Askofu Gwajima amtetea Lowassa

Askofu Gwajima amtetea Lowassa

wote wenye chuki na lowassa mtahaha sana mwaka huu. nani msafi ccm wa kusema anafaa kuwa raisi? hata kama lowassa ni fisadi hategemei hizo pesa. na angekuwa anategemea ufisadi siku nyingi hizo pesa zingeshaisha. acheni unoko maana lowassa ni raisi na itawauma sana.
Tuondolee ujonga hakuna anayemchukia lowasa ila tunachukia ufisadi wake.
 
Nshajua ile helcopta kumbe alinunu lowassa ndo kampa gwajima ili wajikosheee
Endeleeni kutumia pesa chafu
Watanzania tumeskut tuu tunausoma mchezoo
 
Sijui kashamwacha yule mwimbaji wa nyimbo za Injili.Halafu kuna ile scandal ya kuzaa na mke wa mtu Dr fulani sijui kesi imemalizika au imechinjiwa baharini.

Utapata dhambi maana naona unachanganya madesa na ata ulichoandika nina shaka kama unakifaham
 
Gwajima ni jembe. Kumbe anajua penye udhia tia rupia. Mambo ya fedha.
Japo kaongea hii kauli ni ujanja tu. Hapa ana mtu wake ambaye moyoni anamuunga mkono na anataka waumini waone anakowaelekeza. Kama sivyo hakuwa na haja ya kutufahamisha angewaacha wanasiasa wapakane matope ili upinzani ushike dola. Hataki kukemea rushwa Bali.anaunga mkono kimugongoMugongo. Hataki watanzania tujue mbivu na mbichi ni ipi. Hajui hao wanaotumia pesa ndio watakuja kutudai siku moja.
 
Ninawaza tu hapa kwa sauti! Inaelekea kwamba CCM imebadilika sana nyakati hizi za Kikwete!!?? Hivi kazi ya kujenga mtandao ni ya mtu binafsi, au ni ya Chama? Hivi mgombea Urais kutoka Chama Cha Mapinduzi, ni mgombea binafsi, au ni mgombea wa Chama? Je, Mwinyi na Mkapa waliijenga binafsi mitandao yao, au ni Chama Cha Mapinduzi kilichowajengea mitandao yao? Je, Mwinyi na Mkapa, ni nani aliyewalipia ada za fomu zao?
 
Leo nimeona gazeti moja likimzungumzia Askofu huyu mwenye kanisa la watu nyomi mno..kuwa akielezea maswala yanayo ligusa taifa ila nilichoshangaa ni kwamba kichwa cha habari kilivyowekwa ni kama yeye mwenyewe ndie anaetaka kugombea urais yasni nilochoka sn yule jamaa haogopi amewachana wezi wa escro live....daaaa big up gwajima askofu
 
ndo umemaliza au bado unaandika mkuu? Habari haijakamilika ulipaswa useme alichosema gwajima sio kuiacha habari hewani ivi sio kila mtu kaliona hilo gazeti
 
1. kwanza kabisa Gwajima sio Askofu. Gwajima ni Pastor.
2. Unapoleta habari jiandae vizuri, upange mawazo yako, na uamue juu ya kusudi lako la kuleta habari husika. Maana hueleweki kama unaripoti alichosema Gwajima, kilichoandikwa kwenye gazeti au unaripoti ulivyosoma gazeti likakufurahisha???
Zingatia haya: kwanza unaandika habari husika na baada ya hapo ndio unaandika maoni yako (kama unayo au unaandika hisia na vionjo). Tafadhali next time jiandae vizuri
 
Zunguken kote, semen yote, kura yangu nitampatia lowassa, asiposimama kugombea ntawapatia Ukawa kura yangu
 
Sijui kashamwacha yule mwimbaji wa nyimbo za Injili.Halafu kuna ile scandal ya kuzaa na mke wa mtu Dr fulani sijui kesi imemalizika au imechinjiwa baharini.
a cha majungu unauhakika na haya ulioandika jadili key topic sio unarukaruka
 
Usimseme gwajima vby wakati huujui ukweli wake kiundani
 
Wewe unaonekana hata gazeti hujasoma au umesimuliwa, pili upate nafasi ya karibu kumfuatilia Askofu Gwajima, nadhani katika Taifa hili kwa sasa ndiye kiongozi wa dini anayeongoza kwa kukemea wezi, mafisadi, wala rushwa na kila aina ya uovu unaofanywa na serikali.. Askofu Gwajima pekee katika pita pita zangu niliwahi kumsikia akiwataja wezi wa mali za umma na kuwataka wajiwajibishe na wakigoma wawajibishwe tena sio tu kwa kuvuliwa nyadhifa zao bali kwa kurudisha mali walizoziibia taifa hili kwa miaka mingi.

Ukisoma gazeti vizuri, mwandishi ameweka wazi maneno mafupi aliyonukuu toka kwa Askofu, na pia ni jambo la wazi lisilopingika kuwa hakuna njia kuelekea urais pasipo kutumia fedha, huitaji elimu ya ngazi ya phD kufahamu jambo hili. Kwani kinachomtesa Kikwete leo hii ni nini? Kulipa fadhila kwa pesa alizotumia kabla ya kuteuliwa na chama, wakati wa kuteuliwa, baada ya kuteuliwa, kabla ya kampeni na wakati wa kampeni. Kuunda mitandao ya ushindi mambo yote haya hugharimu pesa, tatizo linakuja ni kuwa, "Je, Pesa unazotumia ni pesa halali??" Pia, kwa historia ya Askofu Gwajima angeishakuwa kiongozi huyu tena hata Mbunge kutokana na ushawishi wake kwa watu wengi hapa nchini ila kwakua si mtu wa tamaa na ameweka mbele maslahi ya imani na kazi ya Mungu anayoiyofanya... Kipindi yupo Ubungo kiongozi huyu wa dini angegombea Ubunge asingeshindwa kupitia CCM na yawezekana kukataa kwake ndio sababu ya yeye kuondolewa pale Ubungo kwani alikosesha CCM jimbo.

Wacha ukweli usemwe wazi kabisa, Ni Askofu gani au kiongozi gani wa dini alishakemea serikali juu ya ujenzi wa Misikiti/Makanisa katika public service centres zaidi ya Gwajima??
Truth must be told openly, tuache ushabiki wa kishamba... soma gazeti kwa umakini wacha kukurupuka.
 
Utakoma wewe mwenywewe. Basi wewe ambaye si fisadi gombea urais, hata uenyekiti wa mtaa. Ujinga mtupu zilizojaa hila ndani yake.
 
Back
Top Bottom