Dalton elijah
JF-Expert Member
- Jul 19, 2022
- 780
- 1,831
Ndugu Watanzania!
Kama mtakumbuka, Rais Samia aliunda Tume ya Uchunguzi kuhusu machafuko ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Siku ya Jumamosi tarehe 17 Januari 2026, Mhashamu Baba Askofu Mwamakula aliletewa barua iliyotoka Tume ya Rais ya Kuchunguza Matukio Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 yenye wito rasmi kumuomba yeye kushiriki katika kutoa maoni mbele yake.
Barua hiyo yenye viambata vya hadidu za rejea inamuomba Askofu Mwamakula ili "kukutana na Tume kwa majadiliano yatakayofanyika tarehe 22 Januari 2026, Saa 5:30 asubuhi katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Dar es Salaam."
Baada ya kupokea mwaliko huo alijadiliana na washauri wake wakiwemo wanasheria. Askofu alipata nafasi ya kuutafakari kwa kina wito huo. Lakini baada ya tafakuri hiyo imependeza Baba Askofu kuwajulisha Watanzania kuhusu uwepo wa wito huo na maamuzi aliyoyafikia. Tafakuri yake iiliyopelekea kufikiwa kwa maamuzi yake imejengwa hasa katika misingi mikuu saba (7):
1. Tume hiyo iliteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan ikiwa na malengo yanayotajwa.
2. Rais Samia ndiye ambaye ametuhumiwa na Watanzania walio wengi kuwa kwa amri yake na maelekezo yake kama Amiri Jeshi Mkuu, vyombo vya dola vilitekeleza mauaji ya halaiki yaliyofanywa tarehe 29 - 31 Oktoba 2025.
3. Mhashamu Baba Askofu Mwamakula yuko katika kumbukumbu (he is on records) kupitia ukurasa wake wa Facebook na kupitia vyombo vya habari ambavyo vilifanya naye mahojiano maalum (an exclusive interview) kwani aliweka hadharani msimamo wake kuhusu Tume hiyo pamoja na mamlaka iliyoiteua.
4. Msimamo wa Askofu Mwamakula kuhusu Tume hiyo ni kuwa Tume haiwezi kuwa huru kwani inakwenda kuchunguza mambo ambayo yanamhusu pia mtu aliyeiteua.
5. Msimamo mwingine wa Askofu Mwamakula juu ya mamlaka ya uteuzi wa Tume hiyo pia ni; kwa kuwa Rais Samia ndiye mtu aliyetuhumiwa kutoa amri kwa vyombo vya dola kama Amiri Jeshi Mkuu, iliyovifanya vyombo kuyatekeleza mauaji hayo; Rais Samia amekosa mamlaka ya kimaadili (moral authority) ya kuunda Tume hii ambayo kimsingi inakwenda 'kumchunguza pia yeye mwenyewe'.
6. Pamoja na ukweli kuwa Rais anayo mamlaka kisheria ya kuunda Tume yeyote, lakini ukweli wa mantiki kuhusu upatikanaji wa haki tangu asili unaibatilisha mamlaka ya kisheria ambayo ilipungukiwa au ilikosa mamlaka ya kimaadili. Kwa hiyo mamlaka hiyo ya kisheria iliyokosa pia mamlaka ya kimaadili inakosa uhalali wa kutekeleza jambo lo lote likakubalika na jamii.
7. Rais Samia hakuwahi kutoa kauli hadharani ili kujitenga na vitendo vya mauaji hayo, badala yake yeye alisikika na kunukuliwa mara kadhaa na vyombo vya habari akitoa kauli ambazo kwa namna moja ama nyingine (implicitly) ambavyo vinaonyesha kuwa ama aliviunga mkono ama alivipongeza vyombo vya dola kwa kutekeleza mauaji hayo.
8. Swali la ambalo askofu anajiuliza ni kuwa; je, ni vipi vyombo vya dola ambavyo vilipongezwa au viliungwa mkono hadharani na Amiri Jeshi Mkuu vitaweza kuchunguzwa na Tume hiyo iliyoundwa na yeye ambapo kimsingi sehemu ya tuhuma hizo zinaelekezwa kwake yeye na pia kwa vyombo hivyo? Je, uhuru wa Tume hiyo unaegemea katika nguzo gani?
Kwa sababu hiyo kutokana na hoja hizo nane (7) hapo juu, Askofu Mwamakula anaihifadhi (the bishop is withholding) haki yake ya kutoa maoni katika Tume ye yote hadi pale ambapo Watanzania walio wengi watakapokubaliana kuwa Tume husika iko huru na haijateuliwa na mtuhumiwa! Kwa hiyo, Askofu Mwamakula hatafika kukutana na Tume katika tarehe tajwa na hata tarehe yeyote itakayotajwa baadaye na Tume hiyo.
Askofu Mwamakula hana shida yeyote binafsi na wajumbe wa Tume kwani miongoni mwao wako anaowaheshimu na wao wanamheshimu. Shida ya askofu kwa mamlaka ya uteuzi (Rais Samia) pia siyo ya mambo binafsi. Ila kikwazo kikubwa kwa askofu ni juu ya uhuru na uhalali wa kimaadili wa Tume hiyo.
Askofu Mwamakula anafungwa katika kifungo cha haki kinachomtaka yeye pia kama askofu asione soni (haya) kusimamia mambo yaliyo ya msingi kwa kuogopa mamlaka. Siku zote katika wito huu wa kiaskofu, askofu anakuwa sauti ya dhamiri katika jamii akiiwakilisha dhamiri kuu. Watu wengine wanaoogopa kuisema kweli kwa kuogopa kifo, askofu ndiye anatakiwa kuinuka na kuisema hiyo kweli.
Ni wazi, Askofu hawezi kushiriki kutoa maoni katika Tume ambayo kwa maoni yake anaamini kuwa haiwezi kuleta taarifa itakayomtia hatiani mtu aliyeiteua au ina 'maelekezo maalumu ya kuhalalisha' maamuzi fulani yaliyoamriwa juu ya kile kinachochunguzwa! Tume ambayo watu walio wengi hawaitambui itakuwa ni usaliti wa hali ya juu kwa askofu kuipa uhalali kwa kufika mbele yake!
Baba Askofu anajua ya kuwa baadhi ya watu katika mamlaka hawatapendezwa na muitikio wake. Hivyo, Askofu anajimimina kwake yeye aliyemwita katika wito huu mkuu wa kitume na ambaye anamtaka kila anayetumikia wito huu asiogope kuusema ukweli kwa ajili ya kuokoa watu wengine wasiangamie (Ezekieli 33:1-20).
Askofu anamshukuru pia Mwenyekiti wa Tume kwa kumuona kuwa miongoni mwa watu walio na stahili ya kufika mbele yake. Hata hivyo, hoja alizotoa askofu zinamfanya aihifadhi haki yake ya kutoa maoni hadi pale ambapo dhamiri yake itamuonyesha kuwa Tume husika iko huru na pia imeundwa na mtu ambaye hajalaumika na umma kwa kuwa inachunguza mambo ya taifa!
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Itunge, Dar es Salaam; 19 Januari 2026; Saa 2:20 jioni.
Kama mtakumbuka, Rais Samia aliunda Tume ya Uchunguzi kuhusu machafuko ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Siku ya Jumamosi tarehe 17 Januari 2026, Mhashamu Baba Askofu Mwamakula aliletewa barua iliyotoka Tume ya Rais ya Kuchunguza Matukio Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 yenye wito rasmi kumuomba yeye kushiriki katika kutoa maoni mbele yake.
Barua hiyo yenye viambata vya hadidu za rejea inamuomba Askofu Mwamakula ili "kukutana na Tume kwa majadiliano yatakayofanyika tarehe 22 Januari 2026, Saa 5:30 asubuhi katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Dar es Salaam."
Baada ya kupokea mwaliko huo alijadiliana na washauri wake wakiwemo wanasheria. Askofu alipata nafasi ya kuutafakari kwa kina wito huo. Lakini baada ya tafakuri hiyo imependeza Baba Askofu kuwajulisha Watanzania kuhusu uwepo wa wito huo na maamuzi aliyoyafikia. Tafakuri yake iiliyopelekea kufikiwa kwa maamuzi yake imejengwa hasa katika misingi mikuu saba (7):
1. Tume hiyo iliteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan ikiwa na malengo yanayotajwa.
2. Rais Samia ndiye ambaye ametuhumiwa na Watanzania walio wengi kuwa kwa amri yake na maelekezo yake kama Amiri Jeshi Mkuu, vyombo vya dola vilitekeleza mauaji ya halaiki yaliyofanywa tarehe 29 - 31 Oktoba 2025.
3. Mhashamu Baba Askofu Mwamakula yuko katika kumbukumbu (he is on records) kupitia ukurasa wake wa Facebook na kupitia vyombo vya habari ambavyo vilifanya naye mahojiano maalum (an exclusive interview) kwani aliweka hadharani msimamo wake kuhusu Tume hiyo pamoja na mamlaka iliyoiteua.
4. Msimamo wa Askofu Mwamakula kuhusu Tume hiyo ni kuwa Tume haiwezi kuwa huru kwani inakwenda kuchunguza mambo ambayo yanamhusu pia mtu aliyeiteua.
5. Msimamo mwingine wa Askofu Mwamakula juu ya mamlaka ya uteuzi wa Tume hiyo pia ni; kwa kuwa Rais Samia ndiye mtu aliyetuhumiwa kutoa amri kwa vyombo vya dola kama Amiri Jeshi Mkuu, iliyovifanya vyombo kuyatekeleza mauaji hayo; Rais Samia amekosa mamlaka ya kimaadili (moral authority) ya kuunda Tume hii ambayo kimsingi inakwenda 'kumchunguza pia yeye mwenyewe'.
6. Pamoja na ukweli kuwa Rais anayo mamlaka kisheria ya kuunda Tume yeyote, lakini ukweli wa mantiki kuhusu upatikanaji wa haki tangu asili unaibatilisha mamlaka ya kisheria ambayo ilipungukiwa au ilikosa mamlaka ya kimaadili. Kwa hiyo mamlaka hiyo ya kisheria iliyokosa pia mamlaka ya kimaadili inakosa uhalali wa kutekeleza jambo lo lote likakubalika na jamii.
7. Rais Samia hakuwahi kutoa kauli hadharani ili kujitenga na vitendo vya mauaji hayo, badala yake yeye alisikika na kunukuliwa mara kadhaa na vyombo vya habari akitoa kauli ambazo kwa namna moja ama nyingine (implicitly) ambavyo vinaonyesha kuwa ama aliviunga mkono ama alivipongeza vyombo vya dola kwa kutekeleza mauaji hayo.
8. Swali la ambalo askofu anajiuliza ni kuwa; je, ni vipi vyombo vya dola ambavyo vilipongezwa au viliungwa mkono hadharani na Amiri Jeshi Mkuu vitaweza kuchunguzwa na Tume hiyo iliyoundwa na yeye ambapo kimsingi sehemu ya tuhuma hizo zinaelekezwa kwake yeye na pia kwa vyombo hivyo? Je, uhuru wa Tume hiyo unaegemea katika nguzo gani?
Kwa sababu hiyo kutokana na hoja hizo nane (7) hapo juu, Askofu Mwamakula anaihifadhi (the bishop is withholding) haki yake ya kutoa maoni katika Tume ye yote hadi pale ambapo Watanzania walio wengi watakapokubaliana kuwa Tume husika iko huru na haijateuliwa na mtuhumiwa! Kwa hiyo, Askofu Mwamakula hatafika kukutana na Tume katika tarehe tajwa na hata tarehe yeyote itakayotajwa baadaye na Tume hiyo.
Askofu Mwamakula hana shida yeyote binafsi na wajumbe wa Tume kwani miongoni mwao wako anaowaheshimu na wao wanamheshimu. Shida ya askofu kwa mamlaka ya uteuzi (Rais Samia) pia siyo ya mambo binafsi. Ila kikwazo kikubwa kwa askofu ni juu ya uhuru na uhalali wa kimaadili wa Tume hiyo.
Askofu Mwamakula anafungwa katika kifungo cha haki kinachomtaka yeye pia kama askofu asione soni (haya) kusimamia mambo yaliyo ya msingi kwa kuogopa mamlaka. Siku zote katika wito huu wa kiaskofu, askofu anakuwa sauti ya dhamiri katika jamii akiiwakilisha dhamiri kuu. Watu wengine wanaoogopa kuisema kweli kwa kuogopa kifo, askofu ndiye anatakiwa kuinuka na kuisema hiyo kweli.
Ni wazi, Askofu hawezi kushiriki kutoa maoni katika Tume ambayo kwa maoni yake anaamini kuwa haiwezi kuleta taarifa itakayomtia hatiani mtu aliyeiteua au ina 'maelekezo maalumu ya kuhalalisha' maamuzi fulani yaliyoamriwa juu ya kile kinachochunguzwa! Tume ambayo watu walio wengi hawaitambui itakuwa ni usaliti wa hali ya juu kwa askofu kuipa uhalali kwa kufika mbele yake!
Baba Askofu anajua ya kuwa baadhi ya watu katika mamlaka hawatapendezwa na muitikio wake. Hivyo, Askofu anajimimina kwake yeye aliyemwita katika wito huu mkuu wa kitume na ambaye anamtaka kila anayetumikia wito huu asiogope kuusema ukweli kwa ajili ya kuokoa watu wengine wasiangamie (Ezekieli 33:1-20).
Askofu anamshukuru pia Mwenyekiti wa Tume kwa kumuona kuwa miongoni mwa watu walio na stahili ya kufika mbele yake. Hata hivyo, hoja alizotoa askofu zinamfanya aihifadhi haki yake ya kutoa maoni hadi pale ambapo dhamiri yake itamuonyesha kuwa Tume husika iko huru na pia imeundwa na mtu ambaye hajalaumika na umma kwa kuwa inachunguza mambo ya taifa!
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Itunge, Dar es Salaam; 19 Januari 2026; Saa 2:20 jioni.