Askofu Mwamakula: Tusilale usingizi pasipo kujua Moses Lijenje yupo wapi na ana hali gani

TAJIRI MKUU WA MATAJIRI

JF-Expert Member
Dec 1, 2010
5,722
10,226
TUSILALE USINGIZI PASIPO KUJUA MOSES LIJENJE YUKO WAPI NA ANA HALI GANI!

1666142825307.jpg


Kamanda Kingai na Afande Mahita katika nyakati tofauti kila mmoja akiwa chini ya kiapo, walitoa ushahidi Mahakamani kuwa walikuwa wakimtafuta mtuhumiwa Moses Lijenje kule Moshi. Lakini mmoja wa watuhumiwa hao (aliyesadikiwa kuwa pamoja na Moses Lijenje katika program ya VIP Protection ya Mbowe); akiongozwa na Mawakili wa Utetezi, ameieleza Mahakama mara kadhaa juu ya Moses Lijenje.

Shahidi (mtuhumiwa) huyo ameieleza Mahakama kuwa alipokuwa akiteswa, alitishwa na mmoja wa wasulubu (Polisi) wake huku akigusishwa bastola kichwani kuwa na yeye angelitupwa kama alivyotupwa Moses Lijenje bila kutaja alitupwaje na alitupwa wapi na kwa sababu gani. Kwa maneno mengine, wasulubu (Polisi) hao ndio 'walimtupa Moses Lijenje'!

Mambo mengine ni ya Jaji na Mahakama, sisi watetezi wa haki tuna jambo letu. Kama watetezi wa haki ni lazima tutake kujua Moses Lijenje yuko wapi na hali yake ikoje huko aliko. Kama kweli ametupwa, ametupwa na nani na kwa sababu gani na ametupwa wapi na hali yake ikoje huko aliko? Kutupwa huko kuna maana gani? Kesi hiyo inaweza kuchukua muda mrefu kuisha, lakini hiyo haituzuii sisi watetezi wa haki kutafuta kujua wapi aliko mtu anayeitwa Moses Lijenje na hali yake ikoje.

Kwa sababu hiyo, sisi Askofu Mwamakula tunatoa wito wa kila Mtanzania kufanya 'manhunt' yaani kuanza kumtafuta mtu aitwaye Moses Lijenje kuanzia muda huu. Jeshi la Polisi linao wajibu wa kuuambia umma ni wapi alipo ndugu Moses Lijenje! Paza sauti yako kwa kusema, kuandika na kusambaza ujumbe hadi uwafikie walio karibu na Lijenje, wanaomhifadhi, alikokimbilia au waliomtupa!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
 
Shahidi (mtuhumiwa) huyo ameieleza Mahakama kuwa alipokuwa akiteswa, alitishwa na mmoja wa wasulubu (Polisi) wake huku akigusishwa bastola kichwani kuwa na yeye angelitupwa kama alivyotupwa Moses Lijenje bila kutaja alitupwaje na alitupwa wapi na kwa sababu gani. Kwa maneno mengine, wasulubu (Polisi) hao ndio 'walimtupa Moses Lijenje'!
 
Hili suala la Lijenje lilipoa baada ya ile kesi ya Mbowe kwisha, jambo ambalo halikutakiwa kufanyika, ni kama vile tulichezewa "mind game" na CCM kuimaliza ile kesi haraka ili tumsahau Lijenje.

Ni wakati wa kupaza sauti ajulikane wapi alipo Lijenje, wale polisi watuhumiwa wa kumpoteza Lijenje wakamatwe na kuhojiwa.

Hata kama imeshathibitika polisi wetu hufanya kazi kwa maslahi ya CCM na kupandishwa vyeo, hili lisitukatishe tamaa kupaza sauti zetu ili ijulikane wapi alipo Moses.
 
Mwamakula anataffuta kick
Baada ya kuona watu wamempuuza na umaarufu wake kwisha
Kwanini kuna watu wanaitwa wajinga?
Ni kwa sababu wanawaza kijinga,wanaongea kijinga na wanaandika kijinga.
Moses ni kijana wa Kitanzania tena askari Jeshi shupavu na komandoo. Kwa nyakati tofauti ametetea maslahi ya nchi hii kwa kuhatarisha maisha yake binafsi bila hofu, jee unadhani wanajeshi wenzake na watu wema wanawadha nini kama huyo anapotea tena mikononi mwa vyombo vyetu vya usalama?
Angepotezwa Mwigulu au Makonda mngeishia kusema hajulikani alipo tuu?
Tunamtaka Moses sisi wananchi, na wale wenzake wanamtaka mwenzao!
 
Shahidi (mtuhumiwa) huyo ameieleza Mahakama kuwa alipokuwa akiteswa, alitishwa na mmoja wa wasulubu (Polisi) wake huku akigusishwa bastola kichwani kuwa na yeye angelitupwa kama alivyotupwa Moses Lijenje bila kutaja alitupwaje na alitupwa wapi na kwa sababu gani. Kwa maneno mengine, wasulubu (Polisi) hao ndio 'walimtupa Moses Lijenje'!
Nchi inahitaji maridhiano ya Kitaifa ambapo ninaona kana kwamba watawala wanaamini maridhiano na vyama pinzani ndiyo maridhiano ya kitaifa.

Linjenje ni mmoja kati ya maelfu ya waliopotezwa ktk mazingira tatanishi. Wale wafanyabiashara waliouwawa enzi ya Zombe hawakuwa wanasiasa, yale mauaji ya Mtwara ya yule mfanyabiashara hayakuwa ya kisiasa. Watuhumiwa wanaofia mikononi mwa polisi wengi si wanasiasa. Watu wanaobambikiziwa kesi za ajabuajabu ni maelfu, vijana kukosa elimu kwa sababu ya pesa za kuwekeza kwenye elimu kufisadiwa na viongozi ni janga kubwa kubwa, vijana wanaokosa alama za ufaulu na kuachwa holela mitaani bila mikakati ya kuwaendeleza ni janga lingine baya chini ya jua

Maridhiano ya Kitaifa ni zaidi anavyofikiria mama Samia na CCM yangu. Tuna makosa mengi tumewafanyia Watanzania ni lazima tukae chini kuridhiana na wananchi maisha yabadilike.
 
1. Haya jamani! Tuanzie hapa. Tuwatafute Nduguze/familia yake/marafiki zake watueleze alipoteaje na alituhumiwa na nani!?
2. Vyombo vya dola (polisi) wanaobugia kodi zetu wakitamba kulinda wananchi na mali zao watueleze huyu raia wa Tz yuko wapi?
3. Yule polisi mtesaji aliyetoa kauli hiyo ashtakiwe aeleze walimtupa wapi na kwa nini.
 
Back
Top Bottom