Uchaguzi 2020 Askofu Mwamakula: Wito kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,015
WITO KWA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI KUKUTANA NA CHADEMA NA ACT WAZALENDO KUTATUA TATIZO LA KUENGULIWA KWA WAGOMBEA.

Tarehe 29 Agosti 2020, nimetoa wito kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kukutana na Uongozi wa CHADEMA na ACT Wazalendo kwa lengo la kuzungumza na kutatua tatizo la kuenguliwa kwa Wagombea wa Udiwani na Ubunge kupitia vyama hivyo kulikofanywa na Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi! Nimeitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutafakari kwa kina na kupima kwa uzito jambo hilo kuhusiana na suala zima la kutenda HAKI kwa mustakabali wa nchi kupitia Uchaguzi Mkuu wa 28 Oktoba 2020.

Nimeyasema hayo kama maneno ya utangulizi nilipokuwa natoa Sala katika Ufunguzi wa Kampeni za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Tundu Lissu katika Viwanja vya Tanganyika Packers vilivyoko Kawe jijini Dar es Salaam.

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Makanisa ya Moravian ya Uamsho Duniani
 
Penye haki itendeke haki. Ikikosekana kunakuwa na sintofahamu! Tanzania yetu imefikia hapa? Wapi tunaelekea wateuliwa msitupeleke huko!
 
Maaskofu wetu wa atoliku wanasubiri sadaka jumapili ijayo Kama ambavyo wamenywea bia sadaka zetu za jumapili hii.
 
Bila HAKI hakuna AMANI. Huko Zanzibar, Maalim Seif katika uzee na heshima yake amechoka kutotendewa HAKI na kusema "ukhanithi" huu sasa basi. Ukhanithi wenyewe ni wa Tume kupeleka Pemba wasimamizi wa uchaguzi kutoka bara na wote wakiwa ni maafisa wa Usalama wa Taifa.

Kazi yao ya kwanza ni kuwaondoa wagombea wote 18 wa ACT WAZALENDO. Wakati huohuo hata wagombea wenyewe wa CCM Pemba wanakana kwamba hawajawahi kuwawekea pingamizi lolote wagombea wenzao wa ACT WAZALENDO. Hivyo, ni amri toka juu. Hii si HAKI. AMANI haiwezi kupatikana. Tume ijitafakari. Wapemba hawataki tena ukhanithi.
 
Maaskofu wetu wa atoliku wanasubiri sadaka jumapili ijayo Kama ambavyo wamenywea bia sadaka zetu za jumapili hii.
Hata mashekh wa bakwata wameufyata
Hongera Shk Ponda kwa kuanika ukweli bila mawaa
Yeye kasha towa kauli yake kwenye Waraka na hivi karibuni.
Polisi wakamuona mbaya wakamkamata nakumuhoji.
 
Tume inayopokea maelekezo toka Lumumba - wasitutanie watanzania !! Hata mwalimu enzi zake hakuthubutu kujipitisha bila kupingwa badala yake aliweka picha yake na kivuli... walau kidogo afadhali...

hii ya kukata majina ni uhuni.....
 
Hongera sana baba MWAMAKULA kwa ujasiri wa kutetea HAKI hadharani! Ni HAKI ya KIRAIA kwa raia wote wa JMT wenye umri stahiki kila baada ya miaka 5 kupiga KURA kuchagua viongozi wao wa kisiasa wanao wapenda! Haiingii akilini Tume kuwalazimishia wananchi wa Jimbo/Kata fulani kiongozi asiye chaguo lao simply kwa sababu kapitishwa na kina Polepole & Bashiru kwenye chama chao!
 
Back
Top Bottom