hii ilihudhuriwa pia na Rais Kikwete.

Katika tukio hili ni pale Rais Kikwete alipopata wakati mgumu kutokana na kauli yake mbele ya Maakofu kuwa ni viongozi wa dini wanafanya biashara ya madawa yakulevya huku Maakofu Katoliki Tanzania, maaskofu toka madhehebu mengine na viongozi mbalimbali waalikwa waliohudhuria sherehe hiyo. Wengi hatujasahau tukio hilo.

CC,
MwanaDiwani
 
8D6U8671.JPG


Kikwete na Maarais wastaafu walivyojitahidi kumkumbatia Pengo katika nafasi yake ya anniversary ya uaskofu miaka 25 Dar na ndio maana amekuwa kimbilio la Kikwete kutoa matamkoa yanayoendana kinyume na msimamo wa pamoja wa kanisa katoliki, ndicho anachofanya askofu Ndimbo.
 
...jamani si TEC wameshatoa msimamo?,sasa huyu anatoka wapi?.Kanisa katoliki inapoteza mwelekeo kabisa!.Ikiwa ni kweli Bishop huyu kasema hayo basi kanisa catholic inakosa uwajibikaji wa pamoja.Kanisa inatakiwa kuwa mpatanishi full stop.wamepotoka wengi sana kwa sb ya maslahi binafsi but Tanganyika itashinda.
Pamoja na tamko, viongozi mmoja mmoja kwa wakati wake wanasisitiza msimamo wa kumuunga mkono JK, sidhani kama kuna tatizo, atakemewa yule tu atakayekwenda na kinyume na msimamo wa kanisa
 
8D6U8671.JPG


Kikwete na Maarais wastaafu walivyojitahidi kumkumbatia Pengo katika nafasi yake ya anniversary ya uaskofu miaka 25 Dar na ndio maana amekuwa kimbilio la Kikwete kutoa matamkoa yanayoendana kinyume na msimamo wa pamoja wa kanisa katoliki, ndicho anachofanya askofu Ndimbo.

haya sasa mlifikiri kwa vile SLAA msaliti wa Kanisa alitokea huko basi Kanisa lingemkumbatia, la hasha
 
Maisha ya watanzania yamebadilika!aseme maisha yake ndiyo yamebadilika kutokana na ubinafsi,upuuzi alianzisha mwenyewe kwa kutoa maoni wakati muda Wa kutoa maoni ulishaisha,akaweka msimamo kuwa,serikali Tartu mpaka yeye aondoke madarakani,ila kuna kitu anahofia,nafikiri kuna watu nyuma yake wana mdrive
Ndugu, Are you BAVICHA!

Nadhani hufahamu kuwa hata kupewa uhuru wa kuweza kusema Rais Kikwete ni mpuuzi inaonyesha jinsi maisha yako yalivyobadilika. Kuna nyakati hukuweza kusema au kuandika maneno haya ndani ya nchi.

Uhuru ulionao kwa sasa wa kutafuta, kupokea, kuwa na maoni yoyote na kuyatoa nje kwa kupitia chombo chochote bila kujali mipaka ya nchi ni kioo kinachoonyesha kuwa maisha yamebadilika.
 
inasikitisha sana kuona askofu anafikra potofu katika hili, watanzania wezangu tunakwenda wapi? lakini mtu kama askofu hana dhiki na taabu na ndiyo maana anakashfu haki ya wasakatonge.
 
Mkuu Haya uliyonukuu ni majibu aliyotoa kuhusiana na Mwanaye kuhusishwa na madawa ya kulevya......majibu haya hupaswi kuyageneralize mpaka kwenye ishu hii nyeti ya katiba.......

Hivi UKAWA mnazo kweli? mnajua kabisa issue ya Katiba ni nyeti halafu mfanya utoto kiasi hicho?
 
Ndugu, Are you BAVICHA!

Nadhani hufahamu kuwa hata kupewa uhuru wa kuweza kusema Rais Kikwete ni mpuuzi inaonyesha jinsi maisha yako yalivyobadilika. Kuna nyakati hukuweza kusema au kuandika maneno haya ndani ya nchi.

Uhuru ulionao kwa sasa wa kutafuta, kupokea, kuwa na maoni yoyote na kuyatoa nje kwa kupitia chombo chochote bila kujali mipaka ya nchi ni kioo kinachoonyesha kuwa maisha yamebadilika.

Hawa CHADEMA wamechezea hii nchi vya kutosha ni wakati sasa rais ajae aone uhuru wa kuongea kwa wapuuzi kama hawa basi na awapige pini vya kutosha
 
Back
Top Bottom