Ilikuwa katika ibada ya pasaka ambapo askofu Gwajima akielezea habari ya kupoteza fahamu. Miguu yake ilitetemeka, akasikika akiwaomba wachungaji wake wamshike mkono wa kuume, akisema nataka kutembea, Yesu nimechoka kukalia kiti cha vilema, heri kufa kuliko kukaa hapo. Nimefufua wafu na kuponya wagonjwa siwezi mimi kukaa hapo. Mara akasema, nasikia sauti inasema 'mimi nimeushinda ulimwengu' akaendelea 'roho wa mungu yu juu yangu' ilikua ni jambo la kupendeza sana, Bishop akaanza kutembea mwenyewe. Hallelujah