Askofu Kakobe pitia hapa

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,603
29,743
Leo ni siku ya Jumapili siku ya Bwana kwa sisi wenye imani ya Kikristo, hasa born again.

Nimetoka zangu kigamboni, nikavuka maji nikiwa na dhamira ya kupata Neno lisilogoshiwa kwenye huduma ya Full Gospel Bible Fellowship Churh pale Mwenge. Niliambatana na mke wangu.

Lengo langu ni kupata Neno ili niweze kuimarika kiimani na kujitathmin kama nipo raiti traki kwenda Mbinguni.

Naelewa sana Huduma ya Kakobe, mimi ni miongoni mwa waanzilishi enzi hizo miaka 1984 kisha alipotengana na Rodrick Mmbwambo kutoka The Gospel Evangilical Team (GET) mwaka 1988 kupelekea kuanzishwa kwa kanisa la FGBF pale Mwenge jirani na kanisa Katoliki kabla halijahamia Jamhuri Primary School mjini.

Naelewa msimamo wa kanisa lake. Naelewa viwango vya mahubiri alivyo navyo.

Nilichostuka leo ni kwamba, kutoka kwenye viwango imeelekea kuwa kwenye xtremely faith. Imani kali. Mke wangu alifika kanisani pamoja nami akiwa amevaa nguo inayositiri vyema na kilemba kama kawaida ya taratibu za kanisa lake. Neno la leo lilikuwa ni MAVAZI YA MTU ALIYEOKOKA. Neno lilipoanza nikaaona mke anainuliwa na mama mmoja mhudumu na wakatoka nje. Baada ya dakika tano mama yule akanifuata akisema mke wangu ananiita nje. Nikamuuliza kuna tatizo? Akanijibu yes, amesuka rasta na pale hawaruhusiwi waliosuka rasta kwa sababu ni nywele feki.

Nilitoka nje nikamchukua mke wangu na kuondoka. Alijiona mkosaji nikamwambia kuwa Yesu wetu alikaa na wenye dhambi hakuwabagua lakini sisi ambao ndiyo wanafunzi wake tumevuka viwango kiasi kwamba inakupasa ujitakase kwanza kabla ya kutakaswa na Yesu.

Wakati naingia nilishuhudia baadhi ya waumini wakiingia wakiwa na nguo ambazo hazina viwango na wengine unaona kabisaa wamejichubua ngozi.

Kwa namna nifahamuvyo ni kwamba ili mtu abadilike anahitaji kufundishwa Neno ili hiyari yake ifikie maamuzi ya mabadiliko. Pia kuzuia watu wasiingie kanisani kwa sababu ya kutokidhi vigezo vya kanisa ni kuwabagua na kuwatenga na Kristo kwa sababu haiwezekani mtu asiyeamini akaanza kufuata masharti ya kanisa kama hajafikiwa na Neno.

Jambo lingine ninalojiuliza kwa waamini wenzangu humu ni kwamba, ikiwa fedha, almasi na dhahabu ni mali ya Mungu na havijatajwa kama ni sehemu ya dhambi, je Kibiblia mali hizo zinatumikaje kwa utukufu wake? Watu wanazitaja kwenye mafundisho lakini hata kuvaa kidani au pete za vitu hivyo ni dhambi?

Leo sijamuabudu Mungu kwa kuwa nimenyimwa fursa hiyo.
 
Ni sawa kabisa. Maana kwenye misikiti yetu hakuna mtu asiyetawaza akaingia.
Tofauti kubwa sana baina ya Kanisa na Islam.

Kumbuka kwamba huko kutawadha ni sharti muhimu kwa kila Islam kabla ya ibada na ni tendo la kisheria.

Nipe mstari unaokataza mwanamke kutoingia ibadani kwa sababu ya kusuka rasta.

Imeandikwa kwamba Mwanamke anapoHUTUBU yaani anaposimama kwenye mimbari kuhubiri lazima afunike kichwa kwa sababu ya ishara ya kumilikiwa.

Lakini tunapofika mbele za Mungu ambaye Mwana wake alikuwa karibu na wenye dhambi ili awaokoe tunapaswa kuomba kutakaswa ndani kwanza kabla ya mambo ya mwilini.
 
Mavazi ni mapokeo tu hayana uhuaiano wowote na usafi wa ndani.
Tujiulize kuwa wale waliovaa ngozi kipindi kile hawakuwa na haki ya kuitwa watu wa Mungu?
Watu walitembea vifua wazi tena wanawake
Pascal Mayalla aliwahi kumuhoji Kakobe akamuuliza zile cheni za dhahabu unazochukuaga za waumini hua unazipeleka wapi?Kakobe aliwaka mbaya kabisaaaaaa.
 
Mkuu poleni sana, usiseme haauja abudu leo, ile tu kudhamiria kwenda kanisani leo na kule kutekeleza hio dhamira kwa kujiandaa kupanda gari mpaka sehemu ulikodhamiria kukutana na Mungu ni ibada tosha.

Kwa hizo kanuni za hilo kanisa nisiseme kitu maana sio wao tu wenye kanuni ambazo sio za kiroho bali ni karibu makanisa yote, maadamu umeshajua matwakwa yao yatekeleze kama unaona hapo ndio sahihi ama achana nao yafuta mahali pengine unapoona panafaa ama panalingana na amani ya moyo wako.

Lakini ni heri ungerudia tu lile kanisa la asili na kuachana na haya yaliotokea tu hivi karibuni. Laiti kama hayo makanisa ya asili yasingekuayana faa yasingslipewa kibali cha kulitunza neno la Mungu toka enzi hizo mpaka ujio wa makanisa haya mapya yanayokosoa vikali uwepo wa makanisa ya asili.
 
Msanii,

Mwambie Kakobekuna ndege nyingine zinakuja ajiandae kwenda kuzipokea.

Mwambie pia hatujui Azory Gwanda yuko wapi.

Ben Saanane yuko wapi hatujui.

Tundu Lissu kafanyiwa ukatili kama kama chatu.

Hayo mambo yote yana baraka za Jiwe.

Na kwanini hayo makanisa yao hayatoi hata msaada wa gunia la mahindi kwa watoto yatima
 
Mwambie Kakobekuna ndege nyingine zinakuja ajiandae kwenda kuzipokea.

Mwambie pia hatujui Azory Gwanda yuko wapi.

Ben Saanane yuko wapi hatujui.

Tundu Lissu kafanyiwa ukatili kama kama chatu.

Hayo mambo yote yana baraka za Jiwe.

Na kwanini hayo makanisa yao hayatoi hata msaada wa gunia la mahindi kwa watoto yatima
Siyo lengo la post
 
Mkuu poleni sana, usiseme haauja abudu leo, ile tu kudhamiria kwenda kanisani leo na kule kutekeleza hio dhamira kwa kujiandaa kupanda gari mpaka sehemu ulikodhamiria kukutana na Mungu ni ibada tosha.

Kwa hizo kanuni za hilo kanisa nisiseme kitu maana sio wao tu wenye kanuni ambazo sio za kiroho bali ni karibu makanisa yote, maadamu umeshajua matwakwa yao yatekeleze kama unaona hapo ndio sahihi ama achana nao yafuta mahali pengine unapoona panafaa ama panalingana na amani ya moyo wako.

Lakini ni heri ungerudia tu lile kanisa la asili na kuachana na haya yaliotokea tu hivi karibuni. Laiti kama hayo makanisa ya asili yasingekuayana faa yasingslipewa kibali cha kulitunza neno la Mungu toka enzi hizo mpaka ujio wa makanisa haya mapya yanayokosoa vikali uwepo wa makanisa ya asili.
Kumbuka mtu anayekwenda mara ya kwanza anazuiwa kusikia Neno ili abadilike bali analazimika kubadilika kwanza ili asiki Neno
 
Pole kwa masahibu nenda tena ukiwa na viwango tofauti kuonyesha imani zaidi bila kukata tamaaa wahudumu ninwanadamu kuna wakati wanazidi au kupungua Kwenye kutekeleza maagizo
Imani na kutii Neno hufanyika kwa hiyari.

Mru asikilize kisha akionekana ni mgumu kwenda na viwango mnamtapika
 
Back
Top Bottom